EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 4, 2013

SULUHU HAIPATIKANI KWA KUTOKA NJE YA NDOA

NAAM tumekutana tena kwenye kona yetu ya Mapenzi na Uhusiano ili kujuzana machache kuhusiana na maisha yetu ya kila siku. Asilimia kubwa ya maisha yetu yametawaliwa na mapenzi. Nasema uongo?
Nitakuwa si muungwana kuanza mada mara moja bila kujuliana hali, binafsi sijambo, sijui mwenzangu u hali gani tangu tuachane wiki iliyopita!
 
Naamini kwa uwezo wa Mungu u mzima, kama ni mgonjwa basi Mungu akupe wepesi wa kupona haraka na kama kuna aliyetangulia mbele ya haki, apewe mapokezi mema ili apumzike kwa amani.
 
Leo kuna kitu kimoja kimenivuta kukaa mbele ya compyuta na kuyaandika haya, kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza.
Waswahili wana usemi wao kuwa, usipoziba ufa utajenga ukuta, huo usemi ni kweli kabisa, baada ya kushuhudia tukio moja ambalo nina imani lipo ndani ya nyumba zetu.
Nasema hivi baada ya juzi kumsikiliza mwanaume mmoja akilalamika kitendo cha mkewe kukataa kumpa haki yake ya ndoa, baada ya kukorofishana kwa jambo lisilo na maana yoyote.

Bwana yule nilimsikia akimlalamikia rafiki yake kuwa mkewe amekuwa na
tabia za kumnunia bila sababu, hata kama ni kitu cha kuzungumza na kuelewana yeye hununa hadi kufikia kupeana migongo kitandani, kila mtu kujifunika shuka lake.
Jamaa alimueleza rafiki yake kuwa kutokana na tabia za mkewe, ameamua kutafuta mtu wa nje ambaye amekuwa akimliwaza kila siku. Kwa kweli kauli ile ndiyo iliyonifanya niandike makala haya.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wanaume wengi sasa hivi wamejikuta wakitafuta suluhu ya matatizo ya ndoa zao kwa kutoka nje ya ndoa. Hii imefanya nyumba ndogo ziwe nyingi kila kukicha, kutokana na baadhi ya watu kushindwa kuelewa maadili ya ndoa yanasemaje pindi wanapokorofishana na wenza wao.
 
Hilo si kwa wanawake tu, hata baadhi ya wanaume huwanyima haki za ndoa wake zao pengine kutokana na kupata mwanamke wa nje. Kwa vile mkewe naye ana hamu zake na pa kuzitoa hana, kwa wenye mioyo dhaifu hutafuta mtu wa nje ili kukidhi haja.
Nataka kusema kuwa, kutoka nje ya ndoa si ufumbuzi wa tatizo, bali ni kuongeza ufa sehemu yenye mpasuko ambayo itaiangusha nyumba kabisa.
Siku zote suluhu ya ndoa haipatikani kwa mtu kwenda kutafuta mpenzi nje, bali kukaa chini na mwenzako ili kumaliza tofauti zilizojitokeza.
 
Kwa wanandoa wenye busara, linapotokea tatizo hukaa chini na kuelewana, wala hakuna atakayetaka kumkomoa mwenzake kwa kumnyima haki yake. Unamnyima haki yake wakati wewe ndiye mkewe au mumewe aliyekuchagua, unataka akaitafute wapi?
Unamlazimisha awe na nyumba ndogo au bwana wa pembeni. Thamani ya kitu ione wakati unayo, siku zote kibaya unacho lakini kikikutoka si chako tena, hapo ndipo utakapoijua thamani yake.
 
Mtu kumnyima haki ya ndoa mwenza wake si kutatua tatizo, bali ni kuongeza ukubwa wake na kutoka nje ya ndoa si kutatua tatizo, bali ni kuzidi kuibomoa nyumba.
Siku nyumba yenu itakapoporomoka muanguko wake ni mbaya, mwenzako akirudi na magonjwa ndani, nani wa kumlaumu? Huoni wewe ndiye chanzo? Siku zote kunapotokea tatizo tafuteni suluhu ya kutatua bila kumuathiri mtu yeyote. Oneaneni huruma, hakika hakuna atakayemuumiza mwenzake.

Kwa hayo machache tukutane wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate