EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 9, 2014

DIAMOND KUMNUNULIA WEMA JUMBA LA MIL 125


STAA wa Bongo Fleva mwenye mbwembwe kibao, pia anasifika kwa kuwa msafi na anasemekana ndiye mwenye mkwanja wa nguvu Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ anadaiwa yuko kwenye mchakato wa kumnunulia jumba la kifahari mpenzi wake wa ‘nenda rudi’, Wema Sepetu, Amani limeinyaka hii.
 
KUNA SABABU?
Kwa mujibu wa chanzo, Diamond ameamua kuingia kwenye kujikamua huko kufuatia taarifa kwamba, mmiliki wa nyumba anayoishi Wema kwa sasa (jina lipo), Kijitonyama, Dar es Salaam amemwamuru mlimbwende huyo kuhama kwenye mjengo wake mara baada ya kumaliza mkataba mwezi Juni, mwaka huu. Awali mjengo huo aliutangaza ni wake.
HEBU SIKIA
“Mwenye nyumba anayoishi Wema kwa sasa amekataa mrembo huyo kuendelea kuishi pale, akimaliza mkataba wake Juni, mwaka huu basi, hataki tena.
“Sasa Diamond aliposikia hilo akamwambia Wema isiwe tabu, akamuahidi kumnunulia nyumba ya kifahari yenye thamani ya shilingi milioni mia moja na ishirini na tano.
“Nadhani hiyo nyumba ipo tayari, ndiyo maana amemtajia na bei. Lakini ninavyojua mimi ipo Mwananyamala,” kilisema chanzo.
KUHUSU NYUMBA YA SASA
Kuhusu nyumba ya sasa, ni kweli ‘kifo cha nyani miti yote huteleza’ kwani Wema anatakiwa kutoendelea na mkataba mpya ikiwa ni siku chache tu baada ya Mahakama ya Ilala, Dar es Salaam kuamuru anyang’anywe lile gari lake la kifahari aina ya Audi Q7 lenye usajili wa T 973 BUJ na kukabidhiwa mmiliki wake halali, Shadrack Tweve.
Wema alipewa gari hilo na mwanaume anayedaiwa ni mpenzi wake anayejulikana kwa jina la Clement ambaye alilikopa kwa mmiliki huyo lakini alikuwa akikwepa kulipa deni la shilingi milioni 90.

Akizungumza na mwandishi wetu katika mahojiano maalum yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar, mmoja wa ‘kruu’ ya Wema ambaye hakutaka jina lake lionekane gazetini alisema kwa sasa Wema yuko katika kipindi kigumu baada ya kumwagana na kigogo huyo aliyekuwa akidaiwa kumpa jeuri na kufuatia kuamriwa kuhama kwenye nyumba hiyo.
Chanzo chetu kikazidi kumwaga data kuwa mbali na Wema kuachana na Clement, bado mrembo huyo amekuwa katika kipindi kibaya zaidi baada ya kunyang’anywa gari hilo ambalo ndilo alilokuwa akilitumia.
MKATABA WA NYUMBA ULIVYOKUWA
Mpashaji wetu aliendelea kujuza kuwa mmiliki wa nyumba anayoishi Wema ameamua kusitisha mkataba wa kumuongezea Wema muda wa kuendelea kuishi hapo baada ya kusikia madai ya msanii huyo akitamba kwenye magazeti kuwa mjengo huo ni mali yake na aliununua kwa shilingi milioni 400.
“Mkataba wa awali unaisha Juni, mwaka huu, hivyo hataweza kuendelea kuishi hapo lakini pia hana pesa za kuweza kulipa gharama ya nyumba kama ile, kwa sasa hana jeuri tena,” kilisema chanzo hicho.
Kikaongeza: “Unajua mara baada ya Wema kuingia kwenye nyumba ile na magazeti kuandika kwamba ameinunua, mmiliki wake alimfuata Clement kwa sababu ndiye aliyeingia naye mkataba.
“Akamuuliza inakuaje Wema anatangaza nyumba ni yake? Clement akampoza mwenye nyumba kwa kumwambia kwamba, asiwe na wasiwasi, Wema ni staa, mastaa wa Bongo wanapenda kujisifu, yeye adili na yeye aliyeingia naye mkataba.”
AANZA KUSAKA CHUMBA KIMOJA:
Habari zinadai kuwa mtazamo wa Wema (kama nyumba ya kununuliwa na Diamond itachelewa) ni kutafuta chumba kimoja na kupanga ili maisha yaendelee.
MAMA WEMA ASHAURIWA JAMBO:
Wadau hawakuishia hapo, walifika mbali zaidi kwa kumshauri mama mzazi wa staa huyo, Bi. Mariam Sepetu amchukue Wema na kuishi naye nyumbani kwake, Sinza-Mori, Dar ili kuficha aibu hiyo nzito na kubwa ya binti yake.
“Hata kama kuna tofauti baina yao, namshauri mama Wema amchukue mwanaye waishi pamoja, hii ni aibu ya familia kwa jumla,” alisema mdau mmoja kwa sharti la kutotajwa jina lake.
DIAMOND SASA:
Amani lilimsaka Diamond ili kuzungumza kuhusu madai ya kumnunulia Wema nyumba ambapo alisema:
“Mimi sipendi Wema apate tabu, naweza kumgharamia chochote kile ilimradi atulie tu.”
WEMA ATAFUTWA:
Mwandishi wetu alipomtafuta Wema kwa njia ya simu, iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa, hata mwandishi wetu alipomtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS), bado hakujibu.
CLEMENT NAYE:
Katika harakati zetu za kutetea ukweli, mwandishi wetu alimtafuta kigogo huyo kwa ajili ya kupata ukweli halisi ambapo baada ya mwandishi kujitambulisha, Clement alitoa udhuru wa kwenda kikaoni na kutaka apigiwe baada ya dakika tano.
Baada ya dakika 20, mwandishi alimpigia simu Clement lakini kila ilipoita kwa muda aliikata.
Imeandikwa na Imelda Mtema na Shakoor Jongo
CREDIT:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate