EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 19, 2014

CCM WAKANUSHA WARAKA WA SIRI WA UCHAGUZI WA KALENGA

 Katibu mkuu wa CCM Mkoa wa Iringa,Ndugu Hassani Mtenga akizungumza na wanahabari wa Iringa katika ofisi za chama hicho mapema leo.
  Katibu mkuu wa CCM Mkoa wa Iringa,Ndugu Hassani Mtenga akizungumza na wanahabari wa Iringa katika ofisi za chama hicho mapema leo.
Sahihi halali ya Mwigulu Nchemba ambayo iko tofauti ya waraka uliosambazwa.
=======  ======  ========
Na Denis Mlowe,Iringa


KATIBU wa CCM Mkoa wa Iringa Hassani Mtenga amekanusha chama hicho kuhusishwa na waraka aliodai umesambazwa na Chadema ukihusu mchanganuo wa matumizi ya Sh Milioni 560 katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga.
Alisema propaganda za kisiasa za wapinzani ndio chanzo cha waraka huo kusambaa na kuwaonyesha waandishi wa habari sahihi kamili ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM  Mwigulu Nchemba anayesemekana alisaini waraka huo.

"Kwanza kuna kosa hawa wenzetu wanafanya, waraka huo una anwani ya Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa lakini chini unaonekana umesainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Mwigulu Nchemba, sahihi ambayo imegushiwa,” alisema Mtenga


Katika waraka huo wenye kichwa cha habari kinachosema ‘Malipo ya kamati mbalimbali kwenye ushindi wa jimbo la Kalenga, umeidhinisha fedha hizo zitolewe kwa viongozi mbalimbali kama walivyoomba oili zitumike katika kampeni za jimbo.


Waraka huo unaonyesha kuwa CCM wametumia kiasi cha shilingi milioni 560 kwa ajili ya timu ya ushindi wiki hii ya mwisho ya kampeni, fedha hizo zimetumwa kutokana na tathimini yenu kuwa ni hali mbaya kwetu kwa barua yenu yenye  kumb Namba  CCM/IR/VOL11/096.

“Hakikisha kiwango hiki kinwafikia  walengwa wote wafuatao kwa uwiao tuliokubaliana kulingana na maeneo yao na wao wazigawe kwa mabalozi wetu kwenye kila kitongoji na kata apewe Balozi Sh850,000, Mama Galinoma Sh Milioni 80, Mama Ray (Ulanda) Sh Milioni 60, wenyeviti wa kata wa CCM kila mmoja Sh Milioni 20, makatibu wa kata kila mmoja Sh Milioni 8, makatibu wenezi CCM kila mmoja Sh Milioni 14 na Kamati ya ushindi Nzihi Sh Milioni 108,” sehemu ya waraka huo inasema.

Mtenga alisema lengo la kusambazwa kwa waraka huo lilikuwa kuwaaminisha wapiga kura wa Kalenga kwamba kuna fedha zimetolewa na CCM kwa ajili yao lakini zimeliwa na watu wanaotajwa katika waraka huo.


Alisema kuna kila dalili kwamba waraka huo uliandaliwa na Chadema kwa lengo la kuwarubuni wananchi wa jimbo la Kalenga wakose imani na CCM.

Wakati huo huo CCM kimempa siku 7 Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Iringa, OCD Sifael Pyuza kuwataka radhi kwa madai ya kuwadhalilisha katika ofisi za chama hicho mkoani hapa baada ya kuwafanyia uchunguzi bila kuwa na kibali maalum.

Kamanda Pyuza anatuhumiwa na chama hicho kukihusisha na mchezo mchafu wa siasa kwa kuficha watu ndani ya jengo la ofisi yake waliokuja katika uchaguzi mdogo wa Kalenga uliofanyika machi 16 na ccm kuibuka kidedea.

Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga aliyasema  hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuwa , Machi 16 mwaka huu kamanda huyo alituma makechero wa jeshi hilo katika ofisi za CCM za mkoa wa Iringa waliotumia mabavu kupekua ofisi moja baada ya nyingine bila kuwa na kibali halali.

Alimtaka kamanda huyo kuwaomba radhi baada ya tuhuma yake dhidi yao kubainika haina ukweli.

na chama cha mapinduzi hakiwezi kukaa kimya kwa udhalilishaji huu uliofanywa na mkuu wa upelelezi wa wilaya kwa sababu jambo hilo ni sawa na kukiingiza chama cha mapinduzi katika kashfa ya mchezo mchafu wa kisiasa.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi alisema hana taarifa yoyote kuhusiana na madai ya chama hicho lakini yupo tayari kuyapokea na kuyafanyia kazi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate