EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 11, 2013

Maisha feki ya mastaa wa Bongo.

TASNIA ya muziki wa kizazi kipya Bongo kwa sasa imeshika kasi, wasanii kwa kiasi kikubwa wameweza kuwekeza na hata majina yao yamekuwa juu kiasi cha kujijengea imani kubwa mbele ya jamii.
 
Imani hii kubwa na ushabiki uliokithiri, imezua jambo jingine kubwa ambalo limekuwa tatizo la kimaendeleo. Tatizo hilo ni wasanii kujikuta wakiendeshwa na umaarufu wa majina yao katika namna ya wanavyoishi.

Imebainika kwa kuwa majina yao ni makubwa kuliko uwezo wao wa kuishi. Jambo hili limewafanya wasanii hao waishi maisha feki mbele ya jamii yao.
Kwa kuishi maisha hayo, wamejikuta wakitumia gharama kubwa katika kuishi maisha ambayo si ya daraja lao.

Mavazi
Ukianzia na mavazi, kwa kuwa tu anajulikana yeye ni yule msanii aliyeimba wimbo fulani maarufu, basi hata kama hana mavazi ya gharama atajitahidi hata kwenda kuazima, ili mradi mashabiki wake wakimwona wamkute nadhifu.
Awali tabia hiyo ilidhaniwa ni ya wasanii wa dansi pekee hasa Wakongomani, lakini sasa ni fasheni kwenye Bongofleva.
 https://encrypted-tbn0.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSwNgHCXaC-Q0w0AcPCjoEMTwIQOlTTNDM7Q8wrE35CYcS3zxz7GevTyk6e
Inakubalika na ni dhahiri unadhifu kwa watu wenye mvuto kwa jamii ni jambo lililo wazi, lakini unadhifu unahusiana vipi na gharama?
Wengi wanapotelea hapa, wanafikiri unadhifu ni kuvaa vitu vyenye gharama kumbe uchaguzi wa vitu vya kawaida na mpangilio vinaweza kukufanya kuwa nadhifu kuliko vitu ghali.

Angalia mavazi ya Michael Jackson, yalikuwa ya gharama sana lakini si kweli kwamba mavazi yale ndiyo yalikuwa yakisababisha aonekane nadhifu kuliko wasanii wote duniani, alikuwa tu ni Mfalme wa Pop.
Lakini Bongo ukiachilia mbali kuazimana, kuvaliana na kuambukizana magonjwa, kuna kundi kubwa la wasanii ambao hupenda kujihusisha na maduka ya nguo ili mradi tu wapate kupendeza.

Usafiri
Ukishakuwa staa, tayari kuitwaitwa barabarani, kufuatwa na watoto ukiwa katika matembezi yako, ama kuombwa kupiga picha na mashabiki wako na mambo mengineyo kama hayo ni jambo la kawaida.
Wasanii wetu wanahisi hii ni ghasia na kuwakimbia mashabiki wao. Huukimbia kabisa usafiri wa umma, yaani daladala au wakati wanaenda mikoani huona bora hata wakodi magari badala ya kupanda basi.
Kuna asilimia kubwa ya wasanii tunaowaona wanaendesha magari kana kwamba wanayamiliki, kumbe si yao. Wengi huyakodi ili wakionana na mashabiki wao angalau waonekane wao ni wa matawi ya juu.
Jina linaendelea kuwa kubwa huku mhusika akiteseka kwa kuingia madeni makubwa.
Amini usiamini humu ndimo asilimia kubwa ya kipato cha msanii wa kizazi kipya kinapopotea. Magari hukodishwa kuanzia Dola 25 mpaka Dola 40 kwa siku kulingana na aina ya gari.

Makazi
Hapa ndipo ambapo hawajali kabisa, wengi wao huishi kwa kutegemea wazazi na wengine huishi kwenye nyumba za kupanga kwa kuchangia au kukaa tu kwa mtu huku wakiamini ipo siku mambo yatakuwa sawa wajenge.
Nyumba wanazoishi wengi wao ukiangalia na mavazi wanayovaa na magari wanayoendesha ni vitu tofauti. Wengi huweka kipaumbele mwonekano wa nje kuliko hata wanapoweka ubavu.

Ni wasanii wachache wanaomudu maisha yao kutokana na kipato kilivyo.
Ukiangalia mavazi, usafiri na huku anataka kuonekana kila sehemu ya starehe, sehemu ya pato hupotea huko na mwisho wa siku hubakia kuwa na umaarufu wa maneno na sifa za mdomoni .

Biashara?
Wengi zimewashinda kutokana na ukweli kwamba hawana uzoefu na tija katika biashara. Huanzisha miradi kwa kasi kwa kushirikiana na watu, lakini huwa hawachukui muda kwani hujikuta wakitolewa nje kutokana na matumizi yao makubwa kuliko kipato.

Sifa kubwa ya mfanyabiashara ambaye anasimama kama mchumi ni kuzijua hesabu zake kwa umakini jambo ambalo wasanii wetu wa kizazi kipya hawana.
Ukiachana na hilo, wengi wamekuwa wakitumiwa tu majina yao katika maduka lakini ukija kwenye ukweli, maduka huwa si yao, majina hayo hutumika kunufaisha biashara za watu na mwisho wa siku ukweli huja kubainika.
Upo mfano wa msanii mmoja aliyewahi kuwa na Baa maeneo ya Sinza, lakini ukweli ukaja kugundulika kwamba baa ilikuwa ni ya mwanamke aliyekuwa na uhusiano naye, pale walipoachana ndiyo siri ikavuja.
Kwa kifupi wasanii wengi wa Bongo hawajitambui, unataka kujua sababu?
Inaendelea Jumamosi......

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate