EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 8, 2013

JK aionya Nida utoaji vitambulisho

RAIS Jakaya Kikwete ameitaka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida)kuhakikisha inaendesha zoezi la utambuzi wa watu kwa uhakika na makini akisema kuwa, hali yoyote itayosababisha kutolewa kwa vitambulisho katika mazingira ya ujanja inaweza kuwagharimu watumishi wa mamlaka hiyo.
 
Kwa upande mwingine, Rais Kikwete jana alikabidhiwa rasmi kitambulisho chake cha taifa na hivyo kuwa miongoni mwa Watanzania wa kwanza kukabidhiwa. Wengine waliokabidhiwa vitambulisho vyao ni pamoja marais wastaafu wa awamu ya pili na ile ya tatu, Makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Aman Abeid Karume.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mfumo wa usajili na utambuzi kwa wa watu na utoaji vitambulisho vya taifa, Rais Kikwete alionya juu ya utoaji vitambulisho kwa watu wasiostahili na kusema kwamba Serikali yake haitavumilia kuona hali hiyo ikitendeka.
Alisema suala la vitambulisho vya taifa ni nyeti na linapaswa kuendeshwa kwa kufuata miiko na sheria za nchi, hasa kwa kuzingatia kuwa vitambulisho hivyo vitatumika wakati wa uchaguizi mkuu ujao.

“ Katika hili sitakuwa na mswalie mtume, maana kama kuswalia tulifanya hivyo kabla ya kuwapatia kazi hii. Nataka muendeshe mambo kwa kuzingatia miiko na sheria, sitaki kuona mtu asiye raia wa Tanzania halafu anapatiwa kitambulisho cha uraia.” Alisema Rais Kikwete na kuongeza kuwa .

“ Yale tunayoyashuhudia kwenye uhamiaji, sitaka yajitokeze tena huku maana siku hizi ‘passport’ yetu (hati ya kusafiria) inatolewa ovyo ovyo mitaani”
Kuanza kutolewa kwa vitambulisho hivyo vya taifa, kunakamilisha ndoto ya miaka mingi iliyoasisiwa wakati wa utawala wa awamu ya kwanza na baadaye kuendelea hadi awamu hii ya nne.

Vitambulisho vya taifa vinatazamiwa kusaidia maeneo ya ulinzi na usalama, kutumika kama kitambulisho rasmi wakati wa uchaguzi mkuu ujao na pia kutumiwa kama vyanzo rahisi vya upataji taarifa kwa taasisi za kifedha ikiwamo benki.

Kama sehemu ya kuimarisha utendaji kazi, mamlaka hiyo ya vitambulisho vya taifa imeanzisha ushirikiano na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec),ambayo inakusudia kuvitumia vitambulisho hivyo katika uchaguzi mkuu ujao. Mkurugenzi Mkuu wa Nida, Dickson Maimu alisema ushirikiano huo itasaidia kuboresha kazi za utoaji vitambulisho na kwamba utakamilika kwa wakati. Hata hivyo alisema bado ofisi yake inakabiliwa na tatizo la vitendea kazi na kuiomba serikali kuongeza bajeti.

Hadi sasa mamlaka hiyo imekamilisha kukusanya taarifa kutoka kwa wakazi wa Dar es salaam na ilipanga kuendelea na zoezi hilo katika mikoa mingine.Ili kupata kitambulisho hicho wananchi wanapaswa kuwasilisha taarifa zao kupitia fomu maalumu zinazosambazwa na mamlaka hiyo na baadaye kuchukuliwa kwa alama za vidole, picha na saini za kielekroniki.

Vitambulisho hivyo vitaanza hivi karibuni kutolewa kwa watumishi wa umma, kwani taarifa zao pamoja na alama nyingine zilikwisha chukuliwa. Hatua hiyo inakuja katika wakati ambapo taifa liko kwenye mchakato wa uandikwaji wa katiba mpya, ambayo nayo pia imepangwa kupatikana kabla ya uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Kuhusu Zanzibar ambayo inatumia vitambulisho vya mkazi vilivyoanza kutumika tangu mwaka 2006, kumeelezwa kuwa, wananchi wa eneo hilo nao watajumuishwa kwenye zoezi hilo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate