EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, June 10, 2013

Siyo wakati wa Taifa Stars kukata tamaa

Juzi timu yetu ya taifa ya Soka ‘Taifa Stars’ ilifungwa na Morocco mabao 2-1 katika mechi muhimu ya kuwania tiketi ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia 2014 zitakazofanyika huko Brazil.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Marrackech huko Morroco, vijana wa Taifa Stars walijitahidi kupambana katika mechi kutafuta ushindi, lakini bahati haikuwa yao. 


Kwa matokeo hayo, Taifa Stars imeendelea kushika nafasi ya pili katika Kundi C ikiwa nyuma ya Ivory Coast yenye pointi 10 huku Morroco ikishika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tano na Gambia ipo nafasi ya mwisho ikiwa na pointi moja. Hivi sasa Taifa Stars imebakisha mechi mbili katika hatua hii ya makundi ambazo ni dhidi ya Ivory Coast itakayofanyika jijini Dar es Salaam na dhidi ya Gambia itakayofanyika huko Banjul.

Mechi kati ya Taifa Stars dhidi ya Ivory Coast itachezwa Juni 16 ambayo ni Jumapili hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambapo kama Taifa Stars ikishinda mechi hii itakuwa imefikisha pointi tisa na kuikaribia Ivory Coast ambayo mechi yake ya mwisho itacheza na Morooco huko Abidjan.

Sisi tunaamini huu wa siyo wakati sahihi kwa vijana wa Taifa Stars na mashabiki wa soka nchini kukata tamaa kwani matumaini ya kufanya vizuri katika hatua hii ya makundi na kutinga raundi ya tatu ambayo ni hatua ya mtoano bado yapo.
Kama watu wanakumbuka vizuri, watakumbuka kuwa Stars ilianza kushiriki mashindano haya tangu raundi ya kwanza, ambapo mechi ya kwanza Stars ilicheza ugenini 2011 dhidi ya Chad na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, lakini timu hizo ziliporudiana jijini Dar es Salaam, Stars ilichapwa 1-0 hata hivyo ilisonga mbele na kuingia hatua ya makundi ambayo ni raundi ya pili.

Katika raundi ya pili tayari Taifa Stars imecheza mechi nne, ambapo mechi ya kwanza ilichapwa 2-0 na Ivory Coast ugenini, mechi ya pili Taifa Stars iliichapa Gambia 2-1 nyumbani, mechi ya tatu Taifa Stars iliichapa Morocco 3-1 nyumbani na mechi ya nne Taifa Stars imefungwa 2-1 na Morocco ugenini.

Ni wazi Taifa Stars baada ya juzi kukubali kufungwa na Morocco imejiweka katika wakati mgumu wa kuingia 10 bora au raundi ya tatu, kwani yapo makundi kumi na kila kundi linatakiwa kutoa mshindi wa kwanza kuingia hatua hiyo ya raundi ya tatu ambayo ni hatua ya mtoano, ambapo katika kundi la Taifa Stars timu ya Ivory Coast hivi sasa ina nafasi kubwa kwani ina pointi 10 na imebakisha mechi dhidi ya Taifa Stars na mechi dhidi ya Morocco, ambapo itakuwa nyumbani.

Lakini, hata hivyo siku zote mpira unadunda, na ndiyo maana tunasema huu siyo wakati wa wachezaji na mashabiki wa soka Tanzania kukata tamaa kwani lolote linaweza kutokea. 
Sisi tunaamini kuwa katika mechi ya Jumapili dhidi ya Ivory Coast, wanachotakiwa kufanya wachezaji wa Stars ni kujiamini, kujituma kwa kucheza bila hofu wakitambua kuwa wanakumbana na timu yenye wachezaji wengi wanaocheza soka ya kulipwa Ulaya, lakini inafungika na ndiyo maana hadi sasa haijajihakikishia kuingia raundi ya tatu.
Tunaamini wachezaji wa Taifa Stars watakuwa na uzalendo, umoja na lengo moja, kwa sababu siku zote lengo moja huleta ushindi, na ushindi utaiweka Taifa Stars katika nafasi nzuri katika kundi lake.
Tunatarajia wachezaji wa Taifa Stars wataendelea kutekeleza wajibu wao wa kuliwakilisha taifa na kuwafurahisha Watanzania hasa katika mechi ya Jumapili dhidi ya Ivory Coast, pia tunatarajia mashabiki wengi wa soka watajitokeza Jumapili kuishangilia Taifa Stars.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate