EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 26, 2014

ACHOMWA KISU KISA MUME WA MTU!

JESHIla polisi mkoani hapa linamshikilia mwanamke aliyejulikana kwa jina la Pima Mabubu kwa tuhuma za kumchoma kisu mpaka kumjeruhi vibaya mwanamke mwenzake, Amina Hussein akidai ana uhusiano wa kimapenzi na mumewe, Adam Ndekeja, Risasi Jumamosi lina mkasa wote.
Amina Hussein akipata matibabu katika hospital ya taifa Muhimbili.
Tukio hilo lililowaacha watu vinywa wazi, lilijiri Aprili 22, mwaka huu shambani katika Kijiji cha Kigwa, Kata ya Ukondamoyo wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora.
KISU KILIVYOFANYA KAZI
Habari kutoka kwa baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa, Amina alichomwa kisu mara mbili, kwenye paja mguu wa kushoto kisha kwenye mgongo ambapo kilizama na kutoka mpini tu!
Amina Hussein akikimbizwa hospital baada ya kupatwa na mkasa huo.
KISA KINASIMULIWA
Kwa mujibu wa taarifa za awali, siku ya tukio, Pima alitoka nyumbani kwake na kumfuatilia mumewe huyo kwenye shamba la tumbaku la kaka wa Amina (jina halikupatikana) ambako alisikia kuwa mwanamke huyo yupo na mumewe.
“Pima alisikia Amina ana uhusiano na mumewe. Siku hiyo akasikia wapo shambani. Akatoka nyumbani na kufuatilia akijua atawanasa laivu,” kilisema chanzo hicho.
Kisu kinachosadikika kilitumika kumjeruhi Amina Hussein.
MWANAMKE ALIYECHOMWA KISU
Akizungumza akiwa amelazwa akiuguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete, Amina alisema:
“Mimi sina uhusiano na huyo mwanaume jamani. Kwanza huyo mwanamke simjui kabisa. Nimemwona kwa mara ya kwanza siku hiyo ya tukio.
“Siku hiyo mimi na mwanangu kichanga (wa miezi mitatu) tulikuwa shambani, mimi nilikuwa nikimsaidia kaka yangu kuvuna tumbaku, akaja Adam (mwenye mke) naye akawa anasaidia kuvuna. Kuna wakati nilikwenda kupumzika mahali ili nimnyonyeshe mwanangu.
“Ghafla aliibuka huyo mwanamke. Nilimwona akinifuata mimi moja kwa moja. Aliponifikia alinirukia na kuanza kunichoma kisu mgongoni na kwenye paja la kushoto.
“Ilikuwa ni hatua chache tu tokea mahali ambako mume wake alikuwa akivuna. Nilipiga kelele za kuomba msaada, mume wake akaja mbio kusaidia kwa kumdhibiti mke wake asiendelee kunichoma kisu zaidi,” alisema Amina.
Akaendelea: “Nilianguka chini na kuanza kugalagala huku damu nyingi zikinitoka. Ndipo wasamaria wema nao walifika na kumkamata Pima, wakamfunga kamba na kumpeleka ofisi ya kata ambako alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi Tabora.”
BODABODA YAMKIMBIZA HOSPITALI
Habari zaidi zinasema kuwa, Amina akiwa hoi na damu chapachapa, alipandishwa kwenye bodaboda na kukimbizwa kweynye hospitali ya rufaa ya mkoa kwa ajili ya matibabu huku hali yake ikionekana si ya kuridhisha.

KILA MTU NA WAKE
Taarifa zaidi zinasema kuwa, wakati ndugu wa Amina wakihaha kumshughulikia majeruhi huyo kupata matibabu kwa lengo la kuokoa uhai wake, baadhi ya ndugu wa Pima walipiga kambi nje ya kituo cha polisi wakipigania kumdhamini ndugu yao huyo.
“Ukitaka kujua msemo kwamba kila mchuma janga hula na wa kwao fuatilia mkasa huu. Wakati ndugu wa Amina wakihaha kuokoa maisha yake hospitalini, ndugu wa Pima nao walikuwa wakihangaika kuhakikisha mtuhumiwa huyo anapata dhamana ili arejee uraiani. Hakuna aliyekwenda kumjulia hali Amina,” kilisema chanzo.
KUHUSU MUME WA MTUHUMIWA
Katika hali isiyotarajiwa, mume wa mtuhumiwa huyo alikimbia kusikojulikana muda mfupi baada ya mkasa huo kutokea jambo ambalo limezua maswali yasiyo na majibu.
Wengi wamekuwa wakiuliza ni nini kimemkimbiza mwanaume huyo kama kweli yeye hana uhusiano wowote na mwanamke huyo?!
“Au kuna ukweli unafichwa? Kama hakuna ni kwa nini Adam alikimbia? Hapa kuna haja ya jeshi la polisi kumsaka mwanaume huyo mpaka kumkamata ili ukweli ujulikane,” alisema mkazi mmoja wa eneo hilo.
CREDIT:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate