EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 16, 2014

TFF yafuta usajili wa Domayo

Kiungo mkabaji, Frank Domayo alipokuwa akisaini mkataba na timu ya Azam FC.
Mohammed Mdose na Said Ally
MAMBO yanazidi kuwa mambo kwenye usajili wa Ligi Kuu Tanzania Bara! Wakati Azam FC ikiwa imejihakikishia kumtumia kiungo mkabaji, Frank Domayo kuanzia msimu wa 2014-2015, tamko zito limetolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya usajili huo.
TFF imetoa tamko kuwa mpaka sasa bado haiutambua usajili wa kiungo huyo kutoka Yanga kwenda Azam FC, ikiwa na maana kuwa kwa TFF husajili huo haupo.

Shirikisho hilo limesema kuwa usajili huo kutambulika au kutotambulika itajulikana mara baada ya majibu ya ripoti ya uchunguzi wa usajili huo itakapopitiwa na kutolewa ufafanuzi, ambapo mpaka sasa ipo mezani kwao ikiwa imekamilika.
Ufafanuzi huo umetolewa na Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine ambaye amesema kuwa TFF haijapitisha wala kutambua usajili huo kwa kuwa ulikuwa ukisubiri ripoti ya uchunguzi wa Domayo ambaye inadaiwa alisajiliwa na Azam wakati akiwa kambini kwenye timu ya taifa, Taifa Stars, Tukuyu mkoani Mbeya, wiki kadhaa zilizopita.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Mwesigwa alisema uchunguzi zaidi ulikuwa ukifanyika kama ilivyoagizwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi, lakini akasisitiza kuwa tayari umeshakamilika na kilichobakia ni kupitiwa kisha kutolewa maamuzi kama Azam walikiuka kanuni au walikuwa sahihi kwa huo mchakato wao wa kutaka kumsajili Domayo akiwa ndani ya majukumu ya Stars.
“Suala la Domayo ni jambo kubwa na la kisheria, hivyo hatuwezi kulichukulia kirahisi, tulitoa muda wa siku 14 kufanyika kwa uchunguzi kwa ajili ya mwanasheria wetu kulifanyia kazi.
“Kwa sasa hatuwezi kulizungumzia mpaka pale ripoti itakapotolewa, kwani tayari ameshaikamilika na ameiwasilisha, kilichobaki ni kupitiwa na kutolewa maamuzi sahihi juu ya kilichotokea siku husika,” alisema Mwesigwa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate