EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 6, 2013

Maandamano ya CHADEMA kumng’oa Kawambwa yaiva

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kiko katika hatua za mwisho za kuandaa utaratibu wa kufanya maandamano ya amani kwa ajili ya kumng’oa madarakani Waziri wa Elimu na Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, na Naibu wake, Philipo Mulugo.
 
CHADEMA imeeleza kuwa maandamano hayo ni ya amani na lengo lake hasa ni kuinusuru elimu ambayo iko kaburini.

Akizungumza kwa njia ya simu, jana, Ofisa Habari wa Chama hicho, Tumaini Makene, alisema kuwa maandalizi makubwa wameshayakamilisha na wanachomalizia ni taratibu za mwisho na kueleza kuwa yatafanyika katika kanda za chama hicho.
Akizitaja kanda hizo kuwa ni Kanda ya Ziwa katika mkoa wa Mwanza na yatahusisha mikoa yote iliyo karibu na mkoa huo, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini itakayohusisha mkoa wa Mbeya na mingine yote iliyo karibu.

Kanda nyingine ni ya Mashariki ambayo itahusisha jiji la Dar es salaam na mikoa iliyo jirani na mkoa huo na Kanda ya Kaskazini itakayohusisha mikoa ya Arusha, Manyara na mingine iliyo ndani ya kanda hiyo.
Makene alisema kuwa maandamano hayo yatakuwa ya kwanza na ya kihistoria ambayo serikali haijawahi kuyashuhudia kwani yatahusisha wananchi wote.

“Maandamano hayo yatahusisha wananchi wote, madereva wa bodaboda, daladala, bajaji, mama lishe, wanafunzi waliofeli na hata wale ambao hawajafeli, walimu na watu wote yaani kwa ufupi tusiite maandamano bali ni mgomo wa wananchi,” alisema Makene.

Alieleza kuwa kufeli mtihani kwa wanafunzi wa kidato cha nne kwa asilimia 94 si jambo dogo na ndiyo maana CHADEMA imepanga kuhakikisha elimu inapanda daraja kwa kuwaondoa watu wanaokwazisha jitihada za elimu.

“Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe aliwapa siku 14 wawe wamejiuzulu lakini maadamu wamekataa kufanya hivyo sasa ni mgomo wa wananchi ili kuhakikisha tunawaondoa madarakani,” alisema Makene.

Wameanza maandalizi ya maandamano hayo na watawatangazia wananchi siku husika.
“Baada ya kutoa maamuzi ya maana wao wanaanza kuunda tume ya ajabu na wengine kukaa tu maofisini, tuko ‘seriuous’ katika hili na lazima lifanyike,” alieleza Makene.
Nayo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imejitetea kuwa haipaswi kushutumiwa yenyewe peke yake katika hilo kwani suala la elimu linasimamiwa na wizara mbili.

Chanzo chetu cha ndani ambacho hakikutaka kutajwa jina kilieleza kuwa wadau, wanasiasa na wananchi wamekuwa wakiing’ang’ania wizara hiyo pekee ikiwemo kuwataka mawaziri wake kujiuzulu na kusahau kuwa suala la elimu pia linasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).
Chanzo hicho kilieleza kuwa mambo ya elimu yanahusisha wizara mbili ndio maana wakati mwingine inakuwa ngumu kutolewa uamuzi na kuishauri serikali kuamua moja katika suala la elimu ili libaki katika wizara moja ili ufumbuzi upatikane.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP, Charles Kenyela, alikiri kupokea barua ya taarifa ya maandamano ya amani kutoka CHADEMA.

“Nimepokea barua ya CHADEMA kuhusiana na maandamano juzi saa 9: 20 alasiri na tunajiandaa kutoa majibu na kuona namna ya kushughulikia suala lao, lazima kufanya mawasiliano na kuona namna ya kukabiliana na jambo hilo,” alisema Kenyela.

Awali Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, aliwapa siku 14 mawaziri hao kuachia nyadhifa zao jambo ambalo wamelikaidi na kubaki madarakani.
Alisema waziri huyo lazima ajiuzulu nafasi hiyo, kwani taifa ameliingiza pabaya na kuanza kuzalisha maelfu ya watoto wa maskini kumaliza elimu zao za msingi na sekondari wakiwa hawajui kusoma na kuandika.
Mbowe alisema hilo ni janga la kitaifa, hivyo lazima Kawambwa aondoke ndani ya wiki mbili, vinginevyo CHADEMA ingeliitisha maandamano makubwa nchi nzima kushinikiza kiongozi huyo ang’oke madarakani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate