EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 5, 2013

Israel ilihusika na shambulio la Syria?

Israel imeonyesha ishara kwamba ilifanya mashambulizi ya anga nchini Syria wiki iliyopita, huku Rais Bashar al-Assad akilituhumu taifa hilo la Kiyahudi kwa kujaribu kuidhoofisha nchi yake ambayo inakumbwa na vita.
 Waziri wa Ulinzi wa Israel, Ehud Barak
Israel imeonyesha ishara japo sio wazi kwamba ilifanya mashambulizi ya anga nchini Syria juma lililopita, huku Rais Bashar al-Assad akilituhumu taifa hilo la Kiyahudi kwa kujaribu kulidhoofisha taifa lake hilo ambalo linakumbwa na vita.
Siku nne baada ya Syria kudai kuwa Israel inahusika na shambulio la anga katika kituo cha utafiti wa kijeshi karibu na mji mkuu wa Damascus, Waziri wa Ulinzi wa Israel, Ehud Barak, amezungumza na waandishi wa habari mjini Munich, Ujerumani, lakini ameshindwa kuthibitisha kwamba Israel inahusika na shambulio hilo.

Kiongozi wa Hizbollah, Hassan Nasrallah  
                                             Kiongozi wa Hizbollah, Hassan Nasrallah
Barak jana aliwaambia wanadiplomasia wa ngazi za juu na maafisa wa masuala ya ulinzi katika mkutano wa usalama mjini Munich kwamba hicho kilikuwa ni kithibitisho kwamba wanaposema kitu huwa wanamaanisha. Israel haijathibitisha rasmi kuhusika na shambulio hilo, ingawa imekuwa ikizituhumu Iran na Syria kwa kulipatia silaha kundi la Hizbollah ambalo lilipambana na Israel katika vita vya mwezi mmoja mwaka 2006. Barak amesema hawadhani kama Syria inaruhusiwa kupeleka silaha za kisasa Lebanon.
 
Syria yatishia kulipiza kisasi
Syria imetishia kulipiza kisasi kutokana na mashambulizi hayo yaliyofanywa Jumatano iliyopita. Waziri Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan mkosoaji mkubwa wa Assad na Israel ameituhumu Israel kwa kuendeleza hali ya ugaidi ambapo amelaani shambulio hilo la anga akisema halikubaliki na linakiuka sheria za kimataifa na amekiita kitendo hicho ni uchokozi wa kigeni. Aidha, ameikosoa Iran kwa kuiunga mkono Syria.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Ali Akbar Salehi  
                              Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Ali Akbar Salehi
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Ali Akbar Salehi amesema amepokea kwa furaha uamuzi wa kiongozi wa muungano wa upinzani wa Syria Moaz al-Khatib kufanya mazungumzo na serikali ya Assad. Siku ya Jumamosi, Khatib alikutana na Salehi pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, mjini Munich. Ama kwa upande wa mpango wake wa nyuklia, Salehi amesema Iran iko tayari kufanya mazungumzo na Marekani kuhusu mpango huo, baada ya Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden kutoa ahadi ya kufanyika kwa mazungumzo hayo. Amesema wako tayari kuzungumza lakini lazima wahakikishe upande mwingine mara hii unkuja na nia halisi ya mazungumzo.
Ndani ya Syria kwenyewe watu wapatao 16 wameuawa miongoni mwao wakiwa watoto 10 na kamanda wa waasi, katika shambulio la kombora lililofanywa na jeshi la Syria kwenye mji wa Aleppo jana Jumapili. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa shirika la kusimamia haki za binaadamu la Syria lenye makao yake mjini London, Uingereza. Shirika hilo limesema kiasi watu 125 wameuawa jana Jumapili katika ghasia kuzunguka nchi nzima, miongoni mwao wakiwemo waasi 58.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate