EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 30, 2013

BILIONEA ALIYEMWAGIWA TINDIKALI DAR… HALI TETE.

HALI ni tete kuhusiana na tukio la bilionea Said Mohamed Saad kumwagiwa tindikali, athari ni kubwa. Jinsi alivyoharibika inatia simanzi lakini kumpata mhusika wa unyama huo ni kitendawili kinacholitega Jeshi la Polisi Tanzania.
Rais Kikwete akimjulia hali mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, Said Mohamed Saad.
Said ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, yenye maduka mengi makubwa ya vitu vya nyumbani ndani ya Dar es Salaam na mikoa kadhaa ya Tanzania, anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini lakini mmoja wa watu waliomshuhudia, amefafanua jinsi hali ilivyo mbaya.
 
“Ameungua sana, tunatarajia kati ya kesho au keshokutwa (wikiendi iliyopita) atafanyiwa oparesheni ya jicho. Jamani tindikali ni mbaya sana, usimmwagie mwenzako. Ndugu yetu ameharibika sana,” kilisema chanzo chetu kwa ombi la kutotajwa jina gazetini, kikaongeza:
“Kila anayemjua vizuri, anapomwona anamwaga machozi. Picha za jinsi alivyoathirika baada ya kumwagiwa tindikali zimevuja mpaka kwa familia, ni kilio kwa ndugu. Wanawake wanalia zaidi.”

JK ATINGA HOSPITALI
Wiki iliyopita, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC).
Mkutano huo ni wa Pande Tatu za SADC (Troika of SADC) na akiwa huko, alipata fursa ya kwenda kumjulia hali katika hospitali aliyolazwa ambayo haijajulikana jina.
Chazo chetu kilisema: “Rais Kikwete alisikitika sana. Wakati anatoka wodini alisonya. Alionesha jinsi alivyosikitishwa na unyama aliotendewa Said.”

Bilionea Said Mohamed Saad akiwa hospitali.

WAPELELEZI WAMWAGWA KARIAKOO
 
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Dar es Salaam, ACP Camillius Wambura aliwaambia waandishi wetu wiki iliyopita kwamba jeshi linaendelea kufanya kazi yake kuhakikisha linampata mhusika wa unyama huo.
 
“Mpaka sasa tuseme ukweli hatujampata mtuhumiwa au kitu kinachoonesha mtuhumiwa alivyo lakini kazi inafanyika. Tupo makini kwelikweli na tumeweka mkazo wa hali ya juu,” alisema Wambura.
 
Kwa upande mwingine, chanzo chetu ndani ya jeshi la polisi kimehabarisha kuwa idadi kubwa ya wapelelezi wamemwagwa Kariakoo, Dar es Salaam.
 
“Kuna mambo yanazungumzwa kuhusiana na tukio la Said kumwagiwa tindikali, yanafanyiwa kazi. Kutokana na ukweli kwamba msingi wa biashara za Said ni Kariakoo, vilevile kwa sababu inatambulika kuwa eneo hilo lina wafanyabiashara wengi, imebidi kulimulika kwa undani kabisa.
 
“Inawezekana ni chuki za kibiashara. Yaani aliyemtendea, ama alimshambulia au alifanya kulipa kisasi kutokana na vita ya kimaslahi. Hili suala tunaliangalia kwa upana sana ndiyo maana wapelelezi wamemwagwa Kariakoo.
 
“Wanachunguza kila taarifa. Kila kinachozungumzwa kinafanyiwa kazi na wale ambao itaonekana upo ulazima wa kuwakamata, watakamatwa ili kuisaidia polisi kufanikisha kumpata mtu ambaye alihusika na kummwagia tindikali yule bwana wa Home Shopping Centre,” kilisema chanzo chetu.

DAR YOTE INAPELELEZWA
Kwa mujibu wa chanzo chetu, pamoja na upelelezi kuwekewa mkazo Kariakoo lakini kazi ya kumsaka mhalifu aliyemfanyia unyama Said, inafanyika ndani ya jiji lote la Dar es Salaam pamoja na mikoa ambayo taarifa zitaelekeza.
 
“Kipindi chote ambacho upelelezi unafanyika, pengine zitaibuka taarifa zinazoelekeza mikoani ili kumpata mtuhumiwa, polisi watafika kote. Ukweli ni kwamba siyo tukio hili tu, jeshi la polisi limekuwa imara kufanyia kazi kila aina ya uhalifu.
 
“Pamoja na ugumu wa kumpata mtu hasa aliyemmwagia tindikali kutokana na mazingira yalivyokuwa, hilo halifanyi tukae kimya na tuache hili suala lipite. Maisha ya watu yanathaminiwa sana, unyama wa kuwadhuru wengine kwa vitu hatari kama tindikali, haukubaliki ndani ya polisi,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
 
“Maswali kuhusu aliyemmwagia tindikali hiyo, nani mhusika pamoja na sababu ya huyo aliyemmwagia tindikali, pengine ni mambo ambayo yanahitaji muda zaidi. Polisi wafanye kazi, mafanikio yake, yatatanzua utata wote.”

SHEMEJI MTU ATAJWA
Huku upelelezi ukiendelea, zipo taarifa kwamba mtu mmoja anayedaiwa kuwa shemeji wa Said, anatakiwa kuhojiwa kwani alishawahi kuripotiwa kuwa na uhusiano mbaya.
Ilibainishwa kwamba kumpata mhusika wa unyama huo, ni lazima kila aliyewahi kuripotiwa kuwa na tofauti za kijamii au kibiashara na Said, akamatwe na ahojiwe ili kuisaidia polisi.
 
“Yule shemeji yake ilishaelezwa waligombana sana. Mitandao ya kijamii ikaandika sana. Polisi hawatakiwi kudharau taarifa. Wamfuatilie huyo shemeji mtu, ahojiwe kwa makini,” alisema mfanyabiashara mmoja wa Kariakoo (jina tunalo), akaongeza:
 
“Siyo huyo shemeji yake peke yake, hata watu wengine wenye historia ya kugombana na Said, nao pia wamulikwe. Hili jambo ni nyeti, tena zito sana. Kumtenda binadamu ukatili wa kiwango hicho ni suala ambalo haliwezi kuvumilika.”

BODABODA TISHIO KWA NCHI
Said, alimwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu akiwa kwenye moja ya maduka yake katika Jengo la Msasani Mall, Dar ambalo nalo inadaiwa yeye ndiye analimiliki.
Taarifa za siku ya tukio zilibainisha kwamba Said alikuwa akizungumza na mfanyakazi wake mishale ya saa 1 jioni ndipo akatokea kijana mrefu, mwembamba ambaye alimmwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
 
Ilibainishwa kwamba mfanyakazi huyo wa Said, Hassan Ahmad naye alijeruhiwa kidogo katika purukushani hiyo lakini alipopelekwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, alitibiwa na kuruhusiwa huku bosi wake akipelekwa Afrika Kusini usiku huohuo.
 
Kwa vile mtu aliyemmwagia tindikali Said alifika eneo la tukio na pikipiki, Kamanda Wambura (RPC Kinondoni), alisema kuwa uhalifu kwa njia ya usafiri huo ni mkubwa sana, kwa hiyo kuna taarifa inaandaliwa.
 
“Uhalifu wa pikipiki hususan bodaboda ni tishio kwa nchi yetu kwa sasa, kuna taarifa inaandaliwa na itatolewa baadaye kuhusiana na mwongozo wa usafiri huo pamoja na namna ambavyo kama nchi, tutakabiliana na uhalifu kwa njia ya bodaboda.
“Kwa sasa mamlaka husika zinakaa. Zinajadili, siyo suala la kupuuza kabisa. Majambazi sasa wanatumia pikipiki, tunashuhudia kwamba hata watu wanaotaka kutekeleza njama za mauaji, nao wanatumia bodaboda. Ni hatari sana,” alisema Wambura.

UWAZI LINAMWOMBEA APONE HARAKA
Gazeti hili, linamtambua Said kama mfanyabiashara na mlipa kodi wa nchi yetu ambaye mchango wake ni mkubwa katika kulipa afya taifa kwa upande wa mapato na bajeti yake kwa jumla.
 
Said, vilevile ni mhisani wa kijamii, kwani kupitia kampuni yake ya Home Shopping Centre, aliwasaidia sana waathirika wa mafuriko ya Bonde la Mto Msimbazi, mwaka juzi.
Mfanyabiashara huyo, aliipa kila familia seti ya vyombo vya nyumbani pamoja na taa zinazotumia nishati ya mwanga wa jua.
 
Familia hizo ambazo idadi yake ilikuwa 655, zilipohamishiwa Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, Said alijenga madarasa ya shule ya msingi kwenye eneo hilo ili kusaidia upatikanaji wa elimu na kurahisisha huduma za kijamii.
CHANZO NI GLP

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate