EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 7, 2013

Mchakato Uchaguzi Mkuu TFF kurudiwa

Dar es Salaam. Serikali imelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuandaa upya mchakato wa uchaguzi wake mkuu uliolalamikiwa na wadau mbalimbali wa soka nchini, kiasi cha wengine kufungua kesi mahakamani kuupinga.
 
TFF imeshitakiwa mahakama za Mwanza na Tanga, baada ya baadhi waliokuwa wagombea wa nafasi mbalimba kuenguliwa kwenda kortini kupinga kufanyika uchaguzi huo mpaka kesi zao za msingi zitakaposilizwa.

Kabla ya mchakato huo, TFF pia imetakiwa kuitisha Mkutano Mkuu wa marekebisho ya katiba kabla ya Aprili 15, na baada ya hapo kuitisha pia Mkutano wa Uchaguzi kabla ya Mei 25 mwaka huu.
Uamuzi huo wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ulifikiwa jana katika kikao cha pamoja kati ya waziri mwenye dhamana ya kusimamia michezo, Fenella Mukangara na uongozi wa juu wa TFF.

Mwanzoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema wamewasilisha barua kwa Waziri Mukangara kutaka kukutana naye Alhamisi (leo) na kama ikishindikana wakutane baada ya March 13.

Osiah alisema katika kikao hicho, walipanga kukutana na waziri peke yake bila Naibu Waziri Amos Makala. Kwa siku za karibuni, Makala na Osiah wamejikuta kwenye mjadala mkali wa kurushiana maneno.

Hata hivyo, habari za ndani kutoka wizarani zinadai kuwa, Mkangalla amekataa ombi la awali TFF kukutana naye leo au Machi 23, na badala yake aliwataka viongozi wa TFF kukutana nao jana.

Kikao hicho mbali na waziri na naibu wake, pia alikuwamo Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi na Katibu wake Henry Lihaya, wakati TFF; Osiah, Mkurugenzi wa Ufundi, Sunday Kayuni na mwanasheria wa TFF aliyewakilisha Kamati ya Utendaji, Alex Mgongolwa.

"Mchakato wa uchaguzi unaanza upya, wameambiwa waitishe mkutano mkuu wa marekebisho ya katiba na kuingiza marekebisho yote kuanzia ya mwaka 2007 hadi 2010 kwa kuwa katiba iliyopo kwa Waziri ni ile ya mwaka 2006.

TFF wametakiwa ndani ya siku tano kuanzia leo (jana) mpaka Machi 11 (Jumatatu) kutoa tamko la kukubali kutekeleza agizo la Serikali," kilisema chanzo cha habari ndani ya wizara.

Akizungumzia suala hilo, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema hawezi kulizungumzia suala hilo kwa vile hajapewa barua ya maelekezo kutoka serikali, ingawa habari zilizopatikana baadaye barua hiyo imeshatumwa TFF.

Uchaguzi wa TFF uliingia dosari baada ya baadhi ya wagombea kuenguliwa kwa sababu mbalimbali, hiku wengine wakipeleka malalamiko Shirikisho la Soka Ulimwenguni (Fifa), ambalo linatarajia kutuma wawakilishi wake kuja kutatua mzozo huo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate