EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 6, 2013

HUOGOPI SKENDO, HALAFU UNAJIITA STAA!

AUNT Ezekiel ni muigizaji wa filamu mwenye jina kubwa, linaloenda sambamba na muonekano wake wenye mvuto, hasa anapovaa mavazi yake yanayoonyesha baadhi ya sehemu muhimu za mwili wake.

Kwa wasiomfahamu vizuri, Aunt ni mtoto wa mwanasoka mahiri wa zamani wa Simba na Taifa Stars, marehemu Ezekiel Greyson, maarufu zaidi kwa mashabiki wa kabumbu kama Jujuman. Alitamba katika miaka ya sabini na mwanzoni mwa themanini.

Ni mmoja wa wasichana waliofanikiwa kupata majina makubwa, ingawa uwezo wake kama muigizaji, bado haujakidhi viwango!

Hivi karibuni Aunt, mke wa mfanyabiashara Sunday Demonte, kijana wa Kitanzania anayefanyia shughuli zake Ughaibuni, alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kuwa haogopi kukutwa na skendo, kwani hilo ni jambo la kawaida.

“Mimi sijali, ninachoangalia ni kuingiza kipato, mambo mengine shauri yao, kuna watu wananichukia na kunitungia uongo, huwezi kupendwa na kila mtu, msanii ni kioo cha jamii, lazima upate skendo ili uweze kujirekebisha,” Aunt alinukuliwa akiliambia gazeti hilo.

Ninazifahamu kidogo kazi alizoshirikishwa, nyingi kati ya hizo akicheza na marehemu Steven Kanumba. Aina ya uigizaji wake haubadiliki, ni Aunt yule yule anayependa kuvaa nguo zenye kuonyesha nje sehemu kubwa ya matiti yake, maungo yake na hata mavazi yake mara zote ni yenye utata mkubwa.

Muigizaji mzuri ni yule mwenye kubadilika. Leo anaweza kucheza vizuri kama changudoa, kesho yake akafiti kiufasaha kabisa kama mtoto yatima anayeishi katika umaskini mkubwa, kabla ya keshokutwa kumkuta akiigiza vyema akiwa ni msomi mwenye mafanikio makubwa kimaisha!
Sifa hizo Aunt Ezekiel, kama walivyo mastaa wengi wa Tanzania katika filamu, hana. Ni muigizaji wa kuigiza matanuzi, demu bomba mwenye mitoko mingi, mikogo na mambo kama hayo, ndiyo maana hata mavazi yake, uigizaji wake ni wa aina ileile katika filamu zote alizocheza!

Anasema haogopi skendo, anajali kuingiza kipato. Anahitimisha kwa kukiri kwamba skendo ni jambo la kawaida kwa mastaa, kwani kwa kutokea hivyo, ndipo wao hupata nafasi ya kujirekebisha!

Hawa ndiyo aina ya wasanii tulio nao, wenye wafuasi lukuki mtaani, wanaosimama na kusema wazi kuwa hawaogopi skendo. Mtu makini na hasa anayetakiwa kuwa mfano, hawezi kuwa haogopi skendo!
Ndiyo maana kumbe kila siku tunasikia, mara kapiga picha za nusu utupu na kuzitupia katika mitandao ya kijamii ili watu waone ‘figa’. Mara amepigana na mwenzake club (bila chanzo hasa cha ugomvi kuelezwa, ingawa ni rahisi kuamini walikuwa wakigombea bwana).

Ninaheshimu maoni yake ya kutoogopa skendo, lakini napingana naye kwa kauli kuwa ni kawaida kwa mastaa kupata skendo. Siyo kweli. Wapo mastaa wakubwa, tena wale wanaojua kazi, lakini hawajawahi kuwa mabingwa wa skendo.
Riyama Ally ni mmoja ya waigizaji ‘wanaojua’ kwa levo za Bongo, lakini siwezi kumuweka katika orodha ya wauza sura wanaotumia tasnia kwa malengo yao binafsi.
Wasanii wetu wanaponzwa na uwezo wao mdogo wa ubunifu, ndiyo maana bado wanaamini katika skendo ili kuwaweka juu. Mtu anajisikia vizuri akiandikwa gazetini, bila kujali anaharibu vipi ‘image’ yake kwa jamii. Eti wanasingiziwa, hivi kuna mtu gani makini anaweza kukubali kunyamaza gazeti linapoandika uongo dhidi yake?
Kuna namna moja tu unayoweza kuwazungumzia hawa mastaa wetu wa aina hii, kwamba wanatengeneza skendo makusudi ili wavutie macho na masikio ya wahanga wa ngono!
CREDIT:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate