EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 11, 2014

KURA ZA SIRI,WAZI KIPORO

BADO MUAFAKA! Ndivyo ilivyojidhihirisha jana kwenye Bunge Maalum la Katiba, ambalo limeshindwa kufikia makubaliano ya kura gani, itumike wakati wa kupitisha uamuzi wa ibara za rasimu ya Katiba mpya.
Kura inayobishaniwa na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, ni kama iwe ya siri au wazi, jambo lililogawa Bunge hilo katika makundi mawili, yanayotofautiana kuhusu namna gani uamuzi ufanyike ndani ya Bunge hilo.
Kutokana na jambo hilo kushindwa kupata muafaka, kuhusu aina ya upigaji kura kwenye kufanya uamuzi, sasa Bunge hilo limeamua kupitisha rasimu ya Kanuni huku kifungu hicho cha kufanya uamuzi, kikieleza tu kuwa uamuzi utafanywa kwa kupiga kura.

Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalumu, Pandu Ameir Kificho, alitangaza hatua hiyo jana, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni, Profesa Costa Mahalu, kuliambia Bunge hilo kuwa kifungu hicho, sasa kitasomeka tu kwamba uamuzi wake, utafanywa kwa kupiga kura.

Kificho ambaye aliingia ukumbini saa 6.15 mchana badala ya saa tano aliyoahidi siku ya Jumamosi, aliomba radhi kuchelewa kwa vile alikuwa anaendelea kushauriana na Kamati ya Kumshauri kuhusu kanuni, ambayo ilikuwa inaendelea kufanya marekebisho ya kanuni hasa kwa Kanuni ya 37 na 38.
Profesa Mahalu aliliambia Bunge hilo, kuwa wamekamilisha kazi katika kanuni hizo za 37 na 38, ambazo zinaeleza namna ya kufanya uamuzi utakuwa ni kupiga siri ambayo itaamriwa na Bunge hilo. Kamati hiyo ambayo awali ilipendekeza kura iwe ya siri, sasa imesema tu kuwa mambo yote yataamriwa kwa kura.

Kwa hatua hiyo ya Kamati ya Kanuni, ni wazi kuwa uamuzi wa namna gani litafikia maamuzi umewekwa kiporo. Kificho katika maamuzi yake, alisema kuwa Bunge lingepitisha kanuni, ambazo zimesharidhiwa kwenye semina hiyo na hizo mbili bado zitatafutiwa ufumbuzi na Kamati ya Maridhiano.
Tangazo hilo la Kificho lilizua mjadala mkubwa, hali iliyoonesha baadhi ya wajumbe kutokubaliana na hatua hiyo, ambao baadhi yao walitaka Bunge hilo lipige kura ya kumaliza suala hilo na sio kuendelea kuliweka kiporo, kama alivyotaka Mwenyekiti wa Muda.
Wengine wakapendekeza Bunge livunjwe.
 
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila alisema kwa kuwa wabunge wanaendelea kutafuna posho, ambayo ni kodi ya wananchi, lakini wameshindwa kupata muafaka wa jambo hilo, ni vyema Bunge hilo livunjwe na waletwe watu wengine, wenye dhamira safi ya kufanya kazi hiyo.
“Tangu tuanze hapa tunavutana juu ya jambo hili na kanuni hapa zimekwama na hakuna uamuzi mbadala, kama jioni tukija hapa jambo hili bado halijapata muafaka, ni vyema Bunge hili livunjwe maana hatuwezi kuendelea kupata posho wakati kazi hazifanyiki,” alisema Kafulila.

Kificho alimjibu mbunge huyo kuwa Bunge hilo, limeanza kwa tangazo la Rais ;na Rais ndiye mwenye mamlaka ya kulivunja ;na sio vinginevyo. Hezekiah Oluoch alisema kwa kuwa Kamati ya Maridhiano, imekutana kwa siku tatu na imeshindwa kupata ufumbuzi ni bora suala hilo lipigiwe kura.
“Naomba Sekretarieti itugawie karatasi tuamue jambo hili, wewe tulikuchagua kwa siri na suala hili tutalipiga kwa siri,” alisema.
Hoja ya Oluoch ilikuwa kuwa Bunge haliwezi kuendelea na kazi yake ya kuridhia kanuni nusu, wakati vifungu vingine havijafikia na kumtaka Mwenyekiti atendee haki Bunge hilo ili vifungu hivyo viwili, vipitishwe na wabunge wenyewe.

Diana Chilolo ambaye ni Mbunge wa CCM Viti Maalumu, alisema kama ni kura inapigwa kuhusu vifungu hivyo, ipigwe kura ya wazi. “Kwa nini tunapata kigugumizi juu ya jambo hili? Kama Kamati ya Mashauriano imekwama kupata muafaka tupige kura na wananchi wanataka kura iwe ya wazi.”
Mbunge huyo ambaye wakati anatoa hoja hiyo, alikuwa akizomewa alisema; “ Kuzomea sio jambo la busara na ni tabia mbaya na Mungu hataki, hivyo mimi nashauri tupige kura ya wazi kuhusu vifungu hivyo”.
William Lukuvi ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema kwa kuwa vimebaki vifungu viwili ni vyema Bunge hilo, liendelee na ratiba yake na hizo kanuni kiporo zitapitishwa baadaye baada ya Kuunda Kamati ya Kanuni za Bunge.

Hoja hiyo ya Lukuvi, pia ilisababisha azomewe, lakini akawa ngangari na kuendelea kusema “Nyie zomeeni… lakini mimi ni sugu wa kuzomewa, hapa ninachokisema ni kwamba kama mnataka semina hii tumalize kila jambo basi hakuna hata haja ya kuunda Kamati ya Kanuni ya Kudumu.
“Tusijidanganye kuwa hizi kanuni zitakuwa kamili kwa uhai wote wa Bunge hili, kuna mambo yanaweza kuletwa hapa kwa ajili ya marekebisho na ndio maana kunaundwa Kamati ya Kanuni; hivyo suala hili baadaye litaletwa na kamati hii ni vyema kwa sasa tuendelee na mambo mengine,” alisema Lukuvi.
Lukuvi alisema sio jambo jema kupiga kura kuamua jambo hilo kwani litagawa Bunge hilo.

“Hata tukipiga kura hapa kuna kundi litashinda na lingine litashindwa, iweje tuwe na Bunge ambalo limegawanyika kwenye mambo ya Katiba? Mjumbe wa Kamati ya Kanuni, George Simbachawene, alimkosoa Lukuvi na Kificho kuwa vifungu hivyo, haviwekwi pembeni, bali kanuni zitakazopitishwa zitahusisha vifungu hivyo viwili, kwani vinatamka kuwa uamuzi utafanyika kwa kura, ila haielezi aina ya kura itakayopigwa.

“Vifungu hivi havitaji siri au wazi, ila vinasema tutaamua kwa kura, tumefikia hapo maana wananchi wanalalamika tunakula posho bila kazi, ni vyema tuanze kazi kwa kuapisha watu na kuchagua Mwenyekiti na twende kwenye kamati.
“Tutakapofikia wakati wa kutoa uamuzi kila mtu atakuwa ameshajiuliza na Kamati ya Kanuni italeta jambo hilo na sisi kama Bunge tutaamua ni aina gani ya kura ipigwe na wakati huo, Kamati ya Maridhiano naamini itakuwa imefikia hatua nzuri,” alisema Simbachawene.
Baada ya maoni hayo ya Simbachawene, wajumbe wengi walisimama kutaka kutoa maoni, lakini Kificho alisema kuwa kilichofikiwa kwenye Kamati ya Kanuni, ndicho mbacho kimeamriwa kwenye Kamati ya Mashauriano hivyo ni vyema jioni wapitishe kanuni hizo.

Maoni ya Wabunge Wakizungumza nje ya ukumbi wa Bunge, Joseph Selasini, alisema makundi ya kisiasa, yamelivuruga Bunge na yamevuruga maridhiano ndani ya Kamati ya Mashauriano. Alishauri kwamba kuna haja ya kuongeza watu kwenye kamati hiyo ili kufikia muafaka wa jambo hilo.
“Kamati ya Maridhiano ikaonane na Rais Jakaya Kikwete ili kupata ushauri na hatimaye kufikia uamuzi kuhusu vifungu hivyo. Haiwezekani kupitishwa rasimu ya kanuni wakati vifungu vya 37 na 38 havijafanyiwa uamuzi, lazima uamuzi ufanyike leo na kama tunakwepa leo tutaweza lini?” Alihoji Selasini.
Murtaza Mangunga alitaka Kamati ya Mashauriano, iendelee kufanyia kazi vifungu hivyo na wajumbe wa Bunge la Katiba waendelee na shughuli nyingine kujadili na kupitisha rasimu ya Katiba.
 
Dk Henry Shekifu alisema busara imetumika kwa vile imeshindikana kupata ufumbuzi, ni vyema Bunge liendelee na mambo mengine na baadaye watatafuta namna nzuri ya kufanya uamuzi wa kupiga kura.
“Kwa nini tugome kuendelea na kazi zingine hadi suala hilo lipata ufumbuzi? Hivi wananchi watatuelewaje hii inaonesha watu wana nia mbaya na jambo hili,” alisema Dk Shikifu.
Profesa Ibrahim Lipumba alisema alichofanya Mwenyekiti wa Muda wa Bunge, ni kulaza matatizo kwani Bunge haliwezi kuendelea kujadili Katiba wakati kanuni zenyewe hazijakamilika na inaweza kuleta matatizo huko mbele ya safari.
Lipumba alisema kwenye Kamati ya Mashauriano, walikubaliana kuwa kuwepo na kura ya siri na ya wazi, kwa mambo ya kawaida iwe wazi; lakini kwenye mambo nyeti kama ya dini na Muungano, ambayo yanahatarisha maisha ya wajumbe ipigwe kura ya siri.
“Tulikubaliana hivyo, wenzetu wajumbe wa CCM walivyoenda huko wakatugeuka, tuliwataka pia wakashauriane na Mwenyekiti wao, lakini leo hatukukutana badala yake tumekuja bungeni na hili ndilo ambalo limetokea,” alisema.

Profesa Lipumba alisema huwezi kuendelea mbele na mijadala ya Katiba wakati utaratibu wa kufanya uamuzi haujulikani, kwani wajumbe watafanya mijadala na ikifika wakati wa kupiga kura itashindikana kwani kanuni imekaa kimya juu ya suala hilo.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Mashauriano, alipinga agizo la Kificho la kupitisha kanuni hizo bila kuwepo maridhiano.
Alisisitiza kuwa hakuna afya kwa Bunge hilo kuamua mambo yake kwa kupiga kura ya siri au ya wazi. Alisema mchakato wa Katiba ni wa maridhiano na sio wa kupiga kura kwa kupata shinikizo kutoka kwenye makundi ya vyama vya siasa. “

“Hapa ikipigwa kura CCM ikashinda wengine watagoma na upande mwingine ukishinda CCM nao watagoma, hivyo hatapatikana mshindi na utakuwa mwisho wa mchakato wa Katiba,” alisema. Alisema baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo, wanapata shinikizo na maelekezo ya vyama vyao nje ya maelekezo ya kifungu cha nne cha kanuni hizo, ambacho kinapiga marufuku wajumbe wa Bunge hilo kupata shinikizo lolote nje ya dhamira yake. Alisisitiza kuwa kura ya siri au ya ndio, italivunja Bunge na amependekeza maridhiano zaidi yatumike.
Alitoa mfano kuwa kura ya wazi kwa mambo ya dini au Muungano, yanawaweka baadhi ya wajumbe katika hatari kubwa ya maisha yao. “Kuna suala la Muungano hapa, Mzanzibari akipiga kura ya wazi misimamo ya huko mnaifahamu anaweza kumwagiwa tindikali na hata nyumba yake kuchomwa, lakini pia kuna misimamo ya dini ni hatari kwa muumini mwenyewe,” alisema Mbowe.
Mchungaji Christopher Mtikila, kwa upande wake, alisema kwamba alichofanya Mwenyekiti wa Muda ni kuahirisha tatizo. Alisema kuwa ushabiki ambao umeoneshwa kwenye mambo ya msingi, unaweza kuvuruga upatikanaji wa Katiba mpya.

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Felix Mkosamali, ambaye ni Mbunge wa Muhambwe alikosa uvumilivu baada ya kuitwa mtoto na kusababisha majibizano ya ‘matusi’ miongoni mwa wajumbe.
Majira ya saa 10 jioni baada ya Mwenyekiti wa Muda, Pandu Ameir Kificho kufungua Bunge, Mkosamali alisimama kuomba muongozo, lakini aliambiwa asubiri na atapewa nafasi wajumbe wa Bunge hilo wakifika nusu yake.

Hata hivyo, baada ya dakika kadhaa, James Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, chama anachotoka Mkosamali, alisimama na kuomba muongozo.
Alipokubaliwa alisema kutokana na kutopata nakala ya Rasimu ya Kanuni, hawataweza kujadili rasimu hiyo na Kificho, akamuambia ndiyo maana amesimamisha Bunge kwa muda ili nakala wapewe wajumbe.
Kutokana na hatua hiyo, Mkosamali alisimama na kusema; “Mwenyekiti samahani nakuheshimu sana lakini mimi umeninyima nafasi ya kuzungumza lakini mjumbe (Mbatia), umempa nafasi hivi sivyo njia sahihi ya kuendesha Bunge.”

Baada ya kumaliza, ikasikika sauti ya mbunge mwanamke, ikamjibu “mtoto mdogo hana adabu” na alipomaliza ikatokea sauti nyingine ya Mbunge mwanamume, akajibu “Kubwa jinga halina adabu.”
Naye Mkosamali akajibu; “hakuna mtoto mdogo aliyeishinda CCM.” Kutokana na malumbano hayo, yaliyodumu kwa dakika tano, Kificho akasema; “hakuna mtoto hapa watu wote ni wajumbe”.
Alipomaliza kutoa kauli hiyo, Kificho akaahirisha Bunge saa 10:27 jioni hadi saa 12:00 jioni, kutokana na kazi ya kudurufu kanuni kutomalizika na kupewa wajumbe ili waendelee kuziridhia.
CHANZO NI HABARI LEO

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate