EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 26, 2014

BABA AHUSISHWA KIFO CHA DENTI MWANZA!

Mwili wa marehemu Anastazia Lackfordukiagwa kabla ya kwenda kuzikwa.
Mwili wa marehemu Anastazia Lackford ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanza, umezikwa juzi katika makaburi ya Lunala, Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza lakini simulizi ya baba mzazi wa marehemu, Lackford Magafu kuhusishwa na kifo cha mwanaye inashangaza!
Kabla ya kifo.

Mwili wa marehemu Anastazia Lackfordukiwa kwenye jeneza
Inadaiwa kuwa, Machi 27, mwaka huu baba wa marehemu, Magafu alimpiga sana mtoto huyo kwa madai ya kutopika chakula kwa wakati.
Ilizidi kudaiwa kuwa, mbali na kipigo hicho mzazi huyo alimmwagia mafuta ya taa na kumchoma moto, hali iliyomsababishia majeraha mwilini.
“Baada ya ukatili huo, baba huyo alimchukua Anastazia na kwenda naye Kituo cha Polisi cha Igogo ambako alidanganya kuwa, mwanaye alilipukiwa na jiko, uongo ambao marehemu aliukubali ili kumuokoa baba yake,” kilidai chanzo kilichoomba hifadhi ya jina lake.
Ikaelezwa kuwa, mtoto huyo alipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana, Butimba, baadaye Sekou Toure kabla ya kupelekwa Bugando na kulazwa wodi ya wagonjwa mahututi, wanaohitaji uangalizi maalum (ICU).
Chanzo cha kifo
Hata hivyo, kifo cha Anastazia kilichotokea Aprili 16, mwaka huu hakijathibitishwa kimesababishwa na majeraha yaliyotokana na moto au kinachodaiwa kuwa ni sumu iliyowekwa kwenye juisi inayodaiwa kupelekwa na Magafu wakati marehemu alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Bugando.
Mmoja wa watu waliokuwa wakimuuguza Anastazia (jina linahifadhiwa) alidai kuwa, siku hiyo Magafu alipeleka juisi hiyo na baada ya mgonjwa kuinywa alianza kujisikia vibaya.
Awali, Anastazia aligoma kuinywa juisi hiyo kana kwamba alihisi kitu lakini baada ya kulazimishwa aliinywa kwa shingo upande.
“Baba yake alipoondoka tu, Anastazia akaanza kujihisi vibaya, akawa anatapika mabonge mabonge ya vitu vyeusi.
“Nilipompigia simu baba yake na kumwambia hali ya mgonjwa na kumuuliza kama juisi ile alitengeneza mwenyewe, amenunua au amepewa, alinijibu kuwa ametengeneza yeye.
“Akaniambia nisimwambie mtu lakini nikaona ni bora kuwaambie ndugu zake na wauguzi, haikuchukua muda mrefu mgonjwa akawa amefariki,” alidai mtoa habari huyo bila kueleza chanzo hasa cha kifo hicho.
Akizungumzia kifo cha mwanaye, mama mdogo wa marehemu, Nongwa Gilbert alisema hana cha kusema bali anamwachia Mungu.
“Nimeshazungumza sana hadi nimechoka, kilichobaki namwachia Mungu maana hata nikizungumza sitaweza kumrudisha,” alisema Nongwa.
Hadi sasa Magafu anashikiliwa na jeshi la polisi jijini Mwanza na kuhusu juisi aliyopewa Anastazia kusababisha kifo chake, Kamanda wa Polisi Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Valentino Mulowola alisema:
“Uchunguzi ulifanyika, lakini majibu bado yanasubiriwa kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ambaye amepelekewa sampuli kwa uchunguzi wa kisayansi. Suala la mtuhumiwa kufikishwa mahakamani ni uamuzi wa Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP).”
Marehemu alizaliwa Januari 30,1997, alisoma Shule ya Msingi Kirumba kuanzia mwaka 2004, akajiunga Shule ya Sekondari Mwanza mwaka 2011. Hadi anafariki dunia alikuwa kidato cha tatu akichukua masomo ya sanaa.
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi-Amin.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate