Vita ya kukwepa kushuka daraja itaonekana tena leo kwa mechi sita za Ligi Kuu Bara kwenye viwanja tofauti.
Viwanja vitakavyotimka vumbi leo ni Mkwakwani(Tanga), Azam Complex (Dar es Salaam) na Sheikh Amri, Arusha
Endapo Mtibwa Sugar itafanikiwa kuvuna pointi
tatu, itafikisha pointi 31 na kusimama kwenye mstari mmoja na timu za
Simba na Coastal Union.
Hata hivyo, licha ya timu hizo kulingana kwa pointi, Simba iko juu ikikamata nafasi ya tatu kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa wakati Union inashika nafasi ya nne.
Nao Maafande wa JKT Oljoro baada ya kipigo cha
mabao 2-0 kutoka Coastal Union katika mechi iliyopita, watarudi Sheikh
Amri Abeid kujaribu kuponya jeraha kwa kumenyana na Prisons, wakati
African Lyon inayoburuta mkia itaburuzana na Ruvu Shooting katika
pambano la Uwanja wa Azam Complex.
Oljoro inayokamata nafasi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 22, inafahamu kwamba inahitaji ushindi tu kwenye mchezo huo ili kuepuka kushushwa chini ya Shooting iliyojiweka katika nafasi ya 10 baada ya kujikusanyia pointi 20.
Patashika ya nyingine itaendelea kesho kwa mchezo
mmoja tu, ambapo JKT Ruvu itaikaribisha Kagera Sugar katika pambano
ambalo matokeo yataamriwa kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Ruvu Shooting ya Pwani, imesema mchezo wake dhidi ya African Lyon kwenye Uwanja wa Azam Complex ni sehemu ya mazoezi yao kabla ya mchezo unaofuata dhidi ya Yanga Dar ss salaam .
Ofisa Habari wa timu hiyo, Masau Bwire alisema hawaidharau African Lyon ila kutokuwa na uwezo wa timu wana hakika asilimiaa 99 kuifunga timu hiyo.
Alisema mchezo huo utakuwa sehema ya mazoezi kwa
timu yao kujiandaana mchezo dhidi ya Yanga utakaochezwa Jumamosi, Uwanja
wa Taifa.
"Mchezo unaotuumiza kichwa kwa sasa ni ule dhidi
ya Yanga, kwani tumepania kufanya maajabu makubwa. Uwezo wa kuifunga
Yanga tunaona na tutafanya hivyo," alisema Bwire.
No comments:
Post a Comment