 Hamis Kiiza (20) akishangilia bao alilofunga dhidi ya Ruvu Shooting leo pamoja na Kavumbagu, Niyonzima, Msuva na Chuji
Hamis Kiiza (20) akishangilia bao alilofunga dhidi ya Ruvu Shooting leo pamoja na Kavumbagu, Niyonzima, Msuva na Chuji
Young
 Africans Siku ya jana imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Ruvu 
Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika dimba la 
uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans ambayo katika mchezo wake wa mwisho ilipoteza kwa 
kufungwa na Azam FC mabao 3-2 iliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha
 inapata ushindi katika mchezo huo na ndivyo ilivyokua.
Ikiwatumia
 washambuliaji wake Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu, Saimon Msuva na 
Mrisho Ngassa, Young Africans ilifanya mashambulizi kadhaa langoni mwa 
timu ya Ruvu Shooting lakini kutokua makini kwa washambuliaji wake 
kuliiinyima bao la mapema.
Dakika ya 27, Saimon Msuva alipoteza 
nafasi ya wazi ya kufunga akiwa yeye na mlinda mlango Abdu Juma Seif 
huku Hamis Kiiza pia akishindwa kutumia nafasi kama hiyo dakika ya 33 ya
 mchezo.
Washambuliaji wa Ruvu Shooting  walifanya mashambulizi 
langoni mwa goli la Yanga kupitia kwa Cosmas Lewis, Jerome Lembele na 
Elias Maguli lakini umakini wa walinzi wa Yanga ulikuwa kikwazo kwao 
kuweza kuziona nyavu za Ally Mustapha 'Barthez'.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza, Young Africans 1-0 Ruvu Shooting.
Kipindi
 cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko kwa kumuingiza Athuman 
Idd 'Chuji aliyechukua nafasi ya Frank Domayo mabadiliko yaliyopeleka 
watoto wa Jangwani kuutawala mchezo katika sehemu ya kiungo.
Dakika
 ya 63 mshambuliaji Hamis Kiiza aliipatia Yanga bao la kwanza na la 
ushindi baada ya kuitumia vizuri krosi ya Mrisho Ngassa aliyemtoka 
mlinzi Stephano Mwasika na kupiga krosi iliyomkuta mfugaji aliyefunga 
bao hilo maridadi na la msimu. 
Mara baada ya bao hilo Yanga 
iliendelea kufanya mashambulizi langoni mwa Ruvu Shooting lakini mpira 
uliopigwa na Didier Kavumbagu uliokolewa na golikipa Abdul Juma Seif na 
kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 1- 0 Ruvu Shooting.
Mara
 baada ya mchezo kocha mkuu Ernie Brandts amesema anashukuru vijana wake
 wamepigana kuhakikisha wanapata ushindi katiika mchezo wa jana, ukizingatia
 timu ilikua imetoka kupoteza mchezo wake wa mwisho.
Ushindi huu 
wana Yanga wote, tunaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo
 unaofuata dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya jumamosi ijayo. 
Young Africans: Mustapha, Twite, Luhende, Yondani, Nadir, Domayo/Chuji, Msuva.Nizar, Niyonzima, Kavumbagu, Kiiza, Ngassa 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment