Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiangalia mto Malagalasi ambao ni
mpaka kati ya Tanzania na Burundi alipokuwa katika ziara wilayani
Buhigwe mkoani Kigoma leo Alhamisi, Aprili 10, 2014. Kinana yupo katika
ziara ya siku tano mkoani humo ya kukagua uhai wa Chama na kusikiliza
kero za wananchi mkoani humo. Moja ya kero kwenye mpaka huo
unaokutanisha vijiji vya Kibande (Tanzania) na Murambi(Burundi) ni
Watanzania kulazimika kukumbana na adha ya kuvuka mto huo kwenda kufanya
biashara na kununua mahitaji kwenye soko lililopo upande wa Burundi. Wa
pili kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
Kinana
akitazama mpaka huo na namna wananchi walivyokuwa wakivuka na wengine
kuvushwa kwenye mto wa Malagarasi wakitoka Burundi kuingia Tanzania
Eneo
la soko la Murambi, Burundi ambako Watanzania hulazimika kwenda
kufanyabiashara na kupata mahitaji huko kutokana na upande wa nchi yao
kutokuwa na soko ikiwemo la mifugo lililokuwepo zamani na sasa halipo
kutokana na kufungwa kwa sababu zisizojulikana, ambaopo Kinana alihoji
kwa nini lisiwepo soko upande wa Tanzania ili kuondoa kero ya watu
kuvuka mto kila siku kwenda ng'ambo.
Katibu
wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa pembezoni mwa mto
Malagarasi, mpakani mwa Tanzania na Burundi wakati wa ziara hiyo.
Juu ya maelezo haya ni wananchi wakivuka mto Malagarasi kutoka upande wa Burundi kuingia Tanzania
Baadhi
ya wananchi wa Burundi wakiwa wameingia Tanzania baada ya kuvuka mto
huo kwa taabu, baadhi yao wameomba serikali za nchi hizo kujenga daraja
kwenye mto huo kurahisisha uvukaji
Wananchi
wa Kijiji cha Buhigwe wakimlaki Kinana alipowasili kwenye Ofisi ya CCM
Kata ya Buhigwe, kuzungumza na Kamati ya Siasa ya CCM wilayani humo, leo
Kinana
akizungumza na wananchi hao baada ya kumaliza kuzungumza na Kamati hiyo
ya siasa. Kulia ni Mbunge wa Buhingwe maarufu kwa jina la Obama
Katibu Mkuu wa CCm Abdulrahman Kinana akipokea zawadi mbalimbali kutoka kwa wananchi wa Buhigwe wakati wa mkutano huo
No comments:
Post a Comment