EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 7, 2013

Afutiwa kesi ya kumteka Ulimboka lakini ashtakiwa kwa kudanganya kumteka


Dar es Salaam. 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia mashtaka raia wa Kenya, Joshua Mulundi kuhusu kumteka na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka na sasa atakabiliwa na mashtaka ya kuidanganya polisi kuhusika kumteka daktari huyo.

Hakimu Warialwande Lema aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, alifikia hatua hiyo baada ya 
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), kuwasilisha hati ya kumfutia mashtaka hayo.
Hati hiyo ya DPP iliwasilishwa mahakamani hapo na Wakili wa Serikali, Beatha Kitau kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi umekamilika.

Akiwasilisha hati hiyo mahakamani, Wakili Kitau alisema DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya mshtakiwa, chini ya Kifungu cha 91 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashtaka. Kutokana na uamuzi huo wa DPP, Hakimu Lema alimfutia mashtaka Mulundi na kumwachia huru.
Hata hivyo, muda mfupi baadaye, alikamatwa na kufunguliwa kesi nyingine ya kutoa taarifa za uongo kwa Jeshi la Polisi.

Katika kesi hiyo mpya inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Aloyce Katemana, Wakili wa Serikali Mwandamizi Tumaini Kweka, alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Julai, 2012, katika Kituo cha Polisi Oysterbay.

Wakili Kweka alidai kuwa siku hiyo mshtakiwa akiwa kituoni hapo alitoa taarifa za uongo kwa maofisa wa polisi kuwa yeye na wenzake ndiyo waliokodiwa ili kumteka na kumdhuru Dk Ulimboka wakati akijua kuwa si kweli.
Mshtakiwa huyo alikana shtaka hilo.

Wakili Kweka alisema upelelezi wa kesi hiyo umeshakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa ili waweze kuandaa maelezo ya awali ya kesi hiyo. Pia aliweka pingamizi la dhamana dhidi ya mshtakiwa akidai hana makazi ya kudumu kwa kuwa si raia pia kwa ajili ya usalama wake kulingana na mazingira ya tukio hilo.

Kauli hiyo ya Wakili Kweka ilimfanya mshtakiwa huyo alipuke na kudai kuwa wanamfungulia kesi za uongo ambazo hahusiki na kudai kwamba wamepanga kumpoteza.

“Mheshimiwa Hakimu, naomba unisamehe, kwa kile nitakachokifanya, kwani nikirudi mahabusu mimi itaniumiza,” alidai mshtakiwa huyo na kusisitiza kuwa hahusiki na kwamba bado ni kijana mdogo.

Baada ya mshtakiwa huyo kulalamika hivyo, Hakimu Katemana aliutaka upande wa mashtaka uwasilishe hati ya kuzuia dhamana ambayo hata hivyo, hawakuwa nayo licha ya kuwaongezea saa mbili kuandaa.


Baada ya kushindwa, Hakimu Katemana alimpa mshtakiwa masharti ya dhamana, ambayo hata hivyo, naye hakuweza kuyatekeleza hivyo kurudishwa mahabusu, hadi Agosti 20, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa.

Masharti hayo ya dhamana yalikuwa ni kuwa na wadhamini wawili, mmoja akitoka katika taasisi inayofahamika, ambao wote na yeye, watasaini hati ya Sh5 milioni kila mmoja na kuwasilisha mahakamani hati zake za kusafiria.

Mulundi alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Julai 14, 2012 na kusomewa mashtaka mawili ya kumteka na kutaka kumuua Dk Ulimboka.

Katika kesi hiyo iliyosikilizwa na Hakimu Mkazi, Agnes Mchome, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ladslaus Komanya alidai kuwa Mulundi ambaye ni mkazi wa Murang’a, Kenya, alimteka Dk Ulimboka Juni 26, 2012 akiwa eneo la Leaders Club, Kinondoni.

Katika shtaka la pili, Wakili Komanya alidai kuwa tarehe hiyohiyo, akiwa katika eneo la Msitu wa Mabwepande Tegeta, Dar es Salaam kinyume na sheria, mshitakiwa huyo alijaribu kumsababishia kifo Dk Ulimboka.

Dk Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema Juni 27, 2012 akiwa hajitambui katika msitu huo wa Mabwepande huku akiwa na majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Mshtakiwa alifikishwa polisi, baada ya kwenda katika Kanisa la Ufufuo na Uzima Kawe la Josephat Gwajima, ambako alidai kuwa anataka kutubu kwa kuwa yeye na wenzake ndiyo waliomteka Dk Ulimboka.

CREDIT: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate