EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 29, 2013

Meya atishia kumuua Mbunge • Alitoa kauli hiyo mbele ya DC, akaachwa.

MEYA wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, amefunguliwa jalada polisi akidaiwa kutishia kumuua mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia (CHADEMA), katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemema, Amina Masenza.

Matata ambaye ni Diwani wa Kata ya Kitangiri aliyevuliwa uanachama wa CHADEMA mwaka jana kutokana na kusababisha mgogoro ndani ya chama mkoani Mwanza lakini alifungua kesi mahakamani kupinga uamuzi huo ambapo kesi hiyo bado inaendelea.

Hata hivyo katika hatua ya kushangaza, Septemba mwaka jana, Matata alichaguliwa kwenye mkutano ambao ulikuwa haukidhi akidi ya wajumbe ambao ni madiwani 14 na kwa mujibu wa sheria ndio wanaounda halmashauri hiyo mpya iliyomegwa kutoka katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini hapa, Kiwia alisema Matata alimtishia kumuua Julai 26, mwaka huu, katika kikao hicho na kwamba tayari amefungua jalada polisi mkoa Mwanza kulalamikia vitisho hivyo.

Kiwia alisema kuwa chanzo cha vitisho hivyo ni msimamo wake wa kumpinga Meya Matata kuongoza kikao hicho ambapo siku hiyo mbunge huyo alisimama na kumuomba Mkurugenzi wa Manispaa, Zuberi Mbyana, amteue mwenyekiti wa muda ili aongoze kikao.

Alisema kuwa alifikia uamuzi huo kutokana na madiwani wa CHADEMA kutomtambua Matata kama Meya wa Manispaa hiyo wakilalamikia uchaguzi uliomweka madarakani kuwa ulikuwa batili kwa vile alichaguliwa na madiwani sita wa CCM na CUF bila kuwepo madiwani wao nane.

“Siku ya kikao niliomba ateuliwe mwenyekiti wa muda aongoze kikao maana Matata si Meya wa Ilemela kisheria. Baada ya kusema hivyo, Matata alisimama na kusema angeliniua. 

Alirudia kauli yake mara mbili tena mbele ya mkuu wa wilaya, polisi na wajumbe wengine waliohudhuria kikao hicho,” alisema.

Kiwia alidai kushangazwa na kitendo cha mkuu wa wilaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya pamoja na askari waliokuwepo kikaoni kunyamazia tukio hilo na kushindwa kumkamata Matata na kumchukulia hatua.

Alisema kuwa kwa sasa ana mashaka na usalama wa maisha yake kwani kitendo cha mkuu wa wilaya kushindwa kumchukulia hatua meya huyo kinatia hofu juu ya usimamizi wa sheria.

“Kwa kweli nashindwa kuelewa utendaji wa mkuu huyu wa wilaya, yaani mtu anasimama mbele yake na kumtishia mtu maisha halafu yeye na askari wanakaa kimya tu,” alihoji.
Kiwia aliongeza kuwa baada ya vitisho hivyo, yeye pamoja na madiwani wenzake wawili wa CHADEMA, Rosemary Brown wa Kata ya Pasiansi na Gradis Kiwia wa viti maalumu walitoka nje ya kikao huku Matata akitishia kumfukuza udiwani Brown.

Alipoulizwa jana kuhusu tuhuma hizo za kutishia kumuua Kiwia, Matata alisema mbunge huyo asiogope kuuawa maana asipomuua yeye atauawa na wengine endapo hatapunguza mdomo.

Katika hatua nyingine, meya huyo anadaiwa kushikiliwa kwa muda na Jeshi la Polisi Wilaya ya Ilemela juzi kwa tuhuma za uchochezi.
Matata anadaiwa kuwahamasisha wananchi wa Mhonze kuwapiga mawe maofisa wa jiji la Mwanza watakapokwenda eneo hilo kugawa viwanja.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, polisi ilimshikilia kwa mahojiano zaidi kuhusu tuhuma hizo za uchochezi. Matata alikiri kuwaamuru wananchi wa kijiji cha Mhonze kuwafanya hivyo lakini alikanusha kuhojiwa na polisi badala yake alisema alikwenda kituoni kwa masuala mengine na si vinginevyo.

“Kweli niliwaapia wawapige mawe watu wa jiji maana watakwendaje kupima na kugawa viwanja eneo lisilo lao.”
Uchaguzi wa Matata ulikiuka kanuni na sheria za halmashauri. Kwa mujibu wa sheria ni kwamba akidi ya wajumbe iliyokuwa ikihitajika kwa ajili ya meya kupigiwa kura ni madiwani tisa badala ya madiwani sita walioshiriki kwenye uchaguzi huo.

Badala yake Matata alichaguliwa kuwa meya na madiwani sita pekee, wanne wa CCM na mmoja wa CUF baada ya madiwani wengine wa CHADEMA kususia mkutano huo wa uchaguzi.

Matata alichaguliwa wakati suala lake la kufukuzwa uanachama ndani ya CHADEMA likiwa bado linangojea uamuzi wa mahakama alikofungua kesi kupinga uamuzi wa chama chake.

CHANZO: TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate