EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Mgogoro wa Loliondo: Kagasheki aponda kauli ya Nchemba.

Akizungumza kwa simu jana, Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (CCM), alisema Serikali imeamua kuchukua kilomita za mraba 1,500 kati ya kilomita za mraba 4,000 za eneo la Loliondo.
 
 Waziri Kagasheki 
Alisema ilifikia uamuzi huo ili kulifanya eneo hilo kuwa pori tengefu kwa ajili ya kusaidia wanyama kuzaliana na kupata malisho, hatua ambayo inapingwa na wakazi wa eneo hilo.
Waziri huyo alisema kuwa Nchemba, ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi, anapaswa kuelewa kuwa Serikali haikukurupuka kuchukua uamuzi.

Alisema matamshi ya kiongozi huyo wa CCM hayawezi kuwa msimamo wa chama kwani viongozi hao walitumwa kwenda Loliondo kukusanya maoni na kisha kuyawasilisha kwenye vikao vyake halali na siyo kutumia mikutano ya hadhara kutoa uamuzi.

“Hayo maneno kama kweli yamesemwa na Nchemba, basi hayo ni mawazo yake na wala siyo msimamo wa chama. Mimi najua chama chetu kina taratibu za kujadili mambo na siyo kuanza kuzungumza nje ya vikao,” alisema na kuongeza:

“Ninachoweza kusisitiza hapa ni kwamba huyu (Nchemba) hakutumwa na chama kutoa maagizo, yeye alipaswa kuwasilisha maelezo yake kwenye vikao… Kwa maana hiyo uamuzi wa Serikali bado uko palepale na haya yanayosemwa ni ya kwao.”

Hata hivyo, uamuzi wa Serikali unapingwa vikali na wakazi wa Loliondo kwa madai kuwa maeneo inayoyachukua yana vijiji vyenye hatimiliki.

Hivi karibuni, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana aliunda kamati kufuatilia suala hilo iliyowahusisha Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, Mbunge wa Longido, Lekule Laizer na Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo.

Mbunge Telele na kujiuzulu
Mbunge wa Ngorongoro (CCM), Saning’o Ole Telele amesisitiza kuwa uamuzi wake wa kujiuzulu pamoja na madiwani wake, upo palepale ikiwa Serikali itaendelea kung’ang’ania kuchukua ardhi hiyo bila ridhaa ya wananchi.

Akizungumza jana, Telele alisema kwa sasa wameamua kupeleka mgogoro huo katika chama tawala ili kichukue hatua akiamini kuwa haki ya wananchi wa Loliondo wanaopinga ardhi yao kuchukuliwa itapatikana.

Wananchi wa Tarafa ya Loliondo na Sale, wanapinga hatua ya Serikali kuchukua ardhi hiyo iliyopo katika vijiji vinane kwa madai kuwa ndiyo tegemeo lao la upatikanaji wa huduma muhimu za maji na ufugaji na kwamba iwapo litachukuliwa, maisha ya watu zaidi ya 65,000, ambao ni wafugaji yatakuwa shakani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate