EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 8, 2014

MASHINDANO YA SANAA, KUCHORA KWA WATOTO NA VIJANA KATI YA UMRI WA MIAKA 7 HADI 15


Amsha ubunifu wako!
Benki ya Dunia inawakaribisha watoto wa shule wa Kitanzania ambao ni wabunifu wenye umri kati ya miaka 7 hadi 15 kushiriki katika mashindano ya sanaa / kuchora, ambapo mchoro utakaoshinda utatumika kupamba jalada la mbele la Ripoti muhimu ya Benki ya Dunia kuhusu Tanzania.
Kaulimbiu ya shindano hili ni ‘Kazi kwa Watanzania Wote.’
Ni nani anaweza kuingia shindano hili?
Shindano liko wazi kwa watoto wote wa shule wa Kitanzania, wabunifu walio kati ya miaka 7 hadi 15.

Ninaingiaje kwenye shindano hili?
Unatakiwa kutumia mikono yako tu basi! Unaweza kuchora, kupaka rangi na michoro ya haraka haraka. Unaweza  kutumia peni, penseli, penseli ya rangi, mkaa, rangi ya mafuta, rangi za kikemikali (akriliki) au rangi za maji kutengeneza mchoro wako. Jaribu kuwa mbunifu, na tumia mawazo yako na fikra ili upate mchoro utakaofafanua kaulimbiu hii, ‘Kazi kwa Watanzania Wote.’

Je, naweza kushirikiana na mtu mwingine?
Ndio, unaweza kushiriki aidha kama mtu binafsi au kama timu (iliyo na watu wasiozidi 3).
Kipindi cha Shindano
Shindano linaanza tarehe 17 Machi 2014 na kuishia tarehe 17 Aprili 2014.
Je, kuna zawadi zozote za kushindaniwa?
Ndiyo! Mshindi atajinyakulia Shilingi Milioni Moja (1,000,000) na fursa kwa picha yake na maelezo ya maisha yake kutumika kupamba jalada la ndani la ripoti. Mshindi wa Pili atapata Shilingi 650,000; wakati Mshindi wa Tatu atapata Shilingi 350,000. Kila mshindi atapata shahada ya kutambuliwa kutoka Benki ya Dunia.
Nina maswali zaidi …
Endelea na yatume kwa barua pepe: unleash@worldbank.org na yatajibiwa ndani ya masaa 24 kama yatatumwa siku za kazi.

Sheria na Miongozo

1. Rika: Watoto wa shule kati ya umri wa miaka 7 hadi 15.

2. Ukubwa wa mchoro: Mchoro lazima ufanyike kwenye karatasi ya ukubwa wa A4 au A3.

3. Majina na Mawasiliano: Jina kamili, umri (siku, mwezi, na mwaka wa kuzaliwa), jinsi, na anuani kamili ikijumuisha namba ya simu na barua pepe (kama ipo) lazima iandikwe nyuma ya mchoro, na SIO juu ya mchoro.
4. Aina ya uchoraji: Unaweza kutumia mikono yako tu. Unaweza kuchora, kupaka rangi na michoro ya haraka haraka; tumia peni, penseli, penseli ya rangi, mkaa, rangi ya mafuta, rangi za kikemikali (akriliki) au rangi za maji.

5. Masharti ya kukubalika:
a) Kazi ambazo zimeonyeshwa au kukubaliwa sehemu nyingine hazitakubalika katika shindano hili.
b) Kazi ambazo zinaonyesha mtu maalumu, shirika au jina la biashara hazitakubaliwa.
c) Michoro iwasilishwe kupitia posta au kutumwa kupitia kampuni za kusafirisha vifurushi kabla ya tarehe ya mwisho ambayo ni tarehe 17 Aprili 2014.
d) Michoro inatakiwa ipokelewe siku ya tarehe 17 Aprili 2014 au kabla.
e) Mchoro usiwe na maandishi au maelezo yoyote.

6. Aina ya mchoro unaokubalika: Nakala za michoro zilizoko kwenye karatasi au zilizotumwa kwa mtandao tu ndizo zitakazokubaliwa, ambazo hazina maneno wala maelezo. (*Angalia hapo chini)

7. Idadi ya michoro inayokubalika: Washiriki wanaweza kuwasilisha mchoro mmoja tu.

8.Watoto na ndugu wa wafanyakazi wa Benki ya Dunia hawaruhusiwi kushiriki katika shindano hili.

TAFADHALI ZINGATIA YAFUATAYO:
HATIMILIKI  
Michoro lazima iwe ya asili na isiyonukuliwa kutoka sehemu nyingine kwa njia yoyote ile. Benki ya Dunia itakuwa na mamlaka juu ya hatimiliki zote za michoro iliyoshinda. Tuhuma za kuiba au kunukuu mchoro zitakuwa ni jukumu la mshindani pekee.

KUTANGAZWA KWA WASHINDI
Washindi wa shindano watatangazwa ndani ya wiki mbili baada ya tarahe ya mwisho ya kuwasilisha mchoro.

UWASILISHAJI
Tafadhali lete au tuma barua pepe ya wasilisho lako kabla au ifikapo tarehe 17 Aprili 2014 kwa anuani ifuatayo:

SHINDANO LA SANAA / KUCHORA
Benki ya Dunia
Mtaa wa Mirambo Na. 50
Dar es Salaam
Tanzania
Barua pepe: unleash@worldbank.org

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate