EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 29, 2013

Kesi ya Lwakatare yaanza Mahakama Kuu


Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare
MAOMBI yaliyowasilishwa na jopo la mawakili wanaomtetea Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare kupinga uamuzi wa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini kufuta na kumfungulia kesi nyingine mteja wao yatasikilizwa na Jaji Laurence Kaduri.

Jaji Kaduri wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam alipangwa kusikiliza maombi hayo jana. Majalada mawili ya kesi ya kujihusisha na ugaidi inayomkabili Lwakatare na Ludovick Joseph yalifikishwa mahakamani hapo Jumanne.

Majalada hayo yalipelekwa Mahakama Kuu kutokana na maombi yaliyowasilishwa na jopo la mawakili wa Lwakatare ambao wanaiomba mahakama hiyo kuyafanyia marejeo au kuchunguza ili kujiridhisha usahihi na uhalali wa mwenendo wa kesi katika jalada namba 37 na namba 6 ya mwaka huu.

Wanaomba mahakama hiyo kutengua hati ya DPP iliyofuta mashtaka dhidi ya washtakiwa hao kabla ya kuwafungulia mashtaka mengine kama hayo.

Jopo hilo linaomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutoa uamuzi wa maombi ya dhamana uliokuwa umepangwa kutolewa na Hakimu Mkazi Emilius Mchauru Machi 20 mwaka huu katika kesi namba 37 iliyofutwa.

“Tunaomba mahakama ifanye marejeo na kutengua mwenendo wa kesi mpya namba 6/2013 iliyofunguliwa baada ya kesi namba 37 kufutwa badala yake tunaomba jalada lililofutwa liendelee.
“Tunaomba mahakama iamue kwamba utaratibu wa DPP kufuta mashtaka ulikuwa kinyume cha sheria na haukuwa sahihi au itoe nafuu nyinginezo kadri inavyoona inafaa,”ilisema hati hiyo ya maombi.

Washtakiwa hao walifikishwa Mahakama ya Kisutu Machi 18 mwaka huu na Machi 20 mwaka huu waliachiwa kabla ya kukamatwa tena na kusomewa upya mashtaka ya kujihusisha na ugaidi.

Lwakatare na mwenzake waliachiwa mbele ya Hakimu Mchauru baada ya kukubaliana na maombi yaliyowasilishwa na upande wa Jamhuri ambao uliwasilisha hati kutoka kwa DPP ikionyesha a haikuwa na haja ya kuendelea na kesi hiyo.

“Mheshimiwa DPP amewasilisha nole prosequi chini ya kifungu cha sheria namba 98(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai akionyesha kwamba Jamhuri haina haja ya kuendelea na mashtaka hayo, tunaomba yafutwe,”alidai Wakili Mkuu wa Serikali, Prudence Rweyongeza.

Washitakiwa walisomewa mashtaka upya na Wakili Rweyongeza mbele ya Hakimu Mkazi Aloyce Katemana.

Alidai washitakiwa wanakabiliwa na mashtaka manne yakiwamo ya kula njama ya kumdhuru kwa sumu na kumteka Denis Msaki, Desemba 28 mwaka jana maeneo ya Stop Over Kimara.

“Shtaka la kwanza kwa ajili ya washitakiwa wote wawili ni kwamba wanadaiwa Desemba 28 maeneo ya King’ong’o Kimara Stop Over walikula njama ya kutenda kosa la kutoa sumu kwa nia ya kumdhuru Denis Msaki.

“Shtaka la pili kwa washitakiwa wote limefunguliwa chini ya kifungu cha sheria namba 24 (2) cha sheria ya kuzuia ugaidi namba 21 ya mwaka 2002. Washitakiwa wanadaiwa walikula njama ya kumteka Denis Msaki kinyume cha sheria namba 4(2) aya (C) (iii) cha sheria ya kuzuia ugaidi namba 21 ya mwaka 2002.

“Mheshimiwa shtaka la tatu linawakabili washitakiwa wote ambao pia wanadaiwa kinyume cha kifungu namba 5(a) cha sheria ya kuzuia ugaidi namba 21 ya mwaka 2002, kwa pamoja walifanya mkutano wa kufanya vitendo vya kigaidi, walipanga, walishiriki mkutano huo wenye lengo la kupanga kitendo cha ugaidi kwa kumteka nyara Denis Msaki.

“Shtaka la nne la kuhamasisha vitendo vya ugaidi, linamkabili mshitakiwa wa kwanza. Lwakatare, anadaiwa Desemba 28 mwaka jana, akiwa mmiliki wa nyumba aliruhusu mkutano kati yake na Ludovick kwa lengo la kuhamasisha vitendo vya ugaidi,” alidai Rweyongeza.

Hakimu Katemana hakuruhusu washtakiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kwa vile kesi hiyo inasikilizwa Mahakama Kuu. Aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 3 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Jopo la mawakili wanaomtetea Lwakatare ni Tundu Lissu, Peter Kibatala, Profesa Abdallah Safari, Nyaronyo Kicheere na Mabere Marando wakati mshitakiwa Ludovick hana wakili wa kumtetea.

CHANZO MTANZANIA 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate