EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 6, 2013

Moto wateketeza bidhaa za mabilioni Dar es Salaam

Dar es Salaam. Moto mkubwa uliotokana na hitilafu ya umeme, umeteketeza bidhaa za mabilioni zilizokuwa zimehifadhiwa katika maghala ya Kampuni ya Sunda ya jijini Dar es Salaam.
 
Magari zaidi ya 20 ya vikosi vya zimamoto na uokoaji vya taasisi mbalimbali vilishindwa kuzima moto huo, ulioanza saa 4:45 asubuhi na kuendelea hadi jana mchana.

Akizungumza katika eneo la tukio, Kaimu Kamanda wa Zimamoto Kanda Maalumu, Bakari Mrisho, alisema walichelewa kupata taarifa za moto huo uliokuwa unateketeza maghala hayo ya kuhifadhi vifaa vya ujenzi na samani za ndani la ‘Ubungo Business Park’.
Mmoja wa wamiliki wa maghala hayo ambaye jina lale halikupatikana, alizimia baada ya kuona mali zake zikigeuka jivu.

Baadhi ya vifaa vilivyoelezwa kuwamo kwenye ghala hilo ni pamoja na marumaru, mashine za kufyatulia matofali, jasi, baiskeli, matoroli, mabomba ya plastiki na makasha mbalimbali yaliyokuwa na vocha za simu.


Vifaa vingine ni matairi ya baiskeli, vifaa vya maalumu vya ulinzi (CCTV, Smart Card ) na kontena zipatazo nne za vocha, (Pampasi, chupa za chai, vikombe vya chai vyote  vilitekelea kwa moto huo).

Baadhi ya kampuni zilizokumbwa na janga hilo ni Sandu (T) Limited, Kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel, Poly Machinery na Brick Machinery.
Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Sunda (T) Limited, Mashaka Zuberi alisema moto huo ulianza muda mfupi baada ya fundi umeme wa ghala hilo kufanya matengenezo ya kuongeza nguvu ya nishati hiyo.

Alisema fundi wa umeme jana (juzi) alikuwa anafanya matengenezo  ya kuongeza nguvu ya umeme kwani umeme uliokuwapo haukuwa na uwezo wa kuhudumia vifaa vilivyokuwapo.
Zuberi alisema leo (jana) saa 4.30 fundi huyo alifika kumalizia kazi hiyo ambapo aliwataka kuzima vifaa vyote vya umeme ili kuwezesha kuwasha baada ya kumaliza matengenezo.
Naye Kaimu Kamanda wa Zimamoto, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bakari Mrisho alisema kitendo cha baadhi ya watu kukaidi kuzingatia sheriza zimamoto ndio chanzo cha maafa ya aina hiyo.

Alisema walifanya ukaguzi na kuwataka kuweka kisima cha maji jambo ambalo hawakulitekeleza na kusababisha usumbufu wa kupata maji ya kuzimia moto huo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kutokana na moto huo kuwa mkubwa aliamua kuomba msaada wa magari ya zimamoto kutoka Bandari na Uwanja wa ndege.
Alisema chanzo cha moto huo hakijaweza kujulikana ambapo vitu mbalimbali vimeweza kuteketea kwa moto na hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate