EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 9, 2013

Ukatili wa kutisha "Baba anyonga watoto watatu, amtumbukiza mke kisimani"

*Baba anyonga watoto watatu, amtumbukiza mke kisimani
JESHI la Polisi mkoani Katavi, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Majimoto wilayani Mlele, Justine Albert (24), kwa kosa la kuwaua kikatili watoto wake watatu kwa kuwanyonga. Baada ya kuwanyonga watoto hao, Albert aliichukua miili ya marehemu wote na kwenda kuitumbukiza kwenye kisima cha maji kilichoko jirani na kijiji hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema mauaji hayo yalitokea saa 11:30 alfajiri usiku wa kuamkia jana.

Alisema kwa muda mrefu mtuhumiwa, alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na jirani yao na kwamba baadhi ya watoto wanadaiwa kuzaliwa nje ya ndoa yao.

Aliwataja watoto walionyongwa na baba yao, kuwa ni Frank Justine (6), Elizabeth Justine (4) na Maria Justine mwenye umri wa miezi minne.

Inadaiwa baada ya kuwanyonga watoto wake kwa zamu, alichukua miili ya Frank na Eliza akaitumbukiza kwenye kisima.

Kamanda Kidavashari, alisema Albert pia alimchukua mke wale, Jacqueline Luvika (21) na kumtumbukiza ndani ya kisima hicho ambacho kinamilikiwa na Kawaida Jonas.
“Baada ya kuona amewaua wale watoto, aliamua kumpiga mke wake kisha kumtumbukiza ndani ya kisima kile akiwa hai, lakini majirani walifika na kumtoa na hali yake ni mbaya,” alisema Kamanda Kidavashari.

Akisimulia mkasa huo, Kamanda huyo alisema kulipopambazuka baadhi ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wakielekea kwenye shughuli zao, waliuona mwili wa mtoto ukiwa umetelekezwa kando ya njia na kumtambua kuwa ni Maria mwenye umri wa miezi mine, ambaye ni kitindamimba wa mtuhumiwa.

Inadaiwa ndipo walipoamua kufika nyumbani kwa mtuhumiwa na kumpatia taarifa hiyo na kuhoji alipo mama yake bila kupata majibu ya msingi.

Lakini mtuhumiwa aliwaeleza kuwa alikuwa ametoroka kusikofahamika na watoto wote.

Kutokana na maelezo hayo, wananchi hao walimtilia mashaka mtuhumiwa na kuamua kutoa taarifa kituo cha Polisi.

Baada ya polisi kwenda eneo la tukio, walikuta mwili wa Maria na kubaini ulikuwa na miburuzo ardhini na michubuko kitendo kilichowafanya wafuatilie mpaka kisimani.

Walipofika kisimani, waliamua kufungua mfuniko wa kisima hicho ndipo walikuta miili mitatu ikielea kwenye maji.

Kutokana na hali hiyo, polisi kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kuopoa miili yote, huku mama ambaye alikuwa amekunywa maji mengi akiwa taabani na kupoteza fahamu.

Kamanda Kidavashari, alisema baada ya kumuopoa mama huyo alikimbizwa kituo cha afya cha kijijini Mamba, ambako amelazwa kwa matibabu na mpaka jana mchana alikuwa hajajitambua.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate