EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 11, 2014

KAZI KWENU WAJUMBE BUNGE LA KATIBA

KAMA ilivyo kawaida ya kila siku, ni budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutubariki tena leo, tukikutana tukiwa na uwezo wa kutambua kwamba, bila yeye aliye juu, tusingeweza kuwa pamoja.
Wema wa Mungu umetufanya tuendelee kushikamana kama taifa na tunaishi kama moja ya mifano bora kabisa ya amani katika ukanda huu wa Afrika Mashariki. Hii ni tunu ambayo yatupasa kuitunza na moja ya njia za kutufanya tuifanikishe, ni kuishi katika kumuamini Mungu na kujiweka tayari kwa kumtumikia.

Baada ya kusema hayo sasa tugeukie kwenye hoja yetu ya leo. Hatimaye Rais Jakaya Kikwete ametangaza majina ya wajumbe 201 ambao wataungana na wabunge wa sasa katika kikao cha Bunge maalum la Katiba, watakaokuwa na kazi moja tu ya kujadili katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyopendekezwa katika rasimu iliyokuwa chini ya Uenyekiti wa Jaji Joseph Sinde Warioba.

Haikuwa kazi rahisi kwa Rais kuifanya kazi hiyo, kwani kabla ya hapo, taasisi zipatazo 554 za Tanzania Bara ziliwasilisha majina ya wajumbe 2762 na 178 kutoka Zanzibar zilizokuwa na majina 874. Ni katika majina hayo, ndipo Rais Kikwete na mwenzake wa Zanzibar, Dk Mohamed Shein waliweza kuyajadili na hatimaye kufikia kuwatangaza waliotangazwa.

Ni hatua ya kupongezwa sana kwani kwa vyovyote vile, ilikuwa ni kazi ngumu iliyohitaji umakini mkubwa, hasa kwa jambo kubwa na muhimu linalokwenda kufanywa na wateule hao. Aidha, majukumu mengi na mazito ya kikazi ya viongozi hao wawili, yalichangia kuifanya kazi hiyo kuwa ngumu zaidi.

 Hii ni hatua moja muhimu sana katika mustakabali wa nchi yetu, wanachokwenda kukifanya wateule hao ni kuamua kuhusu uhai wa taifa letu.

Kuna jambo moja tu ambalo Watanzania wote tunaweza kulisema juu ya watu wote watakaoingia ndani ya Bunge hili, nalo ni kututendea haki sisi pamoja na taifa letu kwa ujumla.

Ninafahamu kwamba watu watakaokwenda huko, wako na masilahi kutokana na makundi wanayowakilisha, kama walemavu, wanasiasa, kutoka asasi zisizo za kiserikali na kadhalika.
 
Ninajua, kila mtu atataka kuwakilisha kundi lake, kwa vile kama tunavyojua, majina yao yalitumwa na taasisi zao wakiamini kabisa wakiteuliwa, watatanguliza masilahi ya asasi zao.

Lazima niseme kwamba pamoja na umuhimu wa kuwasilisha maoni ya taasisi wanazotoka, lakini jambo la msingi kabisa ni kila mmoja wao kuzingatia kwamba tunachotaka kukiona mwisho wa siku zao bungeni, ni katiba ambayo itakuwa imetoa upendeleo mkubwa mno kwa mtu mmoja anayeitwa Mtanzania.

Mtu huyu, wote tunajua kuwa siyo mwanasiasa, siyo mlemavu, siyo mkulima, mfanyabiashara wala mwingine.

Ni mtu anayesimama katikati ya vitu vyote hivi, lakini kwa bahati mbaya sana, hataweza kuingia ndani ya jumbe lile pale Dodoma kutokana na ukubwa wake. Anahitaji watu walioteuliwa wiki iliyopita, wazungumze kwa niaba yake.

Kama wateule hawa wataingia ndani ya jumbe lile na kuanza kuzungumza kuhusu masilahi ya asasi iliyompeleka huku akimtelekeza Mtanzania, hakika itakuwa ni usaliti mkubwa sana. Tunawasihi wampiganie, kwa sababu huyu akinyimwa haki yake, hakutakuwa na maana na bunge hilo litapoteza uhalali wake.

Tunataka kila mjumbe, aisikilize hoja, aipime, kwanza kwa kuangalia umuhimu wake kwa wananchi, halafu atoe maoni yake yenye kuboresha au kupinga. Hatutaki hoja kuungwa mkono kwa sababu tu, kundi lililowatuma linataka hivyo.
Ni lazima tutambue kwamba Watanzania ni muhimu zaidi kuliko wafuasi wote wa vyama, ni zaidi ya madhehebu yote ya kidini, ni zaidi ya asasi zote zisizo za kiserikali na kusema kweli, Tanzania ni zaidi ya kila kitu.

Kwa maana hiyo, mjadala huo usigeuzwe sehemu ya kushambuliana kwa misingi ya vyama au makundi, tunataka tuwaone wajumbe hawa wakiiweka mbele Tanzania na watu wake, kwa sababu hiyo ndiyo hasa sababu ya kuanzishwa na hatimaye kutekelezwa kwa mabadiliko ya katiba, ambayo tunataka ikidhi mahitaji yetu ya sasa kama taifa.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate