EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 23, 2013

Yanga: Tutawalipa Nsajigwa, Mwasyika •Kuwamwagia nyota wake sh mil. 100 za ubingwa.

KLABU ya Yanga imepanga kumalizana na nyota wake wa zamani, Stephano Mwasyika na Shadrack Nsajigwa, wanaoidai sh mil. 16, ikiwa ni siku chache tangu wafikishe madai yao Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuomba msaada wa kupata haki yao.

Habari zilizotufikia siku jana na kuthibitishwa na kiongozi mmoja ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe kwa sababu maalumu, Yanga isingependa kuingia kwenye mvutano na nyota hao, hivyo imepanga kumaliza suala hilo wiki ijayo.

Mbali ya Nsajigwa na Mwasyika pia chanzo hicho kimedokeza kuwa Yanga itatoa kiasi cha shilingi mil. 100 kwa wachezaji kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita uliofikia tamati Mei 18, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi kwao.

Chanzo hicho kilisema uongozi wa klabu hiyo unasikitishwa na madeni mengi waliyoyakuta wakati wanaingia madarakani Julai 15, mwaka jana, wamekuwa wakijitahidi kuyalipa kulinda hadhi ya klabu hiyo.

“Tumesikia juu ya kina Mwasyika na Nsajigwa, sisi kama viongozi wapya, kiukweli tumeumia sana hasa ukiangalia mchango wao kwa Yanga, ni kweli wanatudai, sisi tunahangaika kuyalipa madeni ambayo ni mengi,” alisema kiongozi huyo.

Alisema mbali ya wachezaji hao, wapo wengine ambao wamekuwa wakiwadai, hivyo wako mbioni kumaliza madeni hayo kwa lengo la kufanya kazi kwa ufanisi kama walivyotumwa na wapiga kura wao na kuongeza kuchelewa kulipwa ni suala la kawaida.

“Hata wewe kuna siku bosi wako anachelewa kukulipa, ila kuna njia za kuzungumza naye na ukiona amekwambia subiri kidogo, ujue anatafuta mbinu ya kumalizana nawe, na sisi tunajua wajibu wetu, hatuwezi kuwazima, ni haki yao,” alisisitiza.

Alipotafutwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Lawrence Mwalusako, alisema mpango wao ni kuwalipa wachezaji hao kwani ni kweli wanaidai klabu hiyo fedha ambazo ni haki yao kuzipata kutokana na jasho lao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate