EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, September 29, 2013

HOT NEWS: MTOTO ALIYEFARIKI MIAKA MIWILI ILIYOPITA AONWA NA MAMA YAKE AKIWA HAI‏.

  •   Mtoto Shabani Maulidi akiwa tayari melala kitandani katika hospitali ya wilaya ya Geita.
       Mama mzazi wa mtoto Shabani menye kilemba kichwani akiwa amepigwa bumbuazi  maeneo ya hospitali.

     Eneo ambalo mawe yanaonekana nyuma ya nyumba ndipo Mtoto huyo  alipo zikwa

    Wadogo zake na Shabani nao wakiwa wameshikwa na mshangao kama walivyokutwa  nyumbani kwao.

    WATU WAPIGWA BUMBUWAZI
    WANANCHI WAMIMINIKA HOSPITALI KUSHUHUDIA
    Na Denice Stephano-Geita yetu Blog                                 

    MTOTO anayedaiwa kufariki miaka miwili iliyopita  na kufanyiwa matanga ameonekana  akiwa hai  Septemba 28 majira ya mchana baada ya kukutana na mama yake mzazi uso kwa uso  wakati akienda kwenye shughuli zake za kibiashara.

    Mtoto huyo Shabani Maulidi (15) alifariki tarehe 03.01.2010 alishindwa kurudi nyumbani kwao tarehe 01.01.2011  wakati alipokuwa amepeleka Mbuzi machungani kisha kushindwa kurudi nyumbani na baadaye kuonekana baada siku tatu akiwa amefia kwenye kisima cha maji.

    Kwa mujibu wa Baba mzazi wa mtoto huyo Maulid Shabani alisema mtoto wake hakurudi nyumbani siku hiyo waliendelea kumtafuta bila mafanikio na ndipo baada ya siku tatu walimkuta akiwa amefia ndani ya kisima cha maji kilicho maeneo ya Kijiji cha Nyankumbu Kitongoji cha Mwembeni.

    Baba huyo alisema baada ya hapo walitoa taarifa Polisi kisha waliruhusiwa kuuchukua mwili wa mtoto wao na kwenda kuuzika nyumbani kwa kitongoji cha 14 Kambarage ndani ya mji wa Geita.

    Alisema walifanya shughuli zote za matanga na wakajua tayari mtoto wao ameishafariki na kwamba hawakuwa na wazo lolote na kumpata siku zote akiwa hai kama ilivyotokea  akisema ni tukio la kustaajabisha kwake.

    Mama mzazi wa mtoto huyo Aziza Ramadhani akisimulia namna alivyokutana na mtoto wake alisema alikuwa akienda kwenye shughuli zake za ujasiriamali kama mfanyabiashara ya mbogamboga akiwa amefika eneo la Nyankumbu nje kidogo sana na mji wa Geita eneo la Mwembeni alikutana uso kwa uso na  mtoto wake.

    Alisema alipomuona alimwita kwa jina lake akisema "mwanagu Shabani ni wewe naye akamwitikia ni mimi kisha alimshika mkono huku akiwa haamini macho yake ndipo alipompigia simu mumewe naye akaja wakamchunguza vizuri wakaabaini  kuwa ndiye mtoto wa Shabani aliyesadikiwa kuwa alifariki na kuzikwa.

    Akithibitisha zaidi mama wa mtoto huyo alisema mwanae alikuwa na alama ya kinundu kwenye paji la uso na mguuni akiwa na alama ya kovu mguuni iliyosababishwa na kuchomwa na mwiba pia alikuwa na mwanya uliofanan na wa baba yake mzazi.

    Mtoto huyo aliyevuta hisia za watu wengi  mjini Geita ameendelea kuthibitishwa na walimu wake wa shule ya Msingi Mwatulole alikokuwa anasoma darasa la tano kabla ya kifo hicho cha utata kwa sasa.

    Akiongea na Mwandishi wa Geita yetu Blog Makamu mkuu wa shule ya msingi Mwatulole Joseph Nungula aliyekuwa akifuatilia kwa karibu tukio hilo alisema kweli mtoto huyo anaonekana ni yeye bila kutia shaka yoyote .

    Mwalimu huyo alisema amemtambua mtoto huyo kwa sura na alama hasa ya usoni huku akimwelezea mtoto huyo kuwa alikuwa na mahudhurio mazuri shuleni pia maendeleo yake kitaaluma yalikuwa mazuri.

    Mtoto huyo ambaye anaendelea kupewa huduma ya kitabibu katika Hospitali ya wilaya ya Geita kwa uchunguzi zaidi wa kiafya anaongea kwa shida wanapokuwepo watu watu wengi hata hivyo amemtambua Baba na mama yake mzazi ambapo wanapomuuliza baadhi ya maswali anawajibu.

    Jeshi la Polisi mkoani hapa ambalo lilikuwa likiwa likifuatilia tukio hili kwa ukaribu sana limethibitisha kutokea kwa tukio hili huku wakiahidi kuendelea kutoa habari zaidi ambazo tutaendelea kuwajulisha huku wananchi wakisubiri kibali cha mahakama kufukua kaburi alililokuwa amezikwa mtoto huyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate