EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 13, 2013

MZEE SMALL: WALIONIUA NIKIWA HAI, WAMENIONYESHA MAPENZI - 1

Kutoka kushoto ni Mhariri wa Championi Jumatano, Phillip Nkini, Mzee Small, Mhariri Kiongozi wa Magazeti ya Championi, Saleh Ally na Mwandidhi wa Championi, Hans Mloli wakiwa wanaelekea nyumbani kwa Small.
Na Saleh Ally
KUZAGAA kwa taarifa za kufariki dunia kwa Mzee Small kuliwachanganya watu wengi sana, lakini bado ilionekana hakuna uhakika katika suala hilo.
                                                  Mzee Small na Saleh wakijuzana baadhi ya mambo.
Taarifa za kifo chake zilianza kuzagaa Jumanne, saa 4 usiku na ilielezwa amefariki muda mchache uliopita na msiba ulikuwa nyumbani kwake Tabata jijini Dar es Salaam.
Kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele, taarifa za kifo cha Mzee Small ziliendelea kuenea kwa kasi kubwa huku kwenye mitandao ya kijamii zikipata nafasi kubwa.

Achana na blogu mbalimbali kuanza kuandika kuhusiana na ‘kifo’ hicho, kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook, Instagram na Twitter, watu mbalimbali wakiwemo wasanii maarufu walikuwa wakiweka picha zake na kumuombea apumzike kwa amani (R.I.P).
                                           Mzee Small akiionyesha timu ya Championi jinsi bega lake lilivyopooza.
Gazeti hili mara moja lilianza kufuatilia kutaka kujua kuhusiana na ukweli, mafanikio ya kwanza yalikuwa ni kuzungumza na mwanaye aitwaye Yunus, ingawa alikuwa amelala, aliamka na kupokea simu ya Championi na kusema mzee wake ni mzima.

Lakini gazeti hili harikudhika, juhudi zikafanyika hadi kumpata mkewe, Mama Said ambaye alithibitisha kwamba mumewe, Said Ngamba au Mzee Small ni mzima na alikuwa amelala.
                                         Small (katikati) akisalimiana na Nkini (kushoto) na Saleh (kulia).
“Lakini unaweza usiamini, ngoja basi nimuamshe ili upate uhakika,” alisema na kusikika akimuita, “Mzee Small, Mzee Small, zungumza na huyu ndugu yako.”

“Mzee Small hapa, mimi ni mzima. Taarifa ulizosikia si sahihi,” alisema Mzee Small mara baada ya kuichukua simu.
                           Mke wa Mzee Small, Mama Said akiwa ameketi barazani nyumbani kwake Tabata.
Baadaye akasikika tena Mama Said akisema: “Nafikiri umemsikia baba, basi tumuache apumzike.”

Ushirikiano huo wa Mama Said ulitoa hofu ya taarifa hizo za kifo zilizokuwa zikienezwa huku haijulikani yupi aliyekuwa ameamua kufanya hivyo na kusambaza taarifa zisizokuwa na uhakika.

Juzi mchana, timu ya Championi ilifika nyumbani kwa Mzee Small eneo la Tabata kumtembelea, kubadilishana naye mawazo, kumpa pole na kutoa mchango kidogo kumsaidia matibabu (si lazima kusema kiasi gani).

Baada ya kufika Tabata, timu ya gazeti hili ikiongozwa na Mhariri Kiongozi, Mhariri wa Championi Jumatano, Phillip Nkini na waandishi wawili, Khatimu Naheka na Hans Mloli, ilipewa taarifa Mzee Small alikuwa amekwenda mazoezini.

Mipango ya kumfuata ilianza, lakini ghafla Mzee Small aliwasili akiwa katika pikipiki na kupokelewa na baadhi ya majirani zake ambao amekuwa akiwatania ni wachumba zake.

Mzee Small alisaidiwa kushuka kwenye pikipiki na baada ya hapo akaambiwa kuna wageni wake kutoka Championi. Aliwapokea na mazungumzo yakaanza kabla ya yeye kuomba akapunguze nywele zake.

“Mke wangu amekuwa akiniambia kwamba hizi nywele si nzuri, zimekaa vibaya. Si unaona, nafikiri tungekwenda nikapunguze kidogo halafu wote tutakwenda nyumbani,” alisema na wote wakakubali.

                                               Mzee Small akirejeshwa na pikipiki (bodaboda) akitokea mazoezini.
Kwa kinyozi hapakuwa mbali, Mzee Small aliingia pamoja na timu nzima ya Championi, wakati wakinyoa mazungumzo yalianza na akaanza kusimulia mkasa huo wa kuzushiwa kifo akiuita ni bomu.

“Hili bomu la leo la kuzushiwa kifo limeniweka katika wakati mgumu, watu wamekuwa wakipiga simu mfululizo wanataka kujua kama ni hai au la.

“Nimeshangazwa sana, nilitaka kujua huyo aliyezusha hayo yote ni nani, lakini naweza kusema nawashukuru hao waliozusha maana wamenionyesha kitu kimoja ambacho sikutegemea.

“Mapenzi ya watu kwangu, kweli watu wengi wamenipigia sana wakitaka kujua kama ni kweli au la, naendeleaje na kwa nini imekuwa hivyo. Hadi sasa simu zinaendelea kuingia, kumbe kuna Watanzania wanaonijali.

“Hakika maisha ni magumu, nateseka lakini angalau nina nafuu na kila siku, mara mbili, asubuhi na jioni natakiwa kufanya mazoezi,” anasema Mzee Small.
ENDELEA kusoma kuhusiana na Mzee Small, hali yake ya kuumwa, namna anavyoendesha maisha, anavyomzungumzia mkewe huku akitangaza vita na yoyote atakayemgusa.
USIKOSE CHAMPIONI JUMATATU.


HABARI NA GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate