EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 26, 2014

UOZO MAHOSPITALINI: OFM YAIFUNGIA KAZI PALESTINA!

BADO hali ya huduma zinazotolewa na baadhi ya hospitali zetu nchini ni mbaya, utendaji mbovu na wagonjwa hawajaliwi hata pale inapotokea wamepelekwa wakiwa mahututi, Risasi Jumamosi linakufunulia.
Eneo la hospitali ya palestina.
Baada ya kuanika uozo wa hospitali kadhaa – za serikali na binafsi, sasa kikosi kazi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ cha Global Publishers, kilitinga katika Hospitali ya Wilaya ya Kinondoni, Palestina na kugundua udhaifu mkubwa wa huduma mbovu zitolewazo hospitalini hapo.
OFM wakiingia hospitalini hapo.

YALITANGULIA MALALAMIKO
Wananchi mbalimbali kwa nyakati tofauti walipiga simu kwa OFMna kueleza namna hospitali hiyo inavyotoa huduma mbaya hasa Mapokezi, wauguzi na madaktari wa kitengo chote cha wagonjwa wa nje, ‘Outpatient Department’ (OPD).
OFM wakiwa chumba cha daktari bila ya uwepo wa daktari.
OFM KAZINI
Aprili 23, mwaka huu saa 10:42 za alasiri, OFMwaliingia hospitalini hapo wakiwa tayari kwa kazi, ambapo mmoja wao alijifanya mgonjwa mahututi aliyehitaji huduma ya haraka.
Wakiwa chumba cha manesi huku manesi wakiwa hawapo ofisini.
Walipofika Mapokezi, pamoja na kuonekana mgonjwa kuwa na hali mbaya, wahudumu hawakumpa kipaumbele na kuendelea kuwahudumia wagonjwa wengine kwa foleni ambao hawakuonekana kuwa ‘serious’ sana.
Mgonjwa akiwa amelalala kwenye benchi kusubiri huduma.
Baada ya dakika 12 kupita bila msaada, mpelelezi mmoja wa OFMaliyejifanya ni mwanafunzi mwenzake na mgonjwa, alikwenda dirishani kuomba kuandikiwa kadi haraka ili aende kwa daktari, akapewa.
FOLENI NDEFU, HAKUNA DAKTARI
Mapaparazi wa OFMwakiwa na mgonjwa wao kwenye baiskeli ya wagonjwa, walifika kwenye foleni iliyokuwa na watu wengi wanaohitaji kuingia kwa daktari lakini hakuwepo ofisini kwake, zilipita dakika 14 ndipo akatokea.
Hata hivyo manesi waliokuwa wakirandaranda kwenye korido hawakutoa msaada wowote kwa wagonjwa waliokuwa wanamsubiri daktari.
MAIGIZO CHUMBANI KWA DAKTARI
Mgonjwa akionekana kuzidiwa sana (alipatia kweli kuigiza mgonjwa!) alimweleza daktari kuwa alikuwa akisumbuliwa na maumivu makali mwilini, viungo kufa ganzi na shida katika mfumo wa upumuaji.
Hata hivyo, mgonjwa huyo alimweleza daktari kuwa hali hiyo ilimpata ghafla akiwa na wenzake chuoni, haikuwahi kumtokea kabla.
Baada ya kumpima shinikizo la damu, mgonjwa huyo alionekana yupo katika hali ya kawaida, kipimo kilisoma 110/70 mmHg.
TIBABILAVIPIMO
Katika hali ya kushangaza daktari huyo, bila kumpima mgonjwa ili kuthibitisha anachoumwa, aliagiza kwanza achomwe haraka sindano mbili – Diclofenac (ya maumivu) na Hydrocortisone (ya kutuliza maumivu ya kifua).
Kwa msaada wa wenzake, mgonjwa huyo alipelekwa chumba cha sindano na kukubali kuchomwa sindano ya Declofenac kwa vile walijua ni ya maumivu tu lakini wakagoma mgonjwa wao asichomwe ile nyingine mpaka watakapopewa maelezo inatibu ugonjwa gani.
MAABARA
Baada ya kuchomwa sindano hizo alitakiwa kuelekea maabara kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa vipimo mbalimbali ikiwemo cha malaria ambacho kitaalamu kiliandikwa RDT (Rapid Diagnostic Test for Malaria) na RPG.
Mapaparazi wetu walishuhudia wagonjwa wengi wakiwa kwenye foleni huku wengine wakiwa na hali mbaya kwenye baiskeli za wagonjwa wakisubiri huduma.
Paparazi wetu alilazimika kujilaza kwenye fomu katika foleni na kusubiri hapo kwa takribani nusu saa ndipo alipochukuliwa vipimo na kuletewa majibu baadaye yaliyoonyesha hakuwa na ugonjwa wowote.
Kwa kuwa kazi ilikuwa imeshakamilika, mapaparazi wetu hawakuona sababu ya kurudi kwa daktari, walitokomea zao mitaani na mgonjwa feki wao ambaye alionekana kuanza kupata nafuu.
MGANGA MKUU KIKAANGONI
Alhamisi, Aprili 24, mwaka huu, mishale ya saa 6:30 mchana, mmoja wa makachero wa OFMalifika hospitalini hapo na kuonana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Palestina, Dk. Benedict Luoga ili azungumzie tuhuma hizo.
Baada ya kusikiliza madai hayo, Dk. Luoga alikataa kuzungumza kwa maelezo kuwa yeye siyo msemaji, badala yake akamwelekeza mwandishi huyo kwenda kwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Dk. Gunini Kamba aliyedai ndiye msemaji.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate