EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 10, 2013

Mwanafunzi ajinyonga kwa kunyimwa mhindi.

WATU wawili wamefariki dunia akiwemo mwanafunzi wa shule ya msingi mjini hapa ambaye amejinyonga kwa kamba ya katani hadi kufa kwa madai ya kunyimwa mhindi na wadogo zake.

Kamanda  wa Polisi Tarime na Rorya, Justus Kamugisha alimtaja mwanafunzi huyo mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake kuwa ni Richard Charles (14)  anayesoma katika Shule ya Msingi St. Jude ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nyagisya, Kata ya Kiore.

Alisema waligundua mwanafunzi huyo kujinyonga Julai 6 mwaka huu baada ya kunyimwa mhindi wa kula na wadogo zake, hivyo kushindwa kuvumulia na kuchukua uamuzi wa kujinyonga kutokana na njaa aliyokuwa nayo.

Kamanda Kamugisha alisema baadaye mwili wake ulichukuliwa na polisi na kupelekwa katika hospitali ya wilaya ya Tarime kufanyiwa uchunguzi kisha kukabidhiwa ndugu na jamaa zake kwa ajili ya mazishi, na kwamba wanaendelea zaidi na upelelezi kuhusu tukio hilo.

Katika tukio jingine, Mtera Chacha (25) mkazi wa Kijiji cha Genkuru amefariki dunia baada ya kupigwa na kitu chenye ncha kali.
Tukio hilo lilitokea Julai 6 mwaka huu majira ya saa 6.00 mchana katika Kitongoji cha Nyabigena, Kijiji cha Kewanja, Kata ya Kemambo.

Chanzo kilitajwa kuwa ni Chacha kulisha mifugo katika shamba la mzee Mwita Mabya (83), na polisi wanaendelea kumuhoji aliyesababisha tukio hilo.
Katika tukio jingine, Mkwaya Mwita (48) mkazi wa Kijiji cha Gibaso amekatwa panga kiganjani hadi kutenganishwa na mkono wake na Marwa Mwita wa Kijiji cha Gibaso.
Kamanda Kamugisha alisema tukio hilo lilitokea jana na kwamba chanzo chake kinadaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Alisema majeruhi amelazwa katika hospitali ya serikali ya wilaya ya Tarime akipatiwa matibabu.
Pia Emmanuel Mseti (19) mkazi wa Kijiji cha Kegonga amejeruhiwa kwa risasi na askari wa hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Kamanda Kamugisha alisema kuwa mtu huyo alijeruhiwa kwa risasi katika kiwiko cha mkono wake baada ya kudaiwa kuingiza mifugo katika hifadhi hiyo ya taifa na kwamba hivi sasa amelazwa hospitali ya Bugando akipatiwa matibabu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate