EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 15, 2013

WIZI WA ATM WASHAMIRI..SHUHUDIA HAPA



JESHI
la Polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB
imewatia mbaroni watu watatu ambao wanadaiwa kuiba kiasi cha Sh700
milioni kwa nyakati tofauti.
 
Watuhumiwa
hao wamenaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki na polisi 
kwenye saa 6.00 usiku wa Februari 10, mwaka huu na mtuhumiwa mmoja 
alibambwa akichukua fedha katika ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza 
Mwanza.Baada ya kunaswa kwa mtuhumiwa huyo, alisaidia kuwaelekeza polisi walipo wenzake,
ambao walikutwa katika hoteli moja jijini Mwanza wakiwa wamejipumzisha.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mwanza,
Christopher Fuime alisema pia walikamata vifaa mbalimbali ambavyo
walikuwa wakitumia kwa ajili ya kufanyia uhalifu huo.

Vifaa walivyokamatwa navyo
Vifaa
vilivyokamatwa navyo ni kadi za bandia 194 za kuchukulia fedha katika
ATM za Benki ya NMB, ambapo kati yake kadi 95 zilikuwa na
namba 0225152975 zinazotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina
na picha ya mtu anayedaiwa kuwa ni mtumiaji mwenye jina la Molely L. P.
Kadi nyingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti
namba 5068000322 zikitumia jina moja la Mnuo Z. E na picha moja.

Mbali

na kadi hizo pia waliweza kunasa kadi 36 za Benki za DTB, ambazo kati 
yake kadi 18 zilikuwa na jina moja la Kelvin G. Gratias na namba 20497883,
kadi 12 zikitumia jina la John J. Paul zenye akaunti namba 2049783 huku
kadi sita zikitumia jina moja la Joseph Donald akaunti namba 2049783.


Kadi 

nyingine tatu zenye maandishi ya Download List na nyingine ikiwa ni kadi
ya Visa ya Benki ya KCB yenye namba 4183546040003827 zikitumia jina la 
Elikana Zacharia. Kadi nyingine zilikuwa ni tupu zisizo na maandishi 
wala nembo ya benki yoyote na nyingine zikiwa ni Soviet Royalty, kadi ya
raia ya Urusi ikiwa na namba 000724.

Pia walikutwa na kadi ya Benki ya Amerikani yenye namba 549012345678 zilizokuwa zikitumia jina la Richard Croswell.


Walikamatwa

pia wakiwa na vifaa mbalimbali vya kielektroniki ikiwamo kamera za siri
tatu za kienyeji ambazo zimetengenezwa kwa kufungwa betri za simu ya 
mkononi na pia walikamatwa na kifaa cha kutengenezea kadi bandia 
(Magnetic Card reader), mikebe mitatu ya rangi za kupulizia kamera za 
usalama katika ATM ili wasionekane wakati wa wizi wao, ‘printer’ pamoja 
na kifaa cha kuchomea vifaa vya umeme.

Wizi ulivyofanyika
Wahalifu
hufika katika mashine za kutolea fedha ambapo hatua ya kwanza ni kuzima
kamera za usalama za eneo husika kwa kuzipulizia rangi maalumu ili
kuzitia ukungu hivyo kuharibu mwonekano wake na kuruhusu wao kuingia
eneo hilo bila ya kuonekana na kufanya wizi wao.

Mara

baada ya kuziharibu kamera za usalama, walikuwa wakianza kwa kuweka 
kamera zao za siri ili kunasa namba za siri za kufungulia akaunti ambazo
huzisoma katika ‘kompyuta’ na kuzinakili katika daftari lao maalumu na 
kisha kuchukua kadi zao bandia na kuchukua fedha.


Wizi huo 

wa kuchukua fedha waliufanya nyakati za usiku saa sita hadi saa tisa 
usiku wakati ule wa kutegea kamera zao ulifanyika muda ambao huwa na 
wateja wengi hasa siku za mapumziko.
Chanzo Dj Sek Blog

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate