EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 12, 2013

MAWAZIRI WANNE KUSULUHISHA WAKULIMA NA WAFUGAJI MVOMERO

MAWAZIRI wanne wa wizara zenye dhamana ya mifugo, kilimo, ardhi na usalama, wametumwa wilayani Mvomero mkoani Morogoro kutafuta suluhu kwenye mgogoro kati ya wafugaji na wakulima katika Bonde la Mgongola.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, ndiye Mwenyekiti wa ujumbe huo uliotumwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenda kutafuta suluhu.
 
Mbali na mawaziri husika, Mbunge wa Mvomero ambaye ni Naibu Waziri wa Habari ,Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla alihudhuria kikao cha mawaziri hao, kabla ya mawaziri hao kukutana na wananchi kusikiliza hoja zao.
 
Katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika Kijiji cha Mkundo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye, alisema mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu na kusababisha mauaji ya mara kwa mara.
 
Alisema shauri kuhusu mgogoro huo ulioko mahakamani halijamalizika na kesi hiyo imekuwepo Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi bila kusikilizwa kwa miaka minane sasa.
 
Hata hivyo alisema hawawezi kuingilia Mahakama isipokuwa amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara yake, kusukuma suala hilo lipewe kipaumbele na limalizwe mapema.
 
“Tutashauri Mahakama isikilizwe, na ikimalizika pande mbili hizi zikutane ili kufikia muafaka wa kudumu,” alisema Medeye.
 
Aliagiza mamlaka za upimaji ardhi, zihakiki upya kujua wamiliki wa ardhi husika na baada ya hapo, eneo hilo lipimwe na watu wamilikishwe na wenye haki wafaidike nalo.
 
Katika mkutano huo, Chiza alisema ni muhimu matatizo ya wananchi yafanyiwe kazi kwa haraka na kutoa majibu sahihi kwa wakati badala ya kusubiri matukio ikiwemo mauaji.
 
“Tusifanye kazi kwa kusubiri matukio kama haya ya mauaji, tufanyie kazi masuala ya ardhi bila kusubiri kutokea maafa, nafikiri sasa tujisahihishe... siyo waziri aje hapa kuona watu wameuawa,” alisema Waziri Chiza.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, akizungumza kwenye mkutano huo, alieleza kutoridhishwa na utendaji kazi wa Polisi hasa katika operesheni ya kukamata ya watuhumiwa wa vurugu kutoka pande zote.
 
Dk Nchimbi alishangazwa kuona watuhumiwa 32 waliokamatwa wakati wa vurugu na mapingano hayo, wafugaji wakiwa wawili pekee.
 
Alisema katika mapigano hayo, watu sita waliouawa na kati ya hao wakulima ni wanne na wafugaji ni wawili na kuwakamata wakulima wengi tofauti na wafugaji, kunaleta maswali na shaka.
 
Waziri Nchimbi alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, kusaka watuhumiwa wengine hususan wafugaji waliohusika kwenye vurugu na mauaji hayo.
Aliagiza watuhumiwa wachujwe haraka na watakaobainika kutohusika waachiwe mara moja.
Awali, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo David, alitaka wafugaji kufuata utaratibu wa sheria na kuzingatia nchi ina wakulima, wafanyakazi na wafugaji.
 
Alisema sababu za wafugaji kwenda maeneo ya wakulima ni ukosefu wa miundombinu maeneo ya vijijini hasa majosho na maji. Dk Mathayo alitaka halmashauri zenye maeneo ya wafugaji ziweke miumbombinu kwa ajili ya mifugo.
CHANZO HABARI LEO

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate