EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 6, 2013

WEMA YAMKUTA YA KAJALA

Stori: Imelda Mtema na Richard Bukos
KICHEKO! Ile kesi ya kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni Meneja wa Hoteli ya Mediteranian iliyopo Kawe Beach, Dar, Godlucky Kayombo iliyokuwa ikimkabili Wema Isaac Sepetu imetolewa hukumu yake kama ilivyokuwa ile ya shosti’ake, Kajala Masanja.

Wema Sepetu akitinga Mahakama ya Mwanzo ya Kawe, Dar.
Habari kutoka kwa chanzo makini cha gazeti hili kilieleza kuwa Wema alihukumiwa kifungo cha miezi mitatu au faini ya shilingi laki moja kwa maana ya elfu hamsini kwa kila kosa baada ya kukutwa na hatia ya kutenda makosa hayo mawili ya kupiga na kutukana.

WEMA AOMBA IHARAKISHWE
Habari za ndani kutoka kwa mtu wa karibu wa Wema au Madam zilieleza kuwa hukumu ya kesi hiyo ilikuwa iahirishwe lakini staa huyo akaomba itolewe kwa kuwa alitaka kusafiri.
Ilisemekana kuwa mbali na kuwa na safari pia aliomba itolewe kwa sababu yupo ‘bize’ na maandalizi ya arobaini ya baba yake, Isaac Sepetu aliyeaga dunia hivi karibuni.

Hukumu hiyo ilitolewa katika Mahakama ya Mwanzo ya Kawe, Dar ambako ndiko kesi hiyo ilipokuwa ikirindima tangu mwezi Agosti, mwaka huu.

Wema Sepetu na rafiki zake wakijadiliana jambo eneo la Mahakama ya Mwanzo ya Kawe, Dar.
ASUBIRIWA KUPELEKWA GEREZANI, ACHOMOA ‘MADOLARI’
Ilielezwa kuwa katika hukumu hiyo iliyosomwa kwa takriban saa mbili, Wema alikuwa akisubiriwa nje tayari kupelekwa gerezani lakini kama kawaida yake fedha iliongea ambapo alizamisha mkono laini kwenye ule mkoba wake na kuchomoa ‘madolari’.
Chanzo kilidai kuwa zilihitajika fedha za Kibongo hivyo Wema alichambua mkoba wake na kutoa ‘wekundu’ kumi huku akirejesha zile dola za Kimarekani.

“Wema alifanya kama alivyomfanyia Kajala siku ile pale Kisutu. Kwa Wema ishu ya fedha siyo tatizo sana. Kuliko kumpotezea muda, Wema yupo tayari kutoa kiasi chochote cha fedha.
“Kwa Wema muda ni kitu cha muhimu zaidi kuliko hata hiyo fedha ndiyo maana alitoa tu hiyo faini mara moja,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupokea maelezo hayo, gazeti hili lilimsaka Wema ili kupata mzani wa habari hiyo lakini simu yake iliita bila kupokelewa.

Wema na shosti wake Kajala wakitoka mahakamani hapo.
Hata hivyo, alipotafutwa meneja wake, Martin Kadinda na kuulizwa juu ya suala hilo alifunguka:
“Ile kesi iliisha tangu Ijumaa iliyopita, watu hawakujua tu. Wema alihukumiwa kifungo cha miezi mitatu au faini ya shilingi laki moja.

“Alichokifanya Wema alilipa faini hiyo na sasa yupo freshi na mishe zinaendelea. Unajua haruhusiwi kufanya mahojiano hadi amalize arobaini ya baba yake.”
Chanzo kilisema kuwa kabla ya hukumu hiyo, Wema alikuwa katika hali kama ile iliyomkuta Kajala wakati wa hukumu yake miezi kadhaa iliyopita kwani alikuwa akilia, kujuta na kumuomba Mola amuepushe na balaa hilo lililosababishwa na kuwa ‘tilalila’.

Hata hivyo, hukumu hiyo iliwashangaza watu kwani iliendeshwa kwa muda mrefu na kwa mbwembwe nyingi lakini hokumu yake ikawa ya kawaida tofauti na matarajio ya wengi.
Wema Sepetu na kampani yake wakiondoka eneo la mahakama.
KAJALA NAYE KICHEKO TENA
Wakati Wema akikenua, wiki hii Kajala naye ilikuwa chereko chereko baada ya  Mahakama ya Rufaa Kanda ya Dar kuridhika na hukumu yake iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mapema mwaka huu kufuatia rufaa iliyokatwa na mume wa staa huyo Faraji Chambo.

Katika kesi ya awali, Kajala alihukumiwa kifungo cha miaka mitano au faini ya Sh. milioni 13 baada ya kupatikana na hatia ya kushirikiana na mumewe kwenye msala wa kutakatisha fedha haramu wakati mwanaume huyo akifanya kazi Benki ya NBC, Dar.
Hata hivyo, Wema alimlipia faini hiyo kama alivyofanya kwenye kesi yake.

Katika hukumu ya rufaa hiyo, majaji walijiridhisha kwamba kesi hiyo iliendeshwa ipasavyo na Kajala alitimiza taratibu za kuwa huru kwa kulipa faini lakini mumewe aliyehukumiwa miaka saba alishindwa kulipa faini ya Sh. milioni 213.
MAOMBI YAO YASIKIKA
Wema na Kajala wamekuwa kwenye maombi ya kufunga wakisali na kufanya dua ili kuwaepusha na kifungo hivyo kwa sasa wote ni vicheko.

CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate