EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 8, 2013

Vigogo wavuliwa madaraka TBS

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), imewavua madaraka wakurugenzi wawili.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Cuthbert Mhilu alisema jana kuwa waliovuliwa madaraka ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora, Dominic Mwakangale na aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio, Kezia Mbwambo.

 
Profesa Mhilu alisema hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya usaili kwa vigogo mbalimbali wa shirika hilo ulioanza juzi asubuhi hadi saa 3:00 usiku.
Katika taarifa hiyo, Profesa Mhilu ambaye hakutaka kuingia kwa ndani juu ya hatua hiyo, alisema viongozi hao watapangiwa kazi nyingine.

“Kwa kipindi kirefu, TBS imekuwa ikikabiliwa na matatizo mbalimbali yaliyochangia kudhoofisha utendaji wa watumishi na kulifanya shirika kukosa tija na ufanisi. Bodi imeonelea ikae mara moja kuchambua, kujadili na hatimaye kufikia uamuzi wenye lengo la kuweka mazingira bora na kuwezesha kuanza utatuzi wa matatizo ili shirika lifikie malengo yake.”

Baada ya hatua hiyo, bodi hiyo ilimteua Tumaini Mtitu kuwa Mkurugenzi mpya wa Udhibiti Ubora na Agnes Mneney kuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio.

Wengine walioteuliwa ni Emmanuel Ntelya atakayekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Shirika na Edna Ndumbaro kuwa Meneja Uandaaji Viwango vya Uhandisi.
Kadhalika, Matrida Kasanga ameteuliwa kuwa Meneja wa Hati na Tehama na Anitha Kaveva anakuwa Meneja Mipango na Utawala.
Alipoulizwa kama hatua hiyo inakwenda sanjari na sifa baada ya kufanyika kwa usaili Profesa Mhilu alisema: “Ninachowaambia ni hicho... hakuna tatizo tulilobaini kuhusu viongozi hawa, haya ni mabadiliko ya kawaida.”
Alipoulizwa kuhusu hatua hiyo, Mbwambo alijibu kwa kifupi: “Sifahamu, wasiliana na mwenyekiti wa bodi au  mkurugenzi mkuu ndiyo wenye nafasi ya kuzungumzia zaidi kuhusu hatua hiyo.”

Mwalangale hakupatikana na hata alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi iliita bila ya kupokewa.

Akizungumzia uteuzi huo, Profesa Mhilu alisema: “Hata hawa tuliowateua kushika nyadhifa hizo watambue kwamba tutawafuatilia kwa karibu tukiangalia utendaji wao, asiyefanya kazi kwa ufanisi atang’olewa.”

Alisema Bodi hiyo imetoa maagizo kwa Menejimenti ya TBS kuhakikisha kwamba inakomesha bidhaa feki, inafanya ukaguzi wa magari, pia kuhakikisha inaondoa urasimu wa upatikanaji wa leseni kwa wajasiriamali wadogo lakini kwa kuzingatia viwango vya bidhaa wanazotengeneza.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Joseph Masikitiko alisema kuwa amejipanga kushirikiana na menejimenti yake ikiwa ni pamoja na kukomesha makundi miongoni mwa wafanyakazi ili kuleta tija.

Tangu ilipozinduliwa, bodi hiyo imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kusafisha safu za utawala za shirika hilo baada ya kuanza kwa kumvua madaraka Kaimu Mkurugenzi Mkuu Leandiri Kinabo na kumteua Masikitiko kabla ya kuitisha usaili upya wa wakurugenzi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate