EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 12, 2013

KAWAIDA SANA, MWEZI MZIMA BILA STORI!

KILA mmoja angependa awe peke yake katika umiliki wa mwenza wake, hata kama yupo kwenye mitala. Unapokuwa mmiliki halali, unakuwa na mamlaka ya kudhibiti mali yako kwa kila hatua, pasipo kuwa na shaka. Kuna watu, hasa wanaume, huchukia sana wanapoulizwa na wenza wao pale walipo, wanaona kero. Wapo wanaowajibu vizuri wenzao, lakini wapo ambao hutoa maneno makali, kana kwamba kukataa wasiwe wanaulizwa ulizwa walipo.

Nani akuulize ulipo zaidi ya mwenza wako? Mwanzo wakati mnakutana, maswali haya huwa chagizo kubwa sana, kila mmoja hupenda kumuuliza mwenzake alipo, anafanya nini, atarudi saa ngapi na zawadi gani atarudi nayo.

Taratibu mambo huanza kubadilika watu wanapokuwa wamezoeana, raha zetu za wakati ule zinaanza kuwa karaha. Hivi karibuni nilikutana na rafiki yangu mmoja aliyenipa mkasa wake na mke wake. Aliniambia wamekorofishana sana kiasi kwamba hivi sasa anahisi ndoa yake inaweza kuanguka wakati wowote.

Alinipa sababu hasa za hali kufikia hapo. Kitu kikubwa kilichosababisha hali hiyo ni kitendo cha mkewe kumchunguza sana, hasa kuikagua simu yake na kufuatilia kila simu au sms zinazoingia.

Kitendo hicho kilimkera, akaamua kumpiga mke wake na sasa wana wiki ya pili hawaongei na hakuna dalili kama hali hiyo inaweza kubadilika katika siku chache zijazo. Ana hofu, huenda mwanamke akaamua kurudi kwao!

Nilimpa moyo. Kama mmegombana hadi kupigana na hii ni wiki ya pili sasa, uwezekano wa kuondoka ni mdogo. Lakini pia, nilimtaka kutambua kwamba misuguano katika maisha ya kimapenzi ni jambo la kawaida kabisa.

Usishangae kusikia watu wamekaa ndani ya nyumba yao wiki mbili bila kuzungumza, hili lipo na litaendelea kuwepo katika ulimwengu wa mapenzi.
Yanayotutokea katika nyumba au uhusiano wetu, yana nafuu kuliko ya wenzetu ambayo hatuyajui. Usione mtu na mkewe wanacheka na kuonyesha furaha kubwa mnapowatembelea majumbani mwao, huwezi jua, huenda huu ni mwaka sasa hawazungumzi.

Mwanaume anatekeleza majukumu yake ya kulea familia kama kawaida, anasomesha watoto, anaacha hela ya kula mezani, anawajali watoto. Mama naye anakuwa kama hivyo, anatimiza majukumu yake vizuri, anawaogesha watoto, anahakikisha hawakosi shule. Na wote kwa pamoja, wanakuwa kitu kimoja kwa wageni wanaofika, awe ndugu wa mama au wa baba, siyo rahisi kugundua kama kuna tofauti yo yote.

Watafanya hayo yote vizuri, lakini linapokuja suala la wao wawili, hakuna kupiga stori, kila mtu kimpango wake. Chumbani baba yuko bize na simu yake, hali kadhalika mama naye yupo bize kivyake.

Wakati nikiwashauri kuwa watulivu wakati wa hali kama hii, ni vyema pia kukumbuka kwamba migogoro inayosababisha hali hii, ni hatari, siyo tu kwa ustawi wa familia husika, bali hata nje yao.

Upendo wetu, iwe kwa watoto, majirani na ndugu huwa ni unafiki. Hatuwezi kuwapenda wapendwa wetu endapo sisi wenyewe tumenuniana. Tutashindwa kuwaelekeza watoto kwa sababu kila mmoja atapunguza umakini kwa makusudi!   
CHANZO NI GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate