EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 8, 2013

Akina mama kujifungua bure Kenya. Inawezekana?

Serikali nchini Kenya imeanza kutekeleza ahadi yake ya kufutilia mbali malipo yanayotozwa akina mama wajawazito kujifungua katika hospitali za umma kote nchini.

Rais Uhuru Kenyatta aliahidi katika manifesto yake ikiwa atachaguliwa kama rais kufutilia mbali ada inayotozwa na hospitali za umma kwa akina mama kujifungua katika siku miamoja za kwanza za uongozi wake.
Kufikia hapo jana , moja ya hospitali kubwa za huduma kwa wanawake, ya Pumwani, iliwaruhusu wanawake zaidi ya tisini waliojifungua kurejea nyumbani bila kutozwa chochote.
Mpango huu unatekelezwa kote nchini, katika hospitali, zahanati na hata katika kliniki za umma.

Gavana wa jimbo la Nairobi, Evans Kidero alisisitiza kuwa ada inayotozwa wanawake tangu wanapolazwa hospitalini hadi wanapojifungua, itagharamiwa katika mpango huu wa serikali kwa kiwango cha shilingi bilioni 8.
Hospitali ya Pumwani inasemekana kuhitaji zaidi ya shilingi bilioni mbili kukarabatiwa

"Akina mama wote waliojifungua katika hospitali ya Pumwani wanaruhusiwa kwenda nyumbani bila malipo kuambatana na agizo la rais Kenyatta. Pumwani ni moja ya hospitali kubwa ya wanawake kusini mwa jangwa la Sahara,'' alisema gavana Evans kidero.

Rais Kenyatta alifutilia mbali ada wanayotozwa wanawake wanapojifungua katika taasisi za serikali katika kile alichotaka kuwa sehemu ya juhudi za serikali ya Jubilee kutekeleza malengo yake

Kwa upande wake waziri wa afya James Macharia, alisisitiza kuwa hakuna hospitali yoyote ya umma inapaswa kutoza ada yoyote.
"Yeyote aliyelipishwa kwa huduma walizopata, anapaswa kurejeshewa pesa zake. ''

''Ruwaza ya Jubilee, ilithibitisha kuwa tunaweza kutoa huduma za bure kwa akina mama na huu ndi mwanzo wa safari yetu (mpango huu).'' alisema waziri Macharia
Aidha alisisitiza kuwa malipo kwa huduma yoyote yataweza kugharamiwa na serikali.
Katika vituo vya afya vya umma mashinani, mwanamke huhitajika kulipa shilingi 2,500 au dola 31 ,katika baadhi ya vituo kote nchini, baadhi hutozwa shilingi 5,000 au dola sitini na mbili wakati katika hospitali kuu ya serikali, akina mama hutozwa dola zaidi ya miambili.
Wanawake wanatabasamu kwa kuweza kujifungua bila malipo
Gharama hizo zote zitakuwa jukumu la aserikali sasa haijalishi matatizo watakayokabiliwa nayo wanawake, yote yatagharamiwa.

Bwana Macharia, alisema kuwa katika siku miamoja zijazo wizara ya afya itatumia shilingi bilioni moja kutoa huduma za afya ya uzazi kwa akina mama na kisha kuanzia mwaka ujao, inatumia bilioni nane kila mwaka kuwezesha akina mama kupokea huduma hizo.
Tayari mpango huo umeshajadiliwa na hazina ya serikali na wizara imepewa kipaombele katika kuhakikisha kuwa inapokea pesa hizo.
Amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ili kupunguza idadi ya vifo vya akina mama na watoto wachanga.

Hata hivyo licha ya kuwa hii ni habari njema kwa wanawake, bado kuna changamyo si haba. Tayari siku moja tu tangu kuanza kwa mpango huo, mwanamke mmoje mkoani Pwani amepoteza mwanawe kwa kile wanachokiita kupuuzwa na wauguzi wakati mama huyo alikaribia kujifungua.
Mtoto wa mama huyo kwa jina Margaret Munavu, alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa na sasa wanalaumu wauguzi kwa kutokuwa maakini. Mama huyo alijifungulia katika hospitali kuu ya serikali katika jimbo la Mombasa.
Changamoto zengine zinazokabili sekta ya afya nchini Kenya ni pamoja na ukosefu wa vifaa , akina mama kulazimika kuja hospitalini na nyembe,pamba, na vifaa vingione vinavyohitajika wanapojifungua.

Baadhi ya hospitali na vituo vingine ziko katika hali mbaya kiasi cha kuhitaji ukarabati. Katika hospitali ya Pumwani , mjini Nairobi, ambayo ndiyo kubwa zaidi katika kuwahudumia akina mama wajawaziti Kusini mwa jangwa la Sahara, huwashughulikia takriban wanawake miamoja au zaidi kwa kujifungua pekee.
Wakosoaji wanasema ni bora kwa serikali mwanzo kukarabati nyingi ya hospitali za umma kabla ya kuanza kutoa huduma ya bure ya uzazi kwa wanawake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate