EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, June 9, 2013

Biashara haramu ya watu yaathiri laki 6 Afrika

WAKATI mataifa mbalimbali duniani yakipambana kukomesha biashara haramu ya kuuza watu, imeelezwa kuwa ni ya pili kwa ukubwa duniani kufanyika baada ya dawa za kulevya, huku zaidi ya watu laki 6 kutoka Afrika wakiwa waathirika wakubwa.

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Madawa ya Kulevya na Uhalifu (UNODC), zinazoeleza kuwa wafanyabiashara wamekuwa wakijipatia kiasi cha dola bilioni 31 kwa mwaka na kwamba hadi kufika mwaka 2011 watu milioni 2.5 duniani kote walishauzwa.
Katika mahojiano maalum na Tanzania Daima, Msemaji wa Shirika la Uhamiaji Duniani (IOM), Jumbe Omar Jumbe, alisema katika biashara hiyo nchi ya Ukraine na zile za Uarabuni ndizo zinazoongoza.

Aliongeza kuwa watu wanaofanya biashara hiyo kutoka nchi hizo wamekuwa wakiwakusanya watu na kuwauza katika maeneo mbalimbali.
Katika Afrika, Jumbe alisema nchi zinazojishughulisha zaidi na biashara hiyo ni Morocco, Sudan na Uganda huku akibainisha kuwa tatizo hilo limekuwa gumu kugundulika Tanzania kwa kile alichoeleza kuwa matajiri wa biashara hiyo wanakaa nchi za nje na kuwatumia mawakala kufanikisha shughuli zao.

Jumbe alitaja sababu za watu kukubali kuuzwa kuwa ni pamoja na tamaa ya kutafuta maisha bora na kubainisha kuwa wengi wanaofikishwa katika maeneo waliyouzwa wanakuta mambo ndivyo sivyo na kutaja kundi linaloathirika kwa kiasi kikubwa kuwa ni la wanawake.

Alisema imekuwa ngumu kukomesha biashara hiyo kutokana na wafanyabiashara hiyo kuwa na fedha nyingi wanazotumia kuwahonga watumishi wasio waaminifu kufanikisha mbinu zao.
Hivi karibuni Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi Duniani (UNHCR) kwa kushirikiana na IOM, liliandaa semina ya siku mbili ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu masuala ya wakimbizi na wahamiaji, iliyofanyika jijini Dar es Salaam huku biashara ya binadamu ikiwa moja ya mada zilizojadiliwa.
Ofisa Mwandamizi wa UNHCR, Edmond Kamina, alisema lengo la semina hiyo ni kujenga mahusiano ya karibu na mashirika hayo na kuwajengea uwezo waandishi kuandika kuhusu masuala hayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate