EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 17, 2013

Hatima ya dhamana ya Sheikh Ponda Leo.

Morogoro. 
Uamuzi wa dhamana ya mshtakiwa Sheikh Ponda Issa Ponda anayekabiliwa na mashtaka matatu unatarajia kutolewa Septemba 17 (leo) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, baada ya Mahakama hiyo kupitia vifungu vya sheria kutokana na upande wa utetezi kuwasilisha ombi la dhamana wakati upande wa mashtaka ukipinga dhamana ya kiongozi huyo.
 
Ombi la dhamana ya Sheikh Ponda liliwasilishwa mahakamani hapo Agosti 28 na wakili wake, Juma Nasoro mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Richard Kabate baada ya wakili huyo kuiomba Mahakama kumpatia dhamana kiongozi huyo kwa madai kuwa kutokana na mashtaka hayo, mteja wake kisheria anayo haki ya kupatiwa dhamana.

Pamoja na kuomba mteja wake kupatiwa dhamana, pia Wakili Nassoro aliwasilisha ombi la kupatiwa hati yenye maelezo ya mlalamikaji wa kesi hiyo ambaye ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani alidai kuwa anahitaji maelezo hayo kwa ajili ya kuandaa utetezi.

Licha ya kuwasilishwa maombi hayo mahakamani hapo, upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Bernad Kongola ulipinga dhamana ya mshtakiwa huyo kwa madai kuwa ombi hilo halina msingi wowote na kwamba kutokana na cheti kilichotolewa na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini DPP, kimepinga dhamana ya mshtakiwa huyo kwa maslahi ya usalama wa nchi.
Kutokana na mvutano kati ya pande hizo mbili, Hakimu Kabate aliahirisha kesi ili aweze kupata nafasi ya kupitia vifungu mbalimbali vya sheria, ambapo leo atatoa uamuzi wa kumpa ama kutompa dhamana mshtakiwa huyo ambaye anakabiwa na shtaka la uchochezi, kuharibu imani za dini za watu wengine na kushawishi kutenda kosa ambayo aliyatenda Agosti 10 mwaka huu eneo la Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro.

Pamoja na kutoa uamuzi wa dhamana, pia kesi hiyo itasomwa na kupangiwa tarehe ya kuanza kusikilizwa, kwani upande wa mashtaka ulidai kuwa umekamilisha upelelezi ambapo wanatarajia kupeleka mashahidi 15 na vielelezo zikiwamo DVD mbili na kibali cha kongamano la Eid lililoandaliwa na Umoja wa Wahadhiri Mkoani Morogoro ambalo mshtakiwa alitenda makosa hayo akiwa katika kongamano hilo.
CREDIT MWANANCHI.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate