EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, April 1, 2014

TANZANIA NI ZAIDI YA SERIKALI 2/3

Mwenyekiti wa bunge la Katiba, Samweli sita.
NIANZE kwa kulitaja kwa fahari kubwa jina la Mwenyezi Mungu, Baba muweza wa kila jambo, kwa kutuwezesha kuwa wazima wa afya, ambao leo kwa mara nyingine, tunakutana katika ukurasa wetu huu wa kubadilishana mawazo mawili matatu.
Baada ya malumbano ya zaidi ya mwezi mzima ya jinsi gani upigaji kura utakuwa wakati wa kupitisha rasimu ya katiba katika Bunge Maalum, hatimaye ufumbuzi umepatikana kwamba sasa wajumbe watakuwa huru kuamua aina ya upigaji wake wa kura, iwe kwa siri au wazi.

Sasa kazi rasmi ya kupitisha rasimu inaanza kwa kamati zilizoundwa na Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kuanza kupitia kifungu kwa kifungu, mstari kwa mstari na neno kwa neno ili baadaye wawasilishe makubaliano ya wajumbe wa kamati hizo mbele ya Bunge Maalum kwa makubaliano ya pamoja.

Katika siku hizo za mvutano wa kanuni za kuendesha bunge hili maalum, mambo mengi sana yalijitokeza na kuleta majibizano ya maneno baina ya wajumbe wa chama tawala na wale wa kutoka upinzani kuhusiana na masuala mbalimbali, lakini zaidi yakiwa ni kuhusu aina ya muundo wa Muungano, uwe wa serikali moja, mbili au tatu.

Kimsingi, suala hili linalohusu Muungano, ndilo hasa lililosababisha mvutano wa aina ya upigaji kura, kwani inavyoonekana watu wamepania sana kulijadili suala hili, kitu ambacho ni kizuri kutokana na umuhimu wake.
Ninajua watu wengi sana wangependa kuona hatima ya majadiliano ya wabunge wetu kuhusu katiba mpya, wanasubiri kusikia wawakilishi hao watatoa aina gani ya katiba ili wananchi waipigie kura ya maoni. Mjadala mkubwa kwa idadi kubwa ya watu ni kujua kama muungano wetu utakuwa ni ule wa serikali mbili kama ilivyo sasa au tatu.

Binafsi, sina tatizo kabisa na aina ya muungano, uwe wa serikali moja, mbili au tatu. Kwangu mimi kitu cha kwanza ambacho nisingependa kipotee ni Tanzania. Nimezaliwa katika nchi yenye jina hili, nimekulia hapa na kwa kweli ninaipenda sana.

Nina uhakika hakuna anayeitakia mabaya nchi yetu, isipokuwa tu, tunatofautiana mawazo juu ya namna gani tuiendeshe. Sina tatizo na tofauti hizi za kimtazamo, kwa sababu hatuwezi kuendelea bila kufikiri tofauti.

Rai yangu kwa wajumbe wa bunge hili maalum ni kwamba umma wote wa Watanzania, macho yao yako kwenu, hawa wote wanawategemea kuwa mtafanya kila kilicho ndani ya uwezo wenu, kuhakikisha nchi yao inabaki salama, iliyo moja na yenye mshikamano zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Kama nilivyowahi kusema huko nyuma, siku mtakayoondoka hapo ndani ya jengo hilo tukufu na baadhi yenu wakashangilia kwamba wameshinda, basi ni lazima tujue kuwa katiba iliyopatikana siyo bora. Tunataka wajumbe wote wafanye kazi na siku ya mwisho, wote muwe na tabasamu, hata kama hamtakubaliana kwa kila jambo.

Nchi inahitaji mambo mengi zaidi ya uwepo wa serikali tunazopigania. Watu wetu ni maskini na wengi wanakosa haki zao za msingi. Ni wajibu wa wajumbe kuangalia jinsi gani vizazi vyetu, vya sasa na baadaye vitaishi katika nchi nzuri na yenye rasilimali nyingi kwa amani, utulivu, upendo na mshikamano, kama ambavyo waasisi wa taifa letu walivyotaka.

Waasisi wa taifa letu, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Abeid Karume enzi za uhai wao, walikuwa wakisisitiza sana umoja wa kitaifa na kudumisha amani kwani walielewa sehemu yoyote isipokuwa na amani siyo rahisi kuwa na maendeleo.

Kama ambavyo Rais Jakaya Kikwete anavyosema mara kwa mara, wote tuna dhamira ya kuijenga nchi yetu, hatuwezi kugombea fito. Kila kifungu cha katiba kitakachopitishwa, lazima kilenge kuiboresha Tanzania. Tuwe wakali kwa yeyote mwenye nia ya kututenganisha, bila kujali cheo chake, kwa sababu kama nilivyosema mwanzo, taifa kwanza, vyama baadaye!
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate