EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, May 20, 2013

POLISI AMCHARANGA MAPANGA MWANAYE KISA MAPENZI.

Na Mwandishi Wetu, Shinyanga
KATI ya stori za mwaka zinazosikitisha, hii ni mojawapo! Polisi mstaafu, mkazi wa Kitongoji cha Sango, Kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoani hapa, Samson Bwire (54), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumcharanga mapanga binti yake, Devotha Gerald (4), kisa kikidaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Wataalamu wakipigania uhai wa mtoto Devotha Gerald, baada ya kukatwa mapanga na baba yake.
Tukio hilo lilitokea Mei 16, mwaka huu, majira ya jioni nyumbani kwa Bwire alipokuwa akigombana na mke wake, Happiness Elias (28).
Kwa mujibu wa mashuhuda, baba Devotha anadaiwa kufanya tukio hilo huku akiwa amelewa tilalila.
Habari zilidai kuwa, mwanaume huyo alikuwa kwenye ugomvi wa kimapenzi na mkewe ambapo katika purukushani akimtuhumu mama Devotha kumsaliti, mkewe huyo alifanikiwa kuchoropoka.
Mtuhumiwa huyu hapa.
Ilidaiwa kuwa baada ya mama Devotha kuchoropoka ndipo baba huyo akamgeuzia kibao Devotha na kumalizia hasira zake kwa kuanza kumkatakata kwa panga bila huruma.
Kwa mujibu wa majirani, kelele zilisikika kutoka kwenye familia hiyo na kwamba walipokwenda walimkuta baba Devotha akichoma nguo za mkewe na alipowaona, aliingia ndani na kuanza kumkata mapanga mtoto huyo huku akiwa amefunga mlango.
Wananchi  wakiwa eneo la Hospitali ya Wilaya ya Kahama walipolazwa Devotha na baba yake.
Ilifafanuliwa kwamba baada ya kusikia kelele za mtoto, majirani walianza kuvunja mlango huku wakiomba msaada kutoka kwa polisi na baada ya polisi kufika walifanikiwa kumnusuru mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya.
 
Kufuatia hali mbaya ya mtoto aliyekuwa amelowa damu kichwani, majirani walishindwa kuzuia hasira zao na ndipo walipoanza kumpiga Bwire ambaye ni askari polisi mstaafu wa cheo cha koplo.
Katika hali kama hiyo, ilibidi polisi wafanye kazi ya ziada kumnusuru baba Devotha na kumpakia kwenye gari kwenda kituoni.
 
Hata hivyo, wakati gari la polisi likiwa katika mwendo wa kasi eneo la Soko la Mkulima, baba Devotha aliruka kutoka kwenye gari na kuangukia lami, kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa sehemu za usoni.
Mtoto Devotha na baba yake, wote walikimbizwa na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama kwa matibabu huku Bwire akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ikiwa ni pamoja na kufungwa pingu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate