EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 8, 2014

MAMA AJIFANYA NESI, AAJIRIWA HOSPITALINI KWA MUDA MREFU, ADAKWA!



Hatari sana! Mwanamke aliyetambulika kwa jina la Joyce Jonas, mwenye umri unaokadiriwa kuwa kati ya miaka 45 na 50, mkazi wa Tabata, Dar, ametiwa mbaroni kwa madai ya kughushi vyeti vya unesi kisha kufanya kazi ya uuguzi katika hospitali mbalimbali, akijishughulisha na upasuaji bila kuwa na utaalamu wa taaluma hiyo.
Mwanamke aliyetambulika kwa jina la Joyce Jonas ametiwa mbaroni kwa madai ya kughushi vyeti vya unesi.
Tukio hilo lililovuta hisia za wengi, lilijiri hivi karibuni maeneo ya Mwenge, Dar ambapo mtuhumiwa huyo alidakwa katika moja ya hospitali (jina tunalo) na mwenye vyeti ambaye kitaaluma ni nesi kisha kufikishwa kituo kidogo cha Polisi cha Mwenge, Dar.
ILIKUWAJE?
Habari zilidai kuwa Joyce ni binamu wa mmiliki halali wa vyeti vya unesi aliyetajwa kwa jina la Mary Bora.
Ilisemekana kwamba miezi kadhaa iliyopita, Joyce alifika nyumbani kwa nesi huyo na kufanikiwa kuiba vyeti hivyo.

Kitambulisho feki chanye jina la Mary Peter Bura.
Habari zinadai kwamba lengo la mtuhumiwa kuiba vyeti hivyo ni kuvitumia kwa ajili ya kazi aliyokuwa nayo awali ya kuuza duka la dawa baridi za binadamu lililokuwa Mnazi-Mmoja, Dar.
Ilidaiwa kwamba Joyce alipata ushawishi kutoka kwa baadhi ya watu wake wa karibu wakimtaka kutumia vyeti hivyo, kutafuta kazi ya unesi kwani viliruhusu kutokana na kuwa na viwango vya juu.
Ilisemekana kwamba Joyce alidurufu vyeti hivyo kwa kutumia jina halisi la nesi huyo huku akibandika picha yake na kuvirudisha vyeti halisi nyumbani kwa Mary bila mwenyewe kujua.
Nesi feki akipelekwa kituo kidogo cha Polisi cha Mwenge, Dar.
Ilisemekana kuwa Joyce alifanikiwa kupata kazi kwenye hospitali mbili, moja Kariakoo na nyingine Mwenge (majina tunayo) na kuanza kujiingizia ‘mpunga’ wa maana huku akijuhusisha na upasuaji, zoezi ambalo alikuwa akilifanya kwa kutumia uzoefu tu, kutokana na kujua kushona majeraha madogo.

Habari zilidai kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kutumia vyeti hivyo kwa muda mrefu, hatimaye taarifa zilimfikia nesi halisi kuwa jina lake linatumiwa na nesi mmoja kwenye hospitali tofauti.
Ilisemekana kuwa baada ya taarifa hizo kumfikia Mary (mwenye vyeti halisi), alifanya uchunguzi kujua ni nesi gani anatumia jina lake katika hospitali hizo, ilihali yeye si mwajiriwa wa hospitali tajwa.

Ilielezwa kuwa Mary aliunda mkakati kabambe wa kumtia Joyce mbaroni ambapo alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha Mwenge kisha akapewa askari alioambatana nao.
Mary, akiambatana na vijana wa IGP Mangu walifanikiwa kumtia nguvuni Joyce akiwa kazini ndani ya hospitali moja maarufu iliyopo Mwenge.

Baada ya kumkamata, Joyce hakuwa na la kujitetea zaidi ya kukiri kuwa ni kweli alifanya ‘uhuni’ huo huku akijitetea kuwa ni ugumu wa maisha ndiyo ulisababisha.
Wakiwa kwenye ujenzi wa taifa, makachero wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) walipokea taarifa za kuwepo kwa kesi hiyo kituoni hapo ambapo walitinga hapo na kumkuta Joyce akiwa chini ya ulinzi.

Kutokana na uzito wake, madai ya kesi hiyo yalihamishiwa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar.
Wakiwa njiani kuelekea kituoni hapo, Joyce aliwaomba makachero wetu wasifanye chochote, ikiwemo kuandika habari hiyo.
“Jamani,nawaombeni msinipige picha, wala msiandike habari hii, haya ni maisha tu,” alilalamika Joyce.
Baada ya kufikishwa kituoni hapo, Joyce alifunguliwa jalada la mashitaka lenye namba KJN/RB/1883/2014-KUGUSHI na kutupwa rumande kupisha uchunguzi zaidi juu ya madai hayo kisha atafikishwa kortini.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate