EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 30, 2013

Mwanasheria Mkuu amgeuka Pinda.

*Awataka polisi wasitumie nguvu kubwa kudhibiti raia
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, amelitaka Jeshi la Polisi nchini, kuacha kutumia nguvu zilizopita kiasi, pindi linapokuwa likituliza ghasia.

Amesema, pamoja na kwamba jeshi hilo linaruhusiwa kisheria kutumia nguvu wakati wa kutuliza ghasia, nguvu hizo hazitakiwi kuzidi kipimo kwa kuwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria.

Jaji Werema alitoa kauli hiyo mjini hapa jana, alipokuwa akifungua mkutano wa mawakili wafawidhi wa Serikali, wakuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa mikoa na vikosi vingine vya polisi.

“Sheria inaruhusu polisi kutumia nguvu katika baadhi ya maeneo, lakini utaratibu lazima ufuatwe.

Banner 
“Tusitumie nguvu kubwa kupita kiasi, polisi mmejifunza kutumia mabomu, bunduki na mmejifunza pia kutumia bunduki na kulenga shabaha, usimpige mtu kichwani, hilo ni kosa, lenga kwenye mguu,” alisema Jaji Werema.

Kauli hiyo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, inaonekana kwenda kinyume na kauli iliyotolewa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda dhidi ya wanaokaidi maagizo ya polisi.Katika maelezo yake wakati akijibu swali na papo kwa papo aliloulizwa wakati wa Bunge la Bajeti lililopita, Waziri Mkuu Pinda, aliruhusu polisi wawapige raia pindi wanaposhindwa kutii sheria.

Wakati huo huo, jana Jaji Werema alilitaka Jeshi la Polisi nchini pamoja na wanasheria wa Serikali, kuacha tabia ya kuwabambikia kesi raia badala yake watafute ushahidi wa kutosha.

Alisema kama wanamfahamu mhalifu, wanatakiwa kutumia akili kwa kumkamata kwa kufuata utaratibu wala siyo kumbambikia kesi isiyo na ushahidi.

“Katika baadhi ya kesi tusimkamate mtu kama hatuna ushahidi wa kutosha, tunamkamata mtu siku ya Ijumaa ili tumkomeshe akae ndani halafu Jumatatu anatoka.

“Unamjua mtu ni mhalifu, lakini unashindwa kumkamata matokeo yake unambambikizia kesi ya mauaji, sio vizuri, tuache tabia hiyo,” alisema.

Alisema kwamba, kama polisi na wanasheria watafanya kazi kwa kufuata utaratibu, utafika wakati wananchi watajenga imani na vyombo vya dola kwa kuwa watumishi hao watakuwa wakizingatia maadili ya kazi yao.

Alitaka pia uwepo ushirikiano wa kutosha kati ya wapelelezi na wanasheria wa Serikali, kwa kuwa bila kufanya hivyo, hakutakuwa na mafanikio katika utendaji kazi wao.

“Kipindi hiki ni kigumu, tunahitaji kushirikiana zaidi kuliko kipindi chochote kingine, wapelelezi na waendesha mashtaka ushirikiano wenu siyo kitu cha hiari bali ni lazima, kwani kama hamshirikiani, hatuwezi kushinda vita dhidi ya uhalifu,” alisema.

Jaji Werema alisema ingawa mawakili wa Serikali wana mamlaka ya kuondoa kesi mahakamani, hawatakiwi kufanya hivyo bila kuwasiliana na kamanda wa upelelezi wa mkoa husika, ili kujenga uwazi na kuondoa mianya ya rushwa.

Aliwataka watendaji hao kuhakikisha wanakuwa waaminifu katika kutunza majalada ya kesi na kuhakikisha wapelelezi hao na mawakili wa Serikali wanafanya uamuzi wa haraka.

Alisema kwamba, kitendo cha watumishi hao kuchelewa kutatua malalamiko ya wananchi, kinawafanya wananchi wakose imani na vyombo vya dola na hivyo kuwapo ukiukwaji wa sheria kwa wananchi.

“Jinsi tunavyotenda kazi zetu, tunaweza kusababisha dola kuchukiwa, halafu ikichukiwa tuwalaumu waandishi, mimi nawaambia, watuandike tu kama tunakosea.

“Tuwe makini pia na mawasiliano yetu kwenye magazeti, sisi ni dola, tusiwasiliane kupitia magazeti, tusitupiane lawama, tuwe na mawasiliano mazuri kati ya ofisi ya DPP (Ofisi ya Mkurugenzi Mashtaka), Ofisi ya DCI (Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai) na siyo kuwasiliana kupitia magazeti,” alisema.

Awali, akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), Elizer Feleshi, alisema ofisi yake kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, imepokea agizo la Rais Jakaya Kikwete la kuwataka wahalifu kujisalimisha na wapo tayari kulitekeleza.

“Tunawaasa wahalifu watumie vizuri muda wa wiki mbili waliopewa na rais, vinginevyo watajutia vitendo vyao kwa sababu katika mkutano huu, tutajadili namna ambavyo tutawashughulikia wale ambao hawatatekeleza amri hiyo ya rais,” alisema.

Alisema mkutano huo ni miongoni mwa mikutano waliyoanzisha chini ya Jukwaa la Haki Jinai wenye lengo la kuwakutanisha wadau pamoja kujadili changamoto katika utoaji wa haki jinai.

Alisema changamoto mojawapo inayowakabili, ni kupunguza msongamano wa mahabusu na wafungwa magerezani na kwamba idadi yao imepungua kutoka wafungwa 45,000 mwaka 2003 hadi wafungwa 33,033 kufikia Julai mwaka huu.

Pamoja na hayo, alisema uwezo wa magereza yote nchini ni kuhifadhi wafungwa 29,552.
 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate