EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 12, 2014

BENKI YA CRDB YAZINDUA MFUMO WA KULIPIA MATIBABU KWA KUTUMIA NJIA YA KIELEKRONIKI 'KCMC TEMBO CARD'


Kadi mpya ya malipo ya matibabu katika Hospitali ya KCMC inavyoonekana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB akizungumza wakati wa uzinduzi wa KCMC Tembo Card itakayotumika kwa ajili ya malipo ya matibabu katika hospitali ya KCMC.

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dk. Martin Shao akizungumza wakati wa uzinduzi wa kadi ya malipo ya KCMC Tembo Card kwa ajili ya malipo ya matibabu katika hospitali ya KCMC badala ya fedha taslimu.


 Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB, wakiwa katika uzinduzi huo. Kushoto ni Mkurgenzi wa benki ya CRDB tawi la Arusha, Chiku Issa na wa pili  kulia ni Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDBTully Mwambapa. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mikopo Mikubwa, Philip Alfred.


 Baadhi ya wafanyakazi wa hospitali ya KCMC.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), akimkabidhi KCMC Tembo Card, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dk. Martin Shao, itakayowawezesha wagonjwa wanaofika katika Hospitali ya KCMC kulipia huduma za matibabu kwa njia ya kadi badala ya fedha taslimu. Uzinduzi huo ulifanyika mjini Moshi, mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Prof. Raimos Olomi.


 Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dk. Martin Shao akikata utepe wakati wa uzinduzi wa malipo ya matibabu kwa kutumia kadi ijulikanayo KCMC Tembo Card katika hospitali ya KCMC mjini Moshi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (katikati), akiwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dk. Martin Shao.


  Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini , Askofu Dk. Martin Shao akilipia huduma za matibabu katika Hospitali ya KCMC kwa kutumia kadi maalum ya KCMC Tembo Card badala ya fedha taslimu, wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika mjini Moshi.


  Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dk. Martin Shao akionesha  kadi ya malipo ya matibabu katika hospitali ya KCMC.



 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk Charles Kimei akifanya malipo ya matibabu kwa njia ya kadi badala ya fedha taslimu.



Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya KCMC, Prof. Raimos Olomi akilipia matibabu katika hospitali hiyo kwa kutumia kadi maalum ya KCMC Tembo Card.


 Dk. Kimei akipanda mti wa kumbukumbu.


 Zoezi la upandaji miti likiendelea.



 Baadhi ya watu wakishuhudia uzinduzi huo.


Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB.


Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya uzinduzi wa KCMC Tembo Card mjini Moshi.


 Dk.Charles Kimei akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jioni kwa ajili ya wateja wakubwa wa benki iliyofanyika katika ukumbi wa Kuringe mjini Moshi. 


Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, IGP Said Mwema akipata chakula wakati wa hafla hiyo.


 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya KCMC, Prof. Raimos Olomi (kulia) na Mkurugezni wa CRDB, Dk. Charles Kimei wakipata chakula.


Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu (IGP), Said Mwema (wa nne kushoto), akicheza ngoma za asili za kabila la wachaga wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Benki ya CRDB kwa ajili ya wateja wa benki hiyo.

Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDBTully Mwambapa (kulia), akiwa na Mkurugenzi wa tawi la CRDB Arusha, Chiku Issa wakati wa hafla hiyo. 



MOSHI, Tanzania



 BENKI ya CRBD imezindua mpango mpya wa huduma za kulipa kabla kwa kutumia kadi za benki hiyo katika hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo mjini Moshi. kwa lengo la kurahisisha malipo yanayotolewa kwa wagonjwa na kuongeza mapato ya hospitali. Kutokana na uzinduzi huo wa kadi hiyo mpya sasa huduma zitaweza kupatika kwa urahisi kwa wagonjwa ambao ni wateja wa benki hiyo watakapokuwa wanapata huduma katika hospitali hiyo. 



Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo  Dk Charles Kimei alisema Benki kuongeza na kuboresha huduma zake nchini kwa kasi ili iweze kuwafikishia wananchi wa kila aina huduma hizo ili kurahisisha maisha yao. TemboCard KCMC Card’ sasa itakuwa niKadi ambayo itakuwa ni suluhisho la ukusanyaji fedha za malipo ya huduma katika hospitali hii ya rufaa ya KCMC.



Aliongeza kuwa uzinduzi huu wa TemboCArdKCMC utasaidia kurahisisha malipo na kuiwezesha hospitali hiyo kusimamia vema huduma zake kwa masualla yanayohusu kipesa kwani kupokea pesa au kufanya shughuli za malipo katika eneo lenye mchanganyiko wa shughuli kama katika Hospitali hii lina changamoto nyingi zikiwemo zile za kupata noti bandia pamojan a gharama kubwa za kusimamia.



Kwa mujibu wa Dk Kimei, matumizi ya TemboCard kadi za kulipia kabla kwa kiasi kikubwa kupunguza idadi ya shughuli za fedha katika hospitali , kwa kuzingatia kwamba zaidi ya asilimia 50 ya shughuli za kila siku katika hospitali ni kimsingi ni za kifedha  hivyo kwa kutumia Tembocard KCMC kadi, wagonjwa watafanya shughuli za  malipo katika   vituo vilivyoko ndani ya hospitali na  kupata risiti haraka na rahisi ," Dk Kimei alisema.


Mkurugenzi Mtendaji huyo pia alisisitiza kuwa Benki ya CRDB ina lengo kuimarisha usalama wa fedha kwa wateja na ina mifumo jumuishi kupatanisha shughuli yoyote katika muda halisi. Vile vile, benki imetumia teknolojia rahisi katika benki kadi hivyo kufanya Benki ya CRDB Tembo Cards salama zaidi .
 

Kimei alimwambia mgeni rasmi Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Dayosisi ya Kaskazini  Dr. William Shao Askofu kuwa benki hiyo sasa imepata mafanikio na ubora wa kimataifa wa kadi za ‘TemboCard” hivyo kupelekea mashirika makubwa na ya kimataifa ya biashara ya kadi za malipo  duniani yaani  Visa International, MasterCard na China Union Pay kujenga imani na kuvutiwa kujiunga CRDB.



Aliweka bayana kuwa Muungano huo ndio uliopelekea kuzalishwa kwa kadi za TemboCardVisa, TemboCardMasterCard na sasa TemboCard-China Union Pay.  CRDB hadi sasa ni benki pekee katika Afrika nzima kuweza kuunganisha jina la kadi yetu yaani ‘’Co-branding” na kadi hizi za malipo za kimataifa. Hiki ni kithibitisho tosha cha ubora wa kimataifa wa kadi zetu.



Dk Kimei alimhakikishiaAskofu Shao kuwa Kwa wale ambao hawana akaunti za mabenki wala kadi za kimataifa, wao watahitajika kuchukua kadi hizi za TemboCard-KCMC ambazo zitapatikana Kwenye tawi   lililopo hospitalini  KCMC au kwenye tawi lolote la Benki ya CRDB Moshi mjini, Marangu na Boma au vile vile kupitia kwa mawakala wetu wa FahariHuduma waliopo kila kona.



Dk Kimei alieleza upatikanaji wa kadi hizo kwa watu wanaopata huduma KCMC kuwa zitatolewa bure kabisa  ila wateja  watakapozichukua, watalazimika kuziwekea pesa tayari kwa malipo. Kadi hizi zinaweza kujazwa pesa  kwa kupitia njia mbalimbali kama Kuingiza pesa kwenye kadi hiyo kupitia matawi yetu, Kuhamisha moja kwa moja kutoka kwenye akaunti zao kwa kutumia SimBanking au Kwa kutumia njia za mitandao ya simu yaani M-pesa, TigoPesa na Airtell money.



Kimei alizisifu kadi hizo kuwa za TemboCard KCMC kuwa zina ulinzi  wa hali juu hivyo mteja awapo na kadi hiyo asiwe wasiwasi kabisa na usalama wa  fedha zake. Kwani hata ikitokea kwa bahati mbaya mteja akaipoteza kadi yake, hakuna mtu mwingine anayeweza kuitumia kwakuwa inatumia teknolojia ya CHIP na PIN ambayo hairuhusu mtu asiyemuhusika kuweza kuitumia.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate