EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 1, 2014

NAAPA: WANANCHI HAWAJAWAHI KUTAKA KATIBA MPYA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
WABUNGE wa Bunge Maalum la Katiba wanaokutana mjini Dodoma kujadili namna ya kupata Katiba Mpya wamekuwa wakijinasibu kuwa, wanawawakilisha wananchi wa Tanzania katika kupata katiba iliyo bora.
Unaweza kuwepo uongo, lakini huu wa kuwasingizia Watanzania kuhusu kupatikana kwa Katiba Mpya ni uongo mkubwa ambao sijui wanaouanzisha wana malengo gani na taifa hili? Nikiulizwa kwa nini? Nitasema kwa kiapo kuwa, hakuna Mtanzania halisi aliyewahi kuwa na haja ya kupatikana kwa Katiba Mpya!
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe
Mwenye kunihoji kuhusu Watanzania halisi ninaowazungumzia, nitamwelewesha kuwa ni wale waishio vijijini na waliopo mjini ambao wamekosa fursa ya kupata elimu bora ya kuwawezesha kujitambua.
Mwananchi halisi ninayemzungumzia hawezi kuwa Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda, si Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe wala Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, ni Mwanamangwengwe wa Itaga mkoani Tabora ambaye hajui kusoma wala kuandika sambamba na familia yake yote.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana,
Anayekubaliana nami katika hili aitike: ‘Amini’, kwa kuwa nchi hii wananchi wake walio wengi ni wale wa kutoka katika kundi la Mwanamangwengwe wala si la akina Kinana. Kama ni sahihi, anayesema anawawakilisha wananchi lazima awe amepata kibali kutoka kwa wapwa zangu wa Ujiji mkoani Kigoma na si wakazi wa Msasani kwa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Najiuliza,“ni lini wanasiasa wametumwa kutafuta Katiba Mpya badala ya kuwaletea wananchi maendeleo?” Swali la nyongeza anawezaje mtu kukutuma kitu kipya wakati hata kile cha zamani hakifahamu?
Acheni kucheza na akili za watu ninyi binadamu! Haiwezekani mkutane Dodoma na kauli mbiu ya kuwatungia Watanzania Katiba Mpya wakati ile ya zamani mliwanyima fursa ya kuitambua na kiukweli wananchi walio wengi hawaifahamu kabisa.

Ikiwa ni hivyo, katiba ya zamani imewakera nini mpaka watake mpya? Ukisikiliza vimbwanga vya ‘wanjanja wa kisiasa’ utasikia wakisema: “tumewahoji wananchi kadhaa na wengi kati yao wametaka Muundo wa Serikali Tatu,

” hivi wananchi kutaka Muundo wa Serikali Tatu au Mbili ndiyo kutaka Katiba Mpya? Utoto kabisa huu! Kwa kuwa kila Mwanasiasa ameshatambua udhaifu wa wananchi, basi kila mmoja vazi lake ni kutumwa na wananchi.

Kila siku vinaibuka vikundi na mangenge ya kila aina yanayoundwa ndani na nje ya bunge yakijifanya kutafuta katiba ya wananchi, aliyewatuma ni nani? Nashauri, kama wanasiasa wameshindwa kuwafanya
Watanzania kuwa na maisha bora na umoja wa kitaifa ni heri wasichume majanga ambayo naamini hawatayala na familia zao. Tuachane na ujanja wa senene. Nachochea bunge la katiba ni la wanasiasa si la wananchi!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate