EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 6, 2013

Muhongo, Maswi watajwa kuiua TANESCO

WAKATI hali ya Shirika la Ugavi Tanzania (TANESCO) ni mbaya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Eliakimu Maswi, wanatajwa kuwa chanzo cha kulidhoofisha kiuchumi shirika hilo, Tanzania Daima Jumatano, limedokezwa.
Vigogo hao wanadaiwa kuingilia shughuli za kiutendaji za shirika hilo kisiasa na kwa maslahi ya watu binafsi.

Vyanzo vya habari toka serikalini na TANESCO vinasema Muhongo na Maswi wamekuwa wakiliendesha shirika hilo kama taasisi binafsi kinyume na taratibu, jambo ambalo limesababisha hasara ya mabilioni ya shilingi kwa shirika hilo tangu waingie madarakani.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya shirika hilo, zinasema kuwa kumekuwa na msigano wa kimaamuzi kati ya shirika hilo na Wizara ya Nishati na Madini.

Inaelezwa kuwa wakati Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo, Felchesmi Mramba, akianzisha mchakato wa kuomba maoni ya wadau kupandisha bei, Waziri Muhongo aliibuka kupinga mawazo ya kupandisha bei kwa maelezo kuwa shirika lina pesa nyingi na serikali inalipatia ruzuku.

Mramba katika mkutano wake na waandishi wa habari juzi, alisema kuwa kwa hali ilivyo sasa, hata kama TANESCO ikiamua kutolipa mishahara wala isifanye matengenezo ya mitambo, isinunue vifaa vya kuunganishia wateja, au isiingie gharama nyingine zozote, bado ingepata hasara ya karibu sh bilioni 90 kila mwezi, hivyo lazima bei ya nishati hiyo ipande ili liweze kujiendesha.

Taarifa zaidi zinasema, menejimenti ya TANESCO haina mamlaka ya kuendesha kitaalamu shughuli zake isipokuwa Maswi na Muhongo ambao hawana sifa za utaalamu wa kuendesha shirika, huingilia utendaji.

“Maswi na Muhongo wamekuwa wakiingilia utendaji wa kila siku wa TANESCO kwa sababu za kisiasa na sasa shirika hilo linaelekea kufilisika kabisa kwani kwa sasa linatumia sh bilioni 5.4 kwa siku huku likikusanya sh bilioni 2.3 tu, hali hiyo imetokana na maamuzi ya kisaiasa yanayofanywa na viongozi hao,” alisema mtoa habari wetu.
Habari kutoka ndani ya TANESCO, zinasema kuwa Maswi na Muhongo hawataki bei ya umeme ipande kwani wamekuwa wakisema serikali ndiyo yenye shirika, menejimenti ya 

TANESCO ni chombo cha kuelekezwa namna ya kuiendesha tu.
Hivi majuzi, baada ya TANESCO kutaka kupandisha bei ya umeme Katibu Mkuu Maswi aliingilia kati kumshauri Mkurugenzi wa Ewura Haruna Masebu kuwa asikubali uamuzi wa TANESCO kwani ungeiaibisha serikali na walipofanikiwa Maswi alinukuliwa katika andiko moja akimwandikia Masebu kumpongeza:
“Bwana Masebu, naomba kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa uungwana wako na kuamua kazi kwa kuilinda heshima ya serikali yetu. Heshima haina duka. Nakushukuru sana na naomba tuendelee kuisaidia serikali yetu pamoja na matatizo yaliyo mbele yetu. 

Kwa aina hii ya kushirikiana tutafika tu wala haina gogoro”
Wiki hii vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kuwa nchi iko hatarini kuingia gizani wakati wowote kutokana na hali ya uzalishaji umeme kuwa tete TANESCO.
Inaelezwa kuwa hali ya shirika kifedha ni mbaya licha ya serikali kukwepa kukiri uwepo kwa mgawo ikihofia kubanwa kwa ahadi yake kuwa mgawo ungelikuwa historia.
Julai 28 mwaka jana, wakati wa kuhitimisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, Waziri Muhongo na Naibu wake, George Simbachawene, walilihakikishia Bunge kuwa mgawo wa umeme ungelikuwa historia.

Lakini kwa takriban wiki nzima sasa, umeme umekuwa ukikatika hovyo kwa muda mrefu katika maeneo mengi nchini huku TANESCO ikitoa sababu za kawaida kuwa hali hiyo inatokana na matengenezo madogo kwenye miundombinu yake.
Habari zaidi za uchunguzi toka ndani ya TANESCO zinasema, hata mikopo ambayo shirika linapata sasa ni kwa ajili ya kulipa madeni tu wala sio kwa ajili ya kusaidia shirika hilo lisifilisike.

Ofisa habari wa TANESCO Badra Masudi alipoulizwa kuhusu hali hiyo, alijibu kwa kifupi kuwa mchanganuo wa pesa za TANESCO uko wazi.
Waziri Muhongo alipoulizwa kupitia simu yake ya mkononi kuhusu suala hilo, alijibu kwa kifupi tu kwamba yuko kwenye mkutano.
Baadaye alipoandikiwa ujumbe mfupi kwenye simu yake ya mkononi, hakuweza kujibu.
Ujumbe alioandikiwa na gazeti hili ulisomeka hivi: “Mheshimiwa Waziri, jana Kaimu Mkurugenzi wa TANESCO amesema shirika linaendeshwa kwa hasara na wewe ulisema wanakusanya pesa nyingi, sana, taarifa ipi ni sahihi? Pia tumepata taarifa kuwa unaiendesha TANESCO kisiasa; hufuati ushauri wa wataalamu nini maoni yako?”
Waziri alijibu tena kwa kifupi kwamba yuko kwenye mkutano. Jioni alipopigiwa simu, hakuweza kupokea.
Tanzania Daima pia ilimuandikia ujumbe wa simu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini: “Mheshimiwa Maswi, unatuhumiwa kuingilia utendaji wa kila siku wa TANESCO, je ni kweli? Au una taarifa zozote kuhusu hili?” Katibu Mkuu hakujibu ujumbe wala kupokea simu.
                          CHANZO CHA HABARI NI TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate