EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, April 7, 2013

Azam yatinga 16 Bora Afrika.



Azam FC ambao ni wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, huenda wakabaki kuwa wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika mashariki baada ya timu nyingi toka ukanda huu zikiwa zimeaga mashindano hayo na zile zilizosalia zinasubiri maajabu katika mechi zinazochezwa leo.
 
Timu ya Azam FC, jana ilifanikiwa kutinga raundi ya mwisho ya 16 bora baada ya kuing’oa Barrack Young Controllers II ya Liberia katika mbio za Kombe la Shirikisho.
Azam ambao ni wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa baada ya Simba na Jamhuri kuaga hatua ya awali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, wamevuka kikwazo kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-1. Kufuatia kuichapa BYC ll 2-1 kule Liberia na jana kwenda sare ya 0-0

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC inayonolewa na Kocha Stewart John Hall kuzidi kupeta licha ya kushiriki kwa mara ya kwanza michuano ya kimataifa tangu kuasisiwa kwao Juni 24, 2007.
 
Ushindi huo unaifanya Azam kukutana na timu kongwe na Mabingwa wa Afrika  mbara mbili mwaka 1985 na 2005 FAR Rabat inayomilikiwa na jeshi la Morocco ambapo mechi ya kwanza itachezwa wiki mbili zijazo kati ya Aprili 19 na 21 kabla ya kurudiana kati ya Mei 3 hadi 5.
Kwa mujibu wa muundo wa michuano hiyo, mshindi wa jumla kati ya Azam na FAR Rabat, ataingia kwenye hatua ya mtoano itakayojumuisha timu 16; zikiwemo nane zilizoaga raundi ya kwanza ya michuano ya Ligi ya Mabingwa.
 
Tofauti na Azam inayocheza mara ya kwanza michuano ya kimataifa, FAR Rabat iliyoanzishwa 1958, ni timu kongwe iliyowahi kutwaa ubingwa wa michuano hii mwaka 2005 na Ligi ya Mabingwa (wakati huo Klabu Bingwa Afrika) mwaka 1985.
Mwaka 2006, FAR Rabat inayoshiriki kwa mara ya tano Kombe la Shirikisho, ilifika fainali ya michuano hii kabla ya kung’oka raundi ya kwanza mwaka 2010.
Zaidi ya hapo, mwaka 1986 ilifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa na miaka miwili baadaye kuishia hatua ya nusu fainali.
FAR Rabat inamiliki uwanja wa Moulay Abdellah wenye uwezo wa kubeba watu 60,000.
 
Katika mechi ya jana, licha ya timu hizo kushambuliana kwa nguvu hivyo kuwepo kwa kosa kosa nyingi hasa katika lango la Barrack, dakika ya 39, Jockins Atudo alikosa bao baada ya mpira wake wa kisigino kugonga mwamba na kurejea uwanjani.
Mpira huo ulimkuta Kipre TcheTche ambaye alifumua shuti ambalo halikuweza kuzaa bao.
Dakika ya 45, Cammue Tummomie wa Barrack alilimwa kadi ya njano kwa mchezo mbaya.
Barrack walifanya kazi ya ziada kuokoa shuti ya Hamis Mcha iliyotokana na mpira wa adhabu ndogo dakika ya 52, lakini mpigaji akipatwa na kigugumizi cha mguu kabla ya Bocco kushindwa kuutumia vizuri mpira uliokuwa ukirudi.

Dakika ya 60, Tchetche alipiga shuti ambalo lilidakwa vibaya na kipa wa Barrack, Winston, na dakika sita baadae akakosa bao la wazi akiwa na kipa.
Azam: Mwadini Ally, Himid Mao, Wazir Salum, Jockins Atudo, David Mwantika, Kipre TcheTche, Salum Aboubakar, John Bocco, Humphrey Mieno na Brian Umony.
Barrack: Wiston Sayouh, Karleo Anderson, Joseph Broh, Cammue Tummomie, Prince Jetoh, Junior Barshall, Benjamin Gbamy, Abraham Andrews, Randy Dukuly, Maric Paye na Ezekiel Doe.
Habari hii ni kwa msaada wa gazeti la Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate