EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 23, 2013

Kumekucha EBSS 2013 - Madam Ritha Poulsen.

WASHIRIKI 20 wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star Search (EBSS), wanatarajia kuingia kambini hivi karibuni jijini Dar es Salaam ili kuanza mafunzo rasmi yatakayofanikisha kupata washiriki bora katika shindano hilo linalotarajiwa kufikia fainali Novemba 17, mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Benchmark Productions Limited, ambao ndio waandaaji wa EBSS, Madam Ritha Poulsen, alisema shindano la mwaka huu linatarajiwa kuwa la aina yake kutokana na jinsi walivyojipanga na kupata washiriki wenye uwezo kutoka mikoani na jijini.

Ritha alisema wameazimia kuingia kambini mapema ili kuwapa fursa washiriki kujifunza zaidi na kuwa na uwezo wa kutosha, ambao utazalisha waimbaji wazuri katika tasnia ya muziki hapa nchini, kupitia kituo cha runinga cha TBC1.

“Mwaka huu washiriki ni wengi, ila tumewapata 20 bora na kutokana na mambo ya kibiashara, kwa sasa EBSS itakuwa inarushwa TBC1 kila Jumapili saa tatu usiku na marudio Jumatano saa 8 mchana, badala ya ITV, kuhama kwetu hakuna ugomvi wala nini ni mambo ya kibiashara, kwani nimeanza kusikia maneno mengine hususan kwenye ‘social media’, sisi hatuko huko, tuko kibiashara zaidi, zaidi ya hapo hakuna,” alisema Ritha.

Naye Balozi wa EBSS, mshindi wa mwaka jana, Walter Chilambo, aliwashukuru vijana kujitokeza kwa wingi katika mikoa mbalimbali ambayo wametembelea, hususan vijana wa kike, ambao walikuwa hawajitokezi kwa wingi.

Naye Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan, alisema wao kama wadhamini wakuu wa shindano hilo wamejipanga vya kutosha kuhakikisha linakuwa la aina yake mwaka huu.

Kwa upande wake, Meneja Vipindi wa TBC1, Edna Rajab, aliwahakikisha Watanzania kuwa watahakikisha kipindi cha EBSS kinarushwa kwa ubora wa hali ya juu kila Jumapili na marudio yake Jumatano.
Usaili wa EBSS mwaka huu umefanyika mikoa sita ambayo ni Arusha, Mbeya, Mwanza, Zanzibar, Dodoma na Dar es Saalam na sasa usaili unaendelea kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kusailiwa ‘live’, ambapo wanatakiwa wapige simu namba 0901551000 au kutuma ujumbe mfupi kwenda 15530, kama ilivyokuwa kwa mshiriki Meninah Atyk mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate