EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 13, 2013

Wingu zito, Dk. Mvungi afariki

MJUMBE wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Sengondo Mvungi (61), amefariki, katika hospitali ya Milpark, nchini Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu zaidi.
 Marehemu Dk. Sengondo Mvungi enzi za uhai wake.
Dk. Mvungi, mwanasheria maarufu nchini na mwanachama wa NCCR-Mageuzi, alivamiwa Novemba 3, mwaka huu saa 6:30 usiku na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi, nyumbani kwake Kibamba, Kata ya Mpiji Magohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kujeruhiwa kwa mapanga sehemu za kichwani na usoni.

Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema kuwa wamepokea kwa masikitiko taarifa hizo na kuwa chama hicho kimepoteza kiongozi makini, na pengo lake haliwezi kuzibika.

“Ni kweli tumepata taarifa hizo, mwenzetu hatunaye tena, ni huzuni kwa chama na Watanzania tutamkumbuka kwa mambo mengi ndani ya chama, hata taifa,” alisema.

Alisema kuwa Dk. Mvungi alifariki dunia jana saa 9:30 katika hospitali hiyo ambako alihamishiwa Novemba 8, mwaka huu akitokea katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI).

Naye Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, alisema kuwa wamepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo Dk. Mvungi.

Mbowe alisema kuwa CHADEMA kinatoa pole kwa familia, chama cha NCCR-Mageuzi, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na Watanzania wote kwa kupoteza mtu makini na muhimu katika mustakabali wa taifa letu.

“Nimepokea taarifa hizo kwa masikitiko kwa kuwa Dk. Mvungi ni mmojawapo wa waasisi wa mageuzi nchini, ambaye hakukata tamaa kutumia taaluma yake. Mungu ana mipango yake, huyu ndugu alijitahidi kupigania suala la katiba mpya kwa miaka 20, na akateuliwa aiandae, tunasikitika kwa kuwa hataona katiba mpya yenye mawazo yake,” alisema.

Alisema kuwa tume inapaswa kuendeleza mawazo na michango aliyokuwa akisaidia katika kuandaliwa kwa katiba mpya.

Aidha, taarifa ya kifo cha mwanasheria huyo ilisambaa kwa kasi katika mitandao mbalimbali ya kijamii, huku wadau wa mitandao hiyo wakionekana kushitushwa na kuwataka Watanzania kuwa na subira kwa wakati huu mgumu.

Baadhi yao walienda mbali zaidi na kuhoji juu ya mchakato wa kupata katiba mpya utakapoishia kutokana na kuwa mwanasheria huyo ni mtu muhimu kwenye majukumu ya tume, kwani amebobea katika masuala ya katiba.

Aidha, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Bashe, katika ukurasa wake aliandika kuwa wahalifu wamekatisha uhai wa kiongozi huyo wakati akitekeleza jukumu zito kwa ajili ya maslai ya taifa letu.

“Dk. Sengondo Mvungi is no more, taarifa zilizonifikia kutoka Millpark hospitali ndugu yetu Dk. Mvungi amefariki saa 9:30. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,” alisema Bashe.

Alisema kuwa jambo hilo linaumiza sana na Mungu atalipia uhalifu huo, na kuitaka Tume ya Mabadiliko ya Katiba na NCCR-Mageuzi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Dk. Mvungi alivamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana ambao kwa mujibu wa Mbatia, kabla ya kuvunja milango ya nyumba, walilipua kitu ambacho kilitoa moshi mwingi na cheche kisha kuingia ndani na kuanza kudai wapewe fedha.

Mbatia alisema kuwa hatua hiyo ilisababisha Dk. Mvungi kupambana nao bila mafanikio, ndipo wakamjeruhi vibaya kwa kumcharanga mapanga kichwani, usoni na kisha kuondoka na kompyuta mpakato (Laptop) yake, pisto na kiasi cha fedha ambacho hakijajulikana.
Mbatia alisema majirani na ndugu walifanikiwa kumbeba Dk. Mvungi na kumkimbiza katika hospitali ya Tumbi mkoani Pwani ambako alipatiwa matibabu ya awali na kisha kuhamishiwa Muhimbili saa 10:00 alfajiri.

Dk Mvungi ambaye alikuwa hajitambui alitolewa na kuingizwa kwenye gari la wagonjwa lenye namba za usajili STK 8767, akipelekwa katika Hospitali ya Aghakan kwa ajili ya kufanyiwa kipimo cha CT-SCAN kwa ajili ya kuona ameathiriwa vipi katika eneo la kichwa.

Alilazimika kupelekwa kupimwa kipimo hicho Aghakan na kisha arejeshwe kwa sababu uongozi wa MOI uliwaeleza kuwa mtaalamu anayefahamu kutumia kipimo hicho hakuweza kupatikana mara moja.
CHANZO NI TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate