EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 14, 2013

CHOMBEZO: KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA....SEHEMU YA.... 03..


Na IRENE MWAMFUPE NDAUKA
“Simu yako iko wapi?”
“Kule kwenye kibanda changu.”
“Nenda kailete haraka sana.”
Mlinzi alisimama na kutoka.  Mama Joy aliwaza mengi kichwani mwake wakati
anamsubiri mlinzi…
“Huyu lazima alimpigia simu mume wangu,
akamwambia mzoa taka amekuja, maana jana si alisikia baba Joy alivyokuwa
akikataza watu kuingia? Lakini yeye alisema hataki watu waingie usiku, sasa
kwani saa hizi usiku?”
“Halafu ni kweli itakuwa yeye maana
hawapatani tangu zamani. Hata leo yenyewe pale getini si walibalulana kidogo.
Atakuwa yeye tu. Baba Joy alikuja akidhani atamkuta mzoa taka, bahati nzuri
kashaondoka.”
Mara, mlinzi aliingia…
“Iko wapi?”
“Hii hapa.”
Mama Joy aliipokea simu hiyo na kusachi
namba zilizopiga kwa siku hiyo, hakukuwa na namba zilizopiga wala kupigwa…
“We unan’tania siyo..?”
“Hata kidogo mama…”
“Ina maana hii simu yako hujapiga simu wala
kupigiwa..?”
“Leo kuna wakati nilitoa laini. Kwa hiyo
kuna uwezekano namba zote zilizopigwa na nilizopiga zimefutika zenyewe.”
Mama Joy alikubaliana na hilo, lakini alijua
mlinzi alifanya hivyo makusudi. Yaani alipomwambia akachukue simu, mlinzi
alipofika alitoa laini au alifuta namba zote ili kupoteza ushahidi kama
alimpigia baba Joy…
“Haya nenda,” alisema mama Joy. Mlinzi
alisimama, akaondoka bila kuaga.
Nyuma, mama Joy alianza kufikiria vitu
vyake…
“Huyu mlinzi atakuwa adui wangu kwa mzoa
taka. Kama anaweza kumpigia simu mume wangu kumwambia kuna mwanaume ameingia ni
tatizo, tena kubwa sana.“Kinachoonekana, baada ya mume wangu kurudi
alimwambia ameshatoka ndiyo maana hata alipoingia ndani alifikia sebuleni. Tena
mbaya sasa amekuta mi natoka kuoga, si ndiyo hatari zaidi?
“Sasa hapa nifanyeje? Maana kama kutokea
limetokea. Nikisema nimchongee chochote kwa mume wangu atajua natengeneza bifu
kwa sababu anatoa siri zangu na mzoa taka, dawa yake hapa moja tu…” alisema
moyoni mama Joy kisha akabetua vidole, akasimama, akaingia ndani…
“Asumta,” alimwita mwanamke anayefanya kazi
ndani ya nyumba yake…
“Abee…”
“Kaniitie mlinzi.”
Asumta alitoka nje hadi kwa mlinzi, tena
kwenye kibanda chake…
“Fuko unaitwa na bosi wa kike.”
“He! Leo mama yangu umetoka nje, ajabu!”
“Unaitwa huko.”
Asumta na mlinzi huyo waliongozana hadi
ndani, Asumta akawa anapita, mlinzi akabaki sebuleni…
“Asumta…”
“Abee bosi…”
“Endelea na kazi zako, mimi nina maongezi na
Fuko…”
“Sawa bosi,” Asumta aliitika huku
akiinamisha kichwa kama ishara ya utii.
Mama Joy alisimama, akamfuata mlinzi kwenye
kochi alipokaa, akapiga magoti chini yake na kumshika mapajani…
“Niambie ukweli. Ulimpigia mume wangu simu
kumwambia..?”
“Kumwambia nini?”
“Kwamba mzoa taka ameingia..?”
“Lini? Leo?”
“Leo ndiyo.”
“Hapana, sijampigia.”
“Fuko…”
“Naam mama…”
“Usinifiche,” alisema mama Joy huku
akimshikashika sehemu mbalimbali za mwili mpaka kwenye flaizi ya suruali…
“Si…sija…m…mmmpigia,” mlinzi alianza
kupagawa na lile zoezi la kushikwashikwa sehemu za mwili…
“Ma…ma…ma…hu…huko
s…siii…ko…”
“Sema ukweli wewe. Kwanza huku ndiko.
Uli…ulimpigia simu baba Joy..?” alisema mama Joy huku akizidisha kumhamasisha
mlinzi wake huyo kwa kuendelea kumshika sehemu mbalimbali za mwili wake…
“Siiii…sija…sijampigia mama…kwe…kweli tena.”
Mama Joy naye alianza kupagawa, alianza
kuangusha ‘malalamiko’ ya mahaba huku akifumba na kufumbua macho yake makubwa
kama golori.
Sasa ukimya ulitawala, wote walikuwa
wakifanya mambo yao kwa vitendo huku wakiwa wamechanganyikiwa kwa mahaba.
Mama Joy akiwa bado amepiga magoti,
alimsimamisha mlinzi kisha na yeye akasimama na kusogea naye mpaka kwenye kochi
kubwa.
Mama Joy alijitupa, akamvuta mlinzi, naye
akajitupa tii. Hapakuwa na simile, mahaba yalitawala, yakapamba moto. Mama Joy
aligawa raha kwa mlinzi. Maswali kama, ‘ulimpigia simu baba Joy’ yakaisha
yakabaki manung’uniko ya mapenzi.
Mpenzi, mahabuba wangu, sweetheart, wa
rohoni zikawa ndiyo kauli kutoka kwenye kinywa cha mama Joy.
Alipofanikiwa kuvunja dafu tu, mama Joy
akaanza kutoa maonyo…
“Usije ukamwambia mtu lakini…”
“Sa…sawa,” alijibu mlinzi…
“Nihakikishie…”
“Kweli si…sitasema…”
“Ukisema je?”
“Nifukuze kazi…”
“Shauri zako, utafukuzwa kweli.”
Mara, mlinzi alianza kupiga kelele za
‘furaha’ za kufika mwisho wa kilele cha mlima…
“Usipige kelele sana basi, hausigeli
atatusikia, atajua, akijua atasema,” mama Joy alisema akiwa amemmiliki kifuani
mlinzi wake huyo huku akimkaribisha kwenye kilele cha furaha…
“Sa…sawa…” alisema mlinzi huku akizidi
kupiga kelele. Ilibidi mama Joy amuwekee kiganja kwenye midomo ili sauti
isitoke…
“Nimekwambia usipige kelele husikii, unataka
kunitafutia matatizo siyo?” alihoji mama Joy huku kiganja bado kikiwa kwenye
midomo ya mlinzi. Wakati huo mlinzi alipunguza kelele kwani alishasimama
kileleni kwenye mlima wa maraha.
Alitoka haraka kwenye kifua cha bosi wake,
akavaa sawasawa huku akiona aibu kwa mbali…
“Ukiwa mtulivu utafaidi vingi kutoka kwangu,
ukiwa hujatulia kazi itaota mbawa. Umesikia  mpenzi wangu?”
“Nitakuwa mtulivu ili nifaidi. Lakini mzee
si atajua..?”
“Utamwambia wewe..?”
“Mimi siwezi. Lakini wanasemaga wasomi
wanajua mambo mengi.”
“Hawezi kujua kama hataambiwa.”
“Yule mzoa taka je?”
“Mzoa taka hakuhusu wewe, nyamaza. Na ole
wako uzungumzie kuhusu mzoa taka.”
“Sitamzungumzia.”
“Haya nenda kazini kwako, lakini funga mdomo
wako.”
Mlinzi alitoka huku akisemasema maneno
anayoyajua mwenyewe.

***
Mama Joy aliingia chumbani kwake kwenda
kuoga. Alipomaliza alikwenda kukaa kwenye ‘dressing table’ na kujipodoa
vilivyo, pafyumu na manukato mbalimbali ili kuondoa shombo la wanaume hao wasio
na hadhi yake.
Alipomaliza, alikwenda jikoni kwa mfanyakazi
wake wa ndani na kuongea naye mawili matatu huku akimkazia macho ili aone kama
anajua chochote kuhusu kilichotokea…
“Pilipili umeweka za kutosha?”
“Ndiyo bosi…”
“Mchuzi uziwe kama ule wa juzi, umefuata
vile nilivyokufundisha?”
“Ndiyo bosi, wala hakuna shaka.”
Mama Joy alijiridhisha kwamba hakuna siri
yoyote anayoijua mwanamke huyo.

***
Saa moja jioni, mama Joy alipokea simu
kutoka kwa mumewe…
“Nina safari ya Arusha usiku huu. Nakwenda
kufanya makubaliano na wale jamaa wa Tanzanite…”
“Mbona ghafla baba Joy..?”
“Imebidi niende…”
“Kwa ndege au gari..?”
“Kwa gari…saa mbili na nusu asubuhi nitakuwa
na kikao nao.”
“Haya, safari njema mume wangu…”
“Oke, take
care…”
“Usijali mume wangu.”
Mama Joy alikaa sebuleni akijiuliza maswali
mengi kuhusu safari hiyo ya ghafla ya mumewe…
“Ni kweli au ananitega?”
“Si ajabu anataka kujifanya amesafiri ili
usiku arudi kimyakimya akijua atanifumania na mzoa taka. Amechelewa, kama mtoa
siri wake ni mlinzi naye nimemweka mikononi, yuko upande wangu sasa.”
Alitoka nje na kumwita mlinzi…
“We Fuko…”
“Naam bosi…”
“Njoo mara moja.”
Mama Joy alirudi sebuleni, akaa kumsubiri
mlinzi. Aliingia muda huohuo…
“Mzee amekupigia simu..?”
“Ndiyo bosi…”
“Amekwambiaje?”
“Amesema nifunge geti kwa kufuli yeye
hatarudi, anasafiri na wewe ameshakwambia…”
“Oke, vizuri sana kaendelee na kazi, ikifika
saa nne usiku uje hapa sebuleni kuna mambo muhimu tuongee.”
“Sawa bosi.”
Dakika tatu baada ya mlinzi kuondoka, mvua
kubwa ilinyesha huku ikiambatana na upepo mkali…
“Mh! Na kaubaridi haka ukipata mwanaume
akukumbatie kukupa joto…patanoga,” aliwaza mama Joy huku akijikunyata, akaguna
tena baada ya mvua kumwagika zaidi…
“Lakini si nimemwambia Fuko aje saa nne. Leo
hakuna kulinda. Atalala na mimi chumbani mpaka asubuhi, loo!”
Kwa mbali akasikia kama sauti ikisema…
“Na mvua hii mumeo si ataghairi kusafiri?
Sasa akija na kumkuta mlinzi chumbani unadhani ndoa ipo hapo?”
“Mume wangu hataweza kuingia ndani mpaka
afunguliwe  geti, mbaya zaidi mwenyewe
amemwambia mlinzi afunge geti kwa kufuli kwa sababu hatarudi tena leo, ana
safari ya Arusha,” mama Joy alisema kama anayeijibu ile sauti.
Lakini palepale alipata wazo la kumpigia
simu mumewe ili ajifanye anamuonea huruma kwa sababu ya mvua kubwa na safari.
Mama Joy aliamini kwa kuongea na mumewe atapata picha kama ameghairi safari au
la!
Bahati mbaya simu ilikuwa haipo hewani hata
pale alipopiga simu mara tatu hadi tano, baba Joy hakupatikana…
“Kha! Asa huyu vipi?” alijihoji mama Joy
akianza kupata wasiwasi kwamba, kweli mumewe anaweza kuzuka ghafla licha ya
kwamba hataweza kuingia ndani hadi apige simu lakini atakuwa ameondoa uhondo
kati yake na mlinzi. 
Saa nne juu ya alama, mlango mkubwa
uligongwa, mama Joy akiwa amejilaza sebuleni.
Alitoka kwenye kochi akaenda kufungua…
“Umefunga geti kwa kufuli kweli wewe Fuko?”
“Ndiyo mama…”
“Haya pita, lakini sasa nina wasiwasi na
kitu kimoja…”
“Kipi tena mama..?”

JE NINI KITAENDELEA ...USIKOSE...SEHEMU YA ....04... 
Kuwa na mimi hapa tena siku ya Jumatano itaendelea.....

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate